Namna nilivyofunga ndoa kwa harusi nzuri na kubwa (ya ndoto yangu) bila kuchangisha wala kukopa

Namna nilivyofunga ndoa kwa harusi nzuri na kubwa (ya ndoto yangu) bila kuchangisha wala kukopa

Tutafute hela jamani ....mambo ya kufanya sherehe ya harusi kama birthday haikubaliki kwetu..... tunaishi mara moja tu
 
Mimi sina ela na katika harusi yangu nimepanga nitumie laki 5 Tu Kwa watu 20 nguo zote zitakodishwa Mimi na mke wangu wasaidizi nao ivyoivyo Kama ikiwa lazima Ila japo sioni ulazima siowi kumfurahisha mama wala Baba wala mjomba wala Bibi naowa kwaajili ya maisha yangu mwenyewe kama uyo. Mwanamke akikataa wala sitalazimaisha mapema snaa naachana naye
 
Mimi sina ela na katika harusi yangu nimepanga nitumie laki 5 Tu Kwa watu 20 nguo zote zitakodishwa Mimi na mke wangu wasaidizi nao ivyoivyo Kama ikiwa lazima Ila japo sioni ulazima siowi kumfurahisha mama wala Baba wala mjomba wala Bibi naowa kwaajili ya maisha yangu mwenyewe kama uyo. Mwanamke akikataa wala sitalazimaisha mapema snaa naachana naye
Shela unakodi ila suti zenu nunua tu za elfu 80, ni sawa na kukodi.
 
Kwa hizo gharama zote huwezi kusema ulifanya harusi ya bei rahisi! Sijajumlisha gharama zote ila kwa haraka hazipungui 5M hizo hela.

So still ni harusi ya gharama endapo ukijumlisha na hela ya mahari!
Nilishajumlisha ni milioni 2 na laki 3
 
Gharama zote Hizo..? Ngoja Waje Watani zetu Wapare wakupe dondoo Muhimu Kwenye Kubana Bajeti Ya harusi..!
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji16]wapareee.
Lengo la jamaa ni kutochangisha watu wala kuachiwa madeni, amefaulu sana
 
Wasalaam,

Kuna wadau wanaumizwa sana na madeni ya harusi baada ya kufunga ndoa, inampelekea mtu mpaka muda wa miaka minne akilipa tu deni la harusi ya ndo
Hiyo gharama ni kubwa sana
kama wewe ni msabato unafunga ndoa siku ya ibada, mkimaliza hapo nyie wanne mnakutana sehemu mnakula wali na soda shughuli imeisha
 
Mimi sina ela na katika harusi yangu nimepanga nitumie laki 5 Tu Kwa watu 20 nguo zote zitakodishwa Mimi na mke wangu wasaidizi nao ivyoivyo Kama ikiwa lazima Ila japo sioni ulazima siowi kumfurahisha mama wala Baba wala mjomba wala Bibi naowa kwaajili ya maisha yangu mwenyewe kama uyo. Mwanamke akikataa wala sitalazimaisha mapema snaa naachana naye
Hapo nakuunga mkono kijana mwenzangu,tena ukimuona mwenye kutaka makubwa zaidi ya kipato chako ujue huyo ni pasua kichwa kwako,mke mzuri ni yule ambae unapanga nae jambo lililo ndani ya uwezo wenu,Safi sana kwa huo msimamo wako
 
Hiyo gharama ni kubwa sana
kama wewe ni msabato unafunga ndoa siku ya ibada, mkimaliza hapo nyie wanne mnakutana sehemu mnakula wali na soda shughuli imeisha
Kweli kabisa,lazima twende na hali halisi ya uchumi ilivyo
 
Nitafanya sherehe nikiwa na doo tuu, kama sivyo sintofanya huo ujuha wa kufurahisha mijitu afu mi nibaki na maumivu.
 
Wasalaam,

Kuna wadau wanaumizwa sana na madeni ya harusi baada ya kufunga ndoa, inampelekea mtu mpaka muda wa miaka minne akilipa tu deni la harusi ya ndoa yake.

