Namhifadhi kulala pamoja na chakula lakini ni mvivu kwenda kwenye vibarua. Nifanye nini?

Namhifadhi kulala pamoja na chakula lakini ni mvivu kwenda kwenye vibarua. Nifanye nini?

Gemini Are Forever

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2019
Posts
1,508
Reaction score
2,619
Za kwenu!

Nipo mkoa fulani kikazi. Na nina ndugu yangu, mtoto wa Shangazi amekuja huku kikazi na nimempokea kama ndugu yangu. Namhifadhi kulala pamoja na kula.

Kinachonikera kwake ni uvivu. Vibarua vipo sio haba endapo ukiwa na bidii, na huko kwenye vibarua anaweza kwenda na akapata chakula huko huko (ukibahatika) na kupunguza gharama za chakula either kwake au kwangu.

Mimi kila siku naenda kazini ila yeye amekuwa mtu wa kulala tu na kuzurura.

Kuna mgahawa nimempeleka awe anaenda kula then nije kulipa ikiwa siku amekosa kibarua lakini imekuwa kigezo cha yeye kutojishughulisha (pengine kwa sababu ana uhakika wa kula na kulala).

Amekuwa analala, akiamka asubuhi anaenda pale mgahawani anakula, anaingia vijiwe vya drafti, vibanda umiza n.k.

Kiukweli wakuu ananipa gharama za chakula sana na ukizingatia kuna vibarua angefanya tu na kujiingizia angalau visenti pamoja na kula.

Je, nimfanyaje huyu wakuu maana ni kama yupo nyumbani kwa Baba yake amesahau kuwa tumekuja kupambana?
 
Amekuja kwa ajili ya kazi,sawa

Sometimes ni ngumu kwa baadhi ya watu kuendana na mazingira ikiwa unafahamu ajira/vibarua ni changamoto ila kwakuwa wewe mwenyeji na umesema fursa hizo zinapatikana kwa wingi basi Kaa chini uongee naye
 
Mkuu, unamwendekeza mwenyewe. Kama vipi mtafutie kibarua au mfungulie kimradi, vinginevyo anaweza kulemaa hadi uzeeni hadi ataoa na kuzaa watoto hapohapo kwako, maana sponsor upo maumivu ya nini.
Mkuu, unaweza kumtafutia kibarua lakini amekuwa akikwepa, mara aseme hajisikii vizuri, mara kachelewa...! yaan atafanya kila analoweza ili mradi tu asiende kibaruani halafu baadae unamkuta vijiweni.
 
Za kwenu!

Nipo mkoa fulani kikazi. Na nina ndugu yangu, mtoto wa Shangazi amekuja huku kikazi na nimempokea kama ndugu yangu. Namhifadhi kulala pamoja na kula.
Anachofanya ndugu yako ni makosa ila pia wewe ni mnafiki sana; na chances ni kwamba ukiendelea kuwa kama ulivyo sasa, wewe ndiyo utakuja ufanye makosa makubwa yatakaypoelekea kuonekana wewe ndiyo una matatizo na si huyo ndugu yako. Kuwa wazi kwake umweleze na atakuelewa.

Asipokuelewa kwa maswala ya msingi na mbele ya mashuhuda wengine au mbele ya watu wengine, wajulishe wazazi nyumbani halafu mfukuze nyumbani kwako
 
Pole sana. Kuna post moja humu sikumbuki ila mwandishi ameandika "usiwasaidie maskini acha wafe". Nikiipata nitakupa link usome.
Siwezi kumwona akifa mkuu maana nilikubali mwenyewe aje. Ninachotaka hapa ni ipi njia nzuri ya kumrudisha aende nyumbani akafie huko?
 
Are you serious Paula? nilikuwa na mpango wa kukuomba japo dola buku.....basi umeshanikata maini kwa hii comment yako😂
Mimi nimekumbuka tu hiyo post, Nyumisi. Bado sijamshauri OP.
Njoo chukua tu hizo dollars.
 
Mkuu, unaweza kumtafutia kibarua lakini amekuwa akikwepa, mara aseme hajisikii vizuri, mara kachelewa...! yaan atafanya kila analoweza ili mradi tu asiende kibaruani halafu baadae unamkuta vijiweni.
Mtimue, usimdekeze
 
Mi naona kama alikuja kwa mpango maalumu wa kutafuta maisha na yeye hatafuti maisha basi mrudishe ulipomtoa.

Sioni sababu ya muhimu wewe kulalamika.huko alipotoka alikuwa hali chakula? Yeye ni yatima? Ana umri gani?elimu? Ujuzi gani?
 
Za kwenu!

Nipo mkoa fulani kikazi. Na nina ndugu yangu, mtoto wa Shangazi amekuja huku kikazi na nimempokea kama ndugu yangu. Namhifadhi kulala pamoja na kula.

Kinachonikera kwake ni uvivu. Vibarua vipo sio haba endapo ukiwa na bidii, na huko kwenye vibarua anaweza kwenda na akapata chakula huko huko (ukibahatika) na kupunguza gharama za chakula either kwake au kwangu.

Mimi kila siku naenda kazini ila yeye amekuwa mtu wa kulala tu na kuzurura.

Kuna mgahawa nimempeleka awe anaenda kula then nije kulipa ikiwa siku amekosa kibarua lakini imekuwa kigezo cha yeye kutojishughulisha (pengine kwa sababu ana uhakika wa kula na kulala).

Amekuwa analala, akiamka asubuhi anaenda pale mgahawani anakula, anaingia vijiwe vya drafti, vibanda umiza n.k.

Kiukweli wakuu ananipa gharama za chakula sana na ukizingatia kuna vibarua angefanya tu na kujiingizia angalau visenti pamoja na kula.

Je, nimfanyaje huyu wakuu maana ni kama yupo nyumbani kwa Baba yake amesahau kuwa tumekuja kupambana?
Chalii wa moro ww au sio?
 
Dah umenikumbusha stori za huko kwetu br.
Ndugu yangu mmoja yeye ana 40 watoto 5 but hajui kujitegemea. Maisha yake yote alizoeshwa kutokujitegemea. Sijui hii ilitokea kwa bahati mbaya ama vipi.
Hadi 200 ya shule kwa wanae hawezi. Watoto wanamcheki Bibi yao na Ni wengi ( bi mkubwa wangu) yaani Ni mtihani.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom