Namna nzuri ya kutatua changamoto ya machinga na wafanyabiashara ndogo pembezoni mwa barabara na maeneo yasiyo rasmi

Namna nzuri ya kutatua changamoto ya machinga na wafanyabiashara ndogo pembezoni mwa barabara na maeneo yasiyo rasmi

Merci

Member
Joined
Feb 6, 2012
Posts
92
Reaction score
138
Kwa kuzingatia yakua machinga na wafanya biashara ndogo ndogo nao huchangia katika pato la Taifa na la kwao moja kwa moja, ni vema kufikiria na kuweka njia nzuri ambayo itawafanya waendelee kutumia maeneo hayo kwa shughuri zao za kiuchumi.

Mfano, unakuta migambo na askari wa jiji wakipambana kuwaondoa na hata kuharibu bidhaa za wananchi wenzetu hawa ambao walipambana sana kupata mitaji kwa kisa tu eti hawako maeneo rasmi?!

Nashauri tutumie mbinu mbadala za kuhakikisha maeneo hayo yaliyo pembezoni mwa barabara na yale yasiyo rasmi yakitumiwa na machinga kwa nyakati za kuanzia jioni hadi usiku kwa kuhakikisha kuna kuwa na vibanda vizuri ambavyo vinahamishika kiurahisi kama inavyojionyesha kwenye video hii.

Jambo hili litafanya machinga waendelea kujumuika katika kukuza uchumi wa nchi na wa familia zao maana "hakuna maendeleo bila sisi wote kwa ujumla". Maendeleo makubwa huletwa na fikra zilizo nje ya hali ya kawaida iliozoeleka.

 
Namna nzuri ya kumaliza hili tatizo ni sera nzuri na usimamizi bora wa uchumi utakaozalisha viwanda vingi, kukuza sekta ya utalii na sekta nyingine za huduma. Njia ni nyingine zozote ni za mkato ni zitafanya kazi kwa muda mfupi sana.
 
Hawa jamaa Kwa mipango miji tunatoitaka wataonekana tatizo tu. Na hawaondoki wale, mtapiga mnavyoweza dunia nzima wapo.... Labda tuwape maelezo namna y kujipanga na tukusanye kodi tu
 
Back
Top Bottom