Poker
JF-Expert Member
- Oct 7, 2016
- 5,445
- 14,828
Mimi naitwa Telo nilizaliwa huko Kigoma, Kasulu maeneo ya kumsenga miaka 60 iliopita. Elimu yangu ni ya darasa la nne, ijapokuwa kiuhalisia elimu ilinipiga sandakalawe.
Maisha huko Kasulu yalikuwa magumu mno yaani mnoo! Mlo ulikuwa wa shida, nyumbani tupo nyomi yakutosha na magonjwa yakawa yanaibuka mara kwa mara. Hivyo baada ya kuona life lishakuwa tough sana kipande hicho cha kumsenga nikaamua nisafiri kuelekea Mwanga Kigoma, ambapo nilikutana na rasi mmoja alienipa dili la hela.
Rasi alinipa mchongo wa majeneza nakuniambia kuwa kuna watu wanazikwa na majeneza mazuri na ya thamani tena yenye hela, hivyo lazima tuwe tunaenda mida mibaya kufukua huko na kuyaiba. Lakini kabla ya yote inatakiwa tukafanye dawa ya kinga kwa mtaalam ili tuwe vizuri zaidi.
Kweli tulienda kwa mtaalam tufanya manyanga, tukaoga dawa na chale za kutosha mwilini. Nakumbuka ilikuwa jumatatu wanazika huko Kigoma tukaenda kuhudhuria pale makuburini na rasi akanitonya kuwa jeneza ni la uhakika, basi baadae ili tupate ujasiri tukavuta ganja ya kutosha na pombe tukaingia kazini tukiwa wawili tuu.
Shughuli haikuwa ya kitoto tukaanza kuchimbua lile kaburi mpaka tukakuta jeneza mahali pake, tukaitoa maiti huko ndani ya jeneza na kuiweka pembeni. Kisha tukapandisha jeneza juu kwa mishamu na kamba mpaka likatoka! Tulipomaliza tukafukia vizuri na kurudishia msalaba kisha tukaenda kulipaki pembeni vichakani tukisubiri usafiri ambao ras alikuwa ameukodi.
Usafiri ulikuja kweli tukapakia mali yetu na kuyeya. Tulikaa Nalonkwa siku 2 kisha likapata mteja na tukagawana pasu kwa pasu.
Hii biashara ya wizi wa majeneza ikaanza kunilipa nikawa napata sana hela mpaka nikafanikiwa kujenga pale Mwanga, ndipo ras aliponipa mchongo mwingine kuwa twende Dar tukaendeleze biashara yetu ya majeneza.
Tulipofika Dar tukafungua workshop yetu ya majeneza na misalaba ikiwa ni kama geresha wakati sisi dhumuni letu kubwa ni kuiba majeneza makaburini usiku na kuja kuyauza tena.
Mwanzo biashara kwa Dar ilikuwa ngumu kidogo mpaka mtaji ukayumba, hivo tulienda Bagamoyo kwa mtaalam moja akatufanyia manyanga tuwe Gado, kisha tukaingia mzigoni. Siku ya siku tukaenda kuhudhuria mazishi ya tajiri mmoja kwakweli mioyo ilipiga paah! Lile jeneza tuliona ni kama almasi inaenda kufukiwa, hivo na sisi huwa ni watu wamwanzo kabisa huwa tunashika beleshi nakuanza kufukia tukiasaidiana na wengine, bahati nzuri lile kaburi halikusakafiwa. Hivo usiku kama kawa yetu tukaenda kuiba jeneza la huyo tajiri na tukafanikiwa. Lile jeneza tulikaa nalo kwa wiki mbili kisha tukaliuza kwa tajiri mwingine hapo sasa mtaji ukakaa sawa, tukaamua tuajiri vijana wengine wawili kwaajili ya biashara yetu ya majeneza.
Biashara ikaanza kushamiri na kukua, mpaka tukafanikiwa kununua gari mbili kwaajili ya biashara yetu ya majeneza. Tukaanza kupata tenda nyingi za majeneza na sisi tukazidi kuiba majeneza mengi kwa hapo Dar.
Tukaongeza vijana hivyo timu ikawa na watu 8 special kwaajili ya kuiba majeneza makaburini.
Baada ya kuona biashara imeshakuwa na hela ziko za kutosha tukaanza kutofautiana na Ras, mpaka tukaamua kugawana mali. Sasa shida ikawa tunapoenda na vijana wangu kupiga tukio makaburini usiku mara tunabumiana na Ras, sasa inakuwa ni kavita kadogo kadogo. Mwisho tukaanza kununiana ghafla tukawa maadui kila mmoja akiona anamzibia rizki mwenzake, hivyo tukaanza kuwindana sasa kila mtu na mbinu anayoijua yeye.
Kwa kweli tuliwindana sana huku kila mmoja akitaka kuwa juu ya mwenzake. Basi siku ya siku nikafanikiwa kupata timu ya vijana wapya wabobezi wa mishindo yaani kuiba majumbani kwa watu na silaha.