Kuna jamaa mmoja kwenye Ofisi yangu ya zamani alifunga ndoa kwa sherehe kubwa na baada ya miezi mmoja akawa anadaiwa karibia na kila mtu pale Kazini, nikajifunza kitu kikubwa kimenifanya leo nikumbuke namna nilivyofunga ndoa kwa harusi bila ya kuchangisha wala kuwa na madeni.

Kwanza kabisa nilimueleza mke wangu kuwa sina uwezo wa harusi kubwa na sitataka kukopa wala kuchangisha. Nguo za harusi za mke wangu nilienda kukodi Chanika gauni la 120000 kwa dada mmoja anaitwa Grace (Mungu Ambariki sana huko alipo), pete za ndoa pia alinielekeza mahali ambapo tungepata English Gold ya elfu 20 kwa pete mbili, tulifanikiwa kwneye hilo.

Wazazi wa mke wangu waliletwa kanisani na ukumbini kwa gari aina ya Hiace (Kipanya) tuliyokodi kwa rafiki wa kaka yangu kwa 100000, gari ya wazazi wanne jumla niliwakodia gari dogo kwa 30000 kuwapeleka na kuwarudisha kanisani.

Nguo za wazazi wangu jumla nilitumia 200000, nguo zangu na mshenga pamoja na msimamizi wa mke wangu tulitumia 400000, nilinunua suti ya elfu 90 pale Kariakoo, gari ya maharusi nilikodi 150000 kwa wale jamaa wa pale Upanga karibu na Muhimbili magari yao hayana mkanda wa Manispaa, ni kama private cars, likapambwa vizuri pamoja na ukumbi jumla kupamba kila kitu ikiwemo kumpamba bibi harusi ikatumika 150000.

Msimamizi wangu nilimpa 20000 akanyoe na kufanya scrub, nami nikatumia 5000 kunyoa na scrub pale Magomeni kwa Frank (Mungu Ambariki sana huyu jamaa alijua kuniweka vizuri).

Niliomba harusi ipangiwe ratiba ya saa nane mchana. Harusi ilifanyikia Azania Front na baada ya kanisani saa kumi tukaenda Lamada Hotel Ilala kupiga picha na kuchezea maji kwa kulipia 50000 tu ili kuruhusiwa kupiga picha kwenye hoteli yao na kwenye swimming pool. Hakukuwa na matarumbeta, majukwaa, maids wala watoto wa kuwatanguliza mbele, hakukuwa na gari kwa waalikwa wengine, wote walitakiwa kuja wenyewe kwa usafiri wao.

Ukumbi walinisaidia sana dada zangu wabarikiwe sana sana, walikodi kwa 100000 ukumbi wa CCM Ilala, MC alilipwa 50000 na ni rafiki wa dada zangu, akalamba na nafasi yake ya mtu wake mmoja, wakwe zangu niliwaalika jumla 20 tu kwa maneno bila kadi na upande wetu jumla 20 tu, mpiga picha alikuwa ni jamaa yangu aliyejitolea kutupiga picha bure kabisa, abarikiwe sana huko alipo. Mtu wa video tulipata kitonga sana kwa 100000 kwa huduma ya video tu na CD nne na flash disk mbili.

Muziki tulikodi kwa madj hawa wa mitaani kwa elfu 50, hakukuwa na bajeti ya vileo wala bia ingawa dada zangu walitoa kreti mbili kwa wanaotaka kunywa na hazikuwekwa hadharani.

Vinywaji na vyakula jumla ilitumika 700000 pamoja na upishi humo humo. Shampeni nilinunua mwenyewe maduka ya Waarabu pale Magomeni kwa 7000 kila moja, zilikuwa tatu.

Keki ilinunuliwa ya ngazi tatu kwa elfu 60.

