Namna ambavyo watoto wa kike wanavyoandaliwa kuwa viongozi wakiwa skulini

Namna ambavyo watoto wa kike wanavyoandaliwa kuwa viongozi wakiwa skulini

Nusra Shaaban

New Member
Joined
Oct 8, 2024
Posts
2
Reaction score
1
anaongeza kuwa klabu za uongozi ni msingi wakuwajenga wasichana kujiamini na kuwa viongozi wa baadaye.

Kwa Skuli ya Benmbella, Mwalimu Bakari Mohammed anaeleza kuwa uchaguzi wa serikali za wanafunzi unawahamasisha watoto kujiamini. Rais wa wanafunzi huchagua baraza lake la mawaziri na kushiriki kikamilifu katika utawala wa shule.

Mtazamo wa Wazazi Katika Kukuza Viongozi wa Baadaye

Wazazi wana nafasi muhimu katika kuandaa watoto wa kike kuwa viongozi. Leyla Salum Juma, mzazi wa mwanafunzi wa Skuli ya Memon, anasema, "Watoto wasasa wanajitambua zaidi. Kama wazazi, ni jukumu letu kuwaunga mkono na kuhakikisha tunawapa matumaini katika ndoto zao."

Mwanakheri Mohamed Ali, mzazi mwingine, anahimiza wazazi kuwahoji watoto wao kuhusu ndoto zao za baadaye na kuwapa nafasi za kujifunza. "Watoto wote wanahitaji wasikilizwe. Tuwatie moyo katika malengo yao," alisema.
Jitihada za Serikali na Wizara ya Elimu

Afisa Elimu wa Wilaya ya Mjini, Hassan Abbass Hassan, anaeleza kuwa jitihada mbalimbali zinafanyika kupitia miongozo ya walimu na serikali za wanafunzi. "Hatujawahi kuwa na mwongozo rasmi wakukuza uongozi kwa watoto wa kike, lakini serikali za wanafunzi zimekuwa zikiwasaidia watoto kujifunza uongozi."

Suhuba Daud Issa, Mkuu wa Divisheni ya Huduma za Wanafunzi kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, anasema, "Tuna miradi kama Boys and Girls Science and Leadership Programme inayowawezesha watoto wa kike kuwa viongozi wa baadaye."

Hitimisho

Maandalizi ya watoto wa kike kuwa viongozi wa kesho yameonyesha mafanikio makubwa kupitia program mbalimbali shuleni, msaada wa walimu, na uungwaji mkono wa wazazi. Takwimu kutoka Global Partnership for Education zinaonyesha kuwa nchi zinazowekeza katika elimu ya watoto wa kike zina 70% ya uwezekano wakuwa na viongozi bora kwenye nafasi za kisiasa na kijamii katika siku zijazo.

Zanzibar ipo katika mwelekeo sahihi wakufanikisha mpango wake wa Maendeleo wa mwaka 2050, na jitihada hizi ni hatua muhimu kuelekea kujenga kizazi cha viongozi wa kike wenye maono na uwezo wakubadili jamii.
 

Attachments

  • Screenshot_20250207_095030_Instagram.jpg
    Screenshot_20250207_095030_Instagram.jpg
    170.6 KB · Views: 2
  • Screenshot_20250207_095017_Instagram.jpg
    Screenshot_20250207_095017_Instagram.jpg
    158.6 KB · Views: 2
  • Screenshot_20250207_095537_Photos.jpg
    Screenshot_20250207_095537_Photos.jpg
    515.9 KB · Views: 2
Back
Top Bottom