Kisha tukaunda genge letu la kuiba majeneza na kuvamia nyumba za matajiri. Tukatafta mapanga makali mnoo na bunduki zikawa tatu. Hivo kwakuwa Ras alikuwa kauzibe kangu nikapendekeza tukamvamie Ras nyumbani kwake tummalize. Tulienda kwa Ras kweli tukamkuta hana hili wala lile tukammiminia risasi za kutosha na hapo hapo ukawa mwisho wa Ras. Kiupande wa biashara nikawa nimewini ila msala ukabaki katika upelelezi wa kesi hiyo ya mauaji huku wengi wakinihisia kwa sababu ya ule ukaribu tuliokuwa nawo. Itaendelea,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Maisha huko Kasulu yalikuwa magumu mno yaani mnoo! Mlo ulikuwa wa shida, nyumbani tupo nyomi yakutosha na magonjwa yakawa yanaibuka mara kwa mara. Hivyo baada ya kuona life lishakuwa tough sana kipande hicho cha kumsenga nikaamua nisafiri kuelekea Mwanga Kigoma, ambapo nilikutana na rasi mmoja alienipa dili la hela.
Rasi alinipa mchongo wa majeneza nakuniambia kuwa kuna watu wanazikwa na majeneza mazuri na ya thamani tena yenye hela, hivyo lazima tuwe tunaenda mida mibaya kufukua huko na kuyaiba. Lakini kabla ya yote inatakiwa tukafanye dawa ya kinga kwa mtaalam ili tuwe vizuri zaidi.
Kweli tulienda kwa mtaalam tufanya manyanga, tukaoga dawa na chale za kutosha mwilini. Nakumbuka ilikuwa jumatatu wanazika huko Kigoma tukaenda kuhudhuria pale makuburini na rasi akanitonya kuwa jeneza ni la uhakika, basi baadae ili tupate ujasiri tukavuta ganja ya kutosha na pombe tukaingia kazini tukiwa wawili tuu.
Shughuli haikuwa ya kitoto tukaanza kuchimbua lile kaburi mpaka tukakuta jeneza mahali pake, tukaitoa maiti huko ndani ya jeneza na kuiweka pembeni. Kisha tukapandisha jeneza juu kwa mishamu na kamba mpaka likatoka! Tulipomaliza tukafukia vizuri na kurudishia msalaba kisha tukaenda kulipaki pembeni vichakani tukisubiri usafiri ambao ras alikuwa ameukodi.
Usafiri ulikuja kweli tukapakia mali yetu na kuyeya. Tulikaa Nalonkwa siku 2 kisha likapata mteja na tukagawana pasu kwa pasu.
Hii biashara ya wizi wa majeneza ikaanza kunilipa nikawa napata sana hela mpaka nikafanikiwa kujenga pale Mwanga, ndipo ras aliponipa mchongo mwingine kuwa twende Dar tukaendeleze biashara yetu ya majeneza.
Tulipofika Dar tukafungua workshop yetu ya majeneza na misalaba ikiwa ni kama geresha wakati sisi dhumuni letu kubwa ni kuiba majeneza makaburini usiku na kuja kuyauza tena.
Mwanzo biashara kwa Dar ilikuwa ngumu kidogo mpaka mtaji ukayumba, hivo tulienda Bagamoyo kwa mtaalam moja akatufanyia manyanga tuwe Gado, kisha tukaingia mzigoni. Siku ya siku tukaenda kuhudhuria mazishi ya tajiri mmoja kwakweli mioyo ilipiga paah! Lile jeneza tuliona ni kama almasi inaenda kufukiwa, hivo na sisi huwa ni watu wamwanzo kabisa huwa tunashika beleshi nakuanza kufukia tukiasaidiana na wengine, bahati nzuri lile kaburi halikusakafiwa. Hivo usiku kama kawa yetu tukaenda kuiba jeneza la huyo tajiri na tukafanikiwa. Lile jeneza tulikaa nalo kwa wiki mbili kisha tukaliuza kwa tajiri mwingine hapo sasa mtaji ukakaa sawa, tukaamua tuajiri vijana wengine wawili kwaajili ya biashara yetu ya majeneza.
Biashara ikaanza kushamiri na kukua, mpaka tukafanikiwa kununua gari mbili kwaajili ya biashara yetu ya majeneza. Tukaanza kupata tenda nyingi za majeneza na sisi tukazidi kuiba majeneza mengi kwa hapo Dar.
Tukaongeza vijana hivyo timu ikawa na watu 8 special kwaajili ya kuiba majeneza makaburini.
Baada ya kuona biashara imeshakuwa na hela ziko za kutosha tukaanza kutofautiana na Ras, mpaka tukaamua kugawana mali. Sasa shida ikawa tunapoenda na vijana wangu kupiga tukio makaburini usiku mara tunabumiana na Ras, sasa inakuwa ni kavita kadogo kadogo. Mwisho tukaanza kununiana ghafla tukawa maadui kila mmoja akiona anamzibia rizki mwenzake, hivyo tukaanza kuwindana sasa kila mtu na mbinu anayoijua yeye.
Kwa kweli tuliwindana sana huku kila mmoja akitaka kuwa juu ya mwenzake. Basi siku ya siku nikafanikiwa kupata timu ya vijana wapya wabobezi wa mishindo yaani kuiba majumbani kwa watu na silaha.
Kisha tukaunda genge letu la kuiba majeneza na kuvamia nyumba za matajiri. Tukatafta mapanga makali mnoo na bunduki zikawa tatu. Hivo kwakuwa Ras alikuwa kauzibe kangu nikapendekeza tukamvamie Ras nyumbani kwake tummalize. Tulienda kwa Ras kweli tukamkuta hana hili wala lile tukammiminia risasi za kutosha na hapo hapo ukawa mwisho wa Ras. Kiupande wa biashara nikawa nimewini ila msala ukabaki katika upelelezi wa kesi hiyo ya mauaji huku wengi wakinihisia kwa sababu ya ule ukaribu tuliokuwa nawo. Itaendelea,,,,,,,,,,,,,,,,,,