Ni miaka kadhaa imepita sasa ila mpaka leo ukweni inasemwa kwamba mimi nilifanya harusi kubwa sana na ya kipekee kwa binti yao. Waliinjoi sana na hawakuwa bored.

Aiseee nimekumbuka mbali mpaka nimetamani irudiwe, ilikuwa nzuri sana sana na haikuniacha na majuto ya madeni wala lawama za kuchangisha. Marafiki zetu waliimba sana mpaka saa sita usiku, wakaturushia maua, ilikuwa shamrashamra sana. Tukakata keki, na kila aliyekuwepo alikula kipande, shampeni zetu tatu zikafunguliwa na watu watatu tofauti na zikaongeza shamrashamra, hakukuwa na nyama za kuchoma wala ndizi na hakukuwa na ruhusa ya mtu kwenda kujichukulia anavyotaka bali iliseviwa kwa mtindo wa bufeti, vinywaji vilitoka pale pale hakukuwa na suala la kuvisambazwa kwenye meza moja moja, ndugu jamaa na marafiki wakawa na wasaa wa kuongea chochote wanachojisikia kuongea aisee ilikuwa tamu sana na hasa pale nilipokuwa nikikumbuka kwamba nikitoka hapo sina deni lolote zaidi ya kuinjoi.

Maisha matamu na mazuri ni maamuzi yako na kuepuka madeni ni chanzo kimojawapo cha furaha. Ninawatia moyo wanaojiandaa kuingia kwenye ndoa kuwa harusi ya gharama nafuu inawezekana.
Naomba msaada wako wa kuniunga nae mpiga picha na video.....mwisho wa mwaka nina jambo langu nalifanya
 
Kila nikimuambia twende kwa DC hataki.

Sasa mishe zenyewe hazisomi ananiambia atanisubiri mpaka zinyooke. Mimi siamini kwakua recently nimeanza kuota anachepuka
Kuna jambo la kukushauri hapa kama unaweza kufanya ni bora ukajua hatima yako kuliko kupotezeana nae muda,kama demu uwezo anao basi akuwezeshe kipesa ufanye hata biashara ama kama anauchungu na wewe basi ajiongeze kipindi iki ili baadae mishe zako zikikaa vizuri basi fresh tu,mpaka hapo kama yupo kiupendo kweli kwako basi utamuona tu
 
Kuna jambo la kukushauri hapa kama unaweza kufanya ni bora ukajua hatima yako kuliko kupotezeana nae muda,kama demu uwezo anao basi akuwezeshe kipesa ufanye hata biashara ama kama anauchungu na wewe basi ajiongeze kipindi iki ili baadae mishe zako zikikaa vizuri basi fresh tu,mpaka hapo kama yupo kiupendo kweli kwako basi utamuona tu
Madai yake ni kwamba kufunga ndoa kwa DC siyo sahihi Mungu haitambui
 
Naomba msaada wako wa kuniunga nae mpiga picha na video.....mwisho wa mwaka nina jambo langu nalifanya
Ni watu wawili tofauti, ukiwa tayari nicheki inbox nikuelekeze kwao.
 
Mimi ktk harusi yangu sikuwa na Deni.
1. Nililipia ukumbi 2,000,000
2. Nililipia Mc na Mziki 1,000,000
3. Nililipia Picha na Video 700,000
4. Nililipia Usafiri kwa ujumla 1,000,000

Wazazi na familia walideal na mapambo 1800,000 na vinywaji 4,000,000.

Mchango wa kadi single na double 30,000 tu. Pesa za waalikwa ni kwaajili ya msosi.

Nilipata zawad nyingi Sana na pesa nyingi za zawadi. Ilibidi kukodi fuso kubeba.

NB: JIPANGENI MNAOTARAJIA KUOA. MSITEGEMEE MICHANGO. MWISHO HARUSI SI MSIBA
Plus mahari pengine umetumia zaidi ya 10M.

Mbona maisha magumu jamani? Kuoa pesa. Kujenga ndiyo usiguse.

Corolla kwa 1M unapata. Dah
 
Back
Top Bottom