Namhifadhi kulala pamoja na chakula lakini ni mvivu kwenda kwenye vibarua. Nifanye nini?

Namhifadhi kulala pamoja na chakula lakini ni mvivu kwenda kwenye vibarua. Nifanye nini?

Kaa nae kwa upendo umieleweshe kuwa anavyokaa bila kujishughulisha anapoteza muda na aelewe kuwa maisha ni magumu.Mwambie kuwa hata wewe unatamani kushinda nyumbani ila haiwezekani.Muweke wazi kuwa msaada wa kula na kulala unampa kwa sababu yeye ni ndugu yako na si kwa sababu unajiweza sana na pia ajue leo upo kesho haupo,leo unaweza kumsaidia kesho unaweza ukakwama ukashindwa kumsaidia.Msaidie kwa kutia chachu ya kutamani kufanikiwa na ikishindikana ndio umrudishe nyumbani.
 
Za kwenu!

Nipo mkoa fulani kikazi. Na nina ndugu yangu, mtoto wa Shangazi amekuja huku kikazi na nimempokea kama ndugu yangu. Namhifadhi kulala pamoja na kula.

Kinachonikera kwake ni uvivu. Vibarua vipo sio haba endapo ukiwa na bidii, na huko kwenye vibarua anaweza kwenda na akapata chakula huko huko (ukibahatika) na kupunguza gharama za chakula either kwake au kwangu.

Mimi kila siku naenda kazini ila yeye amekuwa mtu wa kulala tu na kuzurura.

Kuna mgahawa nimempeleka awe anaenda kula then nije kulipa ikiwa siku amekosa kibarua lakini imekuwa kigezo cha yeye kutojishughulisha (pengine kwa sababu ana uhakika wa kula na kulala).

Amekuwa analala, akiamka asubuhi anaenda pale mgahawani anakula, anaingia vijiwe vya drafti, vibanda umiza n.k.

Kiukweli wakuu ananipa gharama za chakula sana na ukizingatia kuna vibarua angefanya tu na kujiingizia angalau visenti pamoja na kula.

Je, nimfanyaje huyu wakuu maana ni kama yupo nyumbani kwa Baba yake amesahau kuwa tumekuja kupambana?
Mwambie awe anapika nyumbani kupinguza gharama za kula mgahawani
 
Sio Yale makabila ya mungu ndio anajua. Kufanya kazi mtihani hayo. Sijui tuyasaidie vip walahi. Sio watu wa pwani huyo?
Pwani hamna uvivu usikariri kama unabisha mwambie ataje hilo kabila kama la pwani?
 
Za kwenu!

Nipo mkoa fulani kikazi. Na nina ndugu yangu, mtoto wa Shangazi amekuja huku kikazi na nimempokea kama ndugu yangu. Namhifadhi kulala pamoja na kula.

Kinachonikera kwake ni uvivu. Vibarua vipo sio haba endapo ukiwa na bidii, na huko kwenye vibarua anaweza kwenda na akapata chakula huko huko (ukibahatika) na kupunguza gharama za chakula either kwake au kwangu.

Mimi kila siku naenda kazini ila yeye amekuwa mtu wa kulala tu na kuzurura.

Kuna mgahawa nimempeleka awe anaenda kula then nije kulipa ikiwa siku amekosa kibarua lakini imekuwa kigezo cha yeye kutojishughulisha (pengine kwa sababu ana uhakika wa kula na kulala).

Amekuwa analala, akiamka asubuhi anaenda pale mgahawani anakula, anaingia vijiwe vya drafti, vibanda umiza n.k.

Kiukweli wakuu ananipa gharama za chakula sana na ukizingatia kuna vibarua angefanya tu na kujiingizia angalau visenti pamoja na kula.

Je, nimfanyaje huyu wakuu maana ni kama yupo nyumbani kwa Baba yake amesahau kuwa tumekuja kupambana?
Mfukuze
 
Kata kulipa pesa ya msosi hapo mgahawani weka jiko home na mazagazaga ya kupika yasiwe yale ya vinono mdogo mdogo unakua unapunguza mahitaji atazinduka tu
 
Pole sana. Kuna wakati ukweli unasaidia sana kujenga,suala hapo ni kumwambia ukweli tu.
 
Angekuwa wa kike ungenipata assist angekaa kwangu bure [emoji3]ila nikimchoka nakurudishia
 
Mshike mkono mkatafute wote kazi, akikataa au kufukuzwa kazi , chukua funguo za nyumba mpe nauli na hela ya kula njiani arudi alipotoka
 
Huyo ni mvivu na unamlea ndio maana anakuonea na kukutesa. Watu wavivu furaha yao ni kuona wengine wanateseka kwaajiri yao huku wakitumia chochote kinachotafutwa na mwengine bila kuwazia gharama yake.


Sasa huyo ndugu yako kaa nae kitako na umueleze kuwa hapo umempatia hifadhi ya muda si ya kudumu hivyo asijirahisi sana akachukulia maisha ni kujiachia na kufanya anavyojisikia na uvivu wake.

Mtafutie shughuli ya kufanya ili aanze kuwajibika na maisha yake. Ukiendelea kukaa kimya haumsaidii na unamuongezea tatizo.
 
Kaa nae kwa upendo umieleweshe kuwa anavyokaa bila kujishughulisha anapoteza muda na aelewe kuwa maisha ni magumu.Mwambie kuwa hata wewe unatamani kushinda nyumbani ila haiwezekani.Muweke wazi kuwa msaada wa kula na kulala unampa kwa sababu yeye ni ndugu yako na si kwa sababu unajiweza sana na pia ajue leo upo kesho haupo,leo unaweza kumsaidia kesho unaweza ukakwama ukashindwa kumsaidia.Msaidie kwa kutia chachu ya kutamani kufanikiwa na ikishindikana ndio umrudishe nyumbani.
Mtu wa tanga ww
 
Back
Top Bottom