Namna wanahabari wanavyoharibu lugha ya Kiswahili

Namna wanahabari wanavyoharibu lugha ya Kiswahili

Trubetzkoy

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2018
Posts
349
Reaction score
678
Miaka ya hivi karibuni limeibuka wimbi kubwa la uharibifu wa lugha ya kiswahili (nchini Tanzania). Baadhi ya watu wamekuwa wakipotosha matumizi sahihi ya kiswahili ama kwa kujua au kwa kutokujua kama wanakosea.

Kumeibuka dosari nyingi katika uandishi na utamkaji wa baadhi ya maneno ya kiswahili. Mathalani, baadhi ya watu wanafanya substitution na omission kwenye baadhi ya maneno. Kwa mfano, utasikia/ona mtu ameandika

Hasubuhi badala ya asubuhi,
Hafadhali badala ya afadhali,
Hamka badala ya amka,
Hendelea badala ya endelea,
Humoja badala ya umoja,
Bahadhi badala ya baadhi, yani wana
substitute sound /h/ kwenye sound /a/.

Hali kadhalika wanafanya omission kwenye baadhi ya maneno mfano,
Ela badala ya hela
Alafu badala ya halafu
Angaika badala ya hangaika
Abari badala ya habari, hapa wanafanya complete omission of sound /h/. Makosa ni mengi sana na mbaya zaidi wanaofanya hivyo wengi wao hufanya makusudi wakichukulia kuwa ni swaga kumbe shit.

Sasa turudi kwa wana habari
Nikiwa kama mfuatiliaji mkubwa wa habari za michezo, kuna baadhi ya wachambuzi hasa kwenye channel yetu pendwa wamekuwa wakinikata mood kutokana na uharibifu wa lugha ya kiswahili wanaoufanya. Inawezekana wanakosea kutokana na haraka wanayokuwanayo wakati wa kuchambua soka, hata hivyo kama baadhi yao watabahatika kupitia uzi huu basi ni vema wajirekebishe.

Sio ajabu kusikia mchambuzi akisema sentensi hizi;
1. Miongoni mwa kitu ambacho kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa mchezaji ambaye...
3. Moja ya kitu ambacho...

Tukianza na sentensi ya kwanza, neno miongoni linatumika kutaja kitu kimoja kati ya vingi, sentensi ya pili vilevile.

Sentensi ya tatu nayo ina dosari kubwa, unaposema 'moja ya' tunakusudia kuona idadi kubwa ya vitu ambapo hicho kimoja ulichokitaja ni exceptional.

Kwa minajili hiyo basi, sentensi hizo hapo juu usahihi wake ni huu ufuatao;

1. Miongoni mwa vitu ambavyo kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa wachezaji ambao...
3. Moja ya vitu ambavyo...

Lengo la kusoma ni kuelimika na tunapoelimika hatuna budi kuielimisha jamii.
Mimi nimetimiza wajibu wangu sasa ni zamu yako,
Naomba kuwasilisha.
 
Mtoa mada umenifanya nijisikie raha sana kugundua kwamba angalau bado wapo watu wanaoona uchungu lugha ya kiswahili isipotumika kwa usahihi.

Kuna makosa mengi sana kwenye uandishi na pia matamshi ya baadhi ya maneno ya kiswahili.
Wakati mwingine unakuta mtu ka-post kabisa kwenye ukurasa wake sentensi zenye makosa makubwa ya lugha.

Kiswahili ni kipana sana na kitamu. Niliwahi kusoma mahala matumizi na tofauti ya maneno 'ndio' na 'ndiyo' pia 'sio' na 'siyo'. Maneno ambayo tunayatumia tu bila kujali usahihi wa matumizi yake
 
Mtoa mada umenifanya nijisikie raha sana kugundua kwamba angalau bado wapo watu wanaoona uchungu lugha ya kiswahili isipotumika kwa usahihi.

Kuna makosa mengi sana kwenye uandishi na pia matamshi ya baadhi ya maneno ya kiswahili.
Wakati mwingine unakuta mtu ka-post kabisa kwenye ukurasa wake sentensi zenye makosa makubwa ya lugha.

Kiswahili ni kipana sana na kitamu. Niliwahi kusoma mahala matumizi na tofauti ya maneno 'ndio' na 'ndiyo' pia 'sio' na 'siyo'. Maneno ambayo tunayatumia tu bila kujali usahihi wa matumizi yake
Karibu tuungane kuiokoa lugha yetu adhimu ya kiswahili
 
Kuna hawa HALOTEL wameajiri watu wasiojua matumizi ya R na L kabisa.
Sms kutoka kwao unakuta imeandikwa tunakutakia SheLEhe njema za Uhulu au TafadhaRi badala ya Tafadhali
Ilibidi nitupe line yao kutokana na huo upuuzi wa waajiriwa wao.
 
Kuna hawa HALOTEL wameajiri watu wasiojua matumizi ya R na L kabisa.
Sms kutoka kwao unakuta imeandikwa tunakutakia SheLEhe njema za Uhulu au TafadhaRi badala ya Tafadhali
Ilibidi nitupe line yao kutokana na huo upuuzi wa waajiriwa wao.
Na kuna sehemu wanakwambia "Tutakutaarifu kwa ujumbe ufupi" Daah sema tusiwajadili tusije tukaingilia biashara za watu
 
Karibu tuungane kuiokoa lugha yetu adhimu ya kiswahili
Mkuu kwanza hongera sana kwa kuwa na uchungu namna ambavyo lugha ya kiswahili inavyozidi kuharibiwa na sisi watumiaji wenyewe kwa maksudi huku wenye dhamana ya kukiendeleza kiswahili wakiwa wamekaa zao tu maofisini.

Huwa nakereka sana na matumizi mabaya ya kiswahili. Nilishawaambia watu wanaonizunguka endapo mtu akituma ujumbe usiozingatia matumizi sahihi ya maneno ya kiswahili basi sitomjibu ujumbe wake hadi atakaporekebisha.
 
Miaka ya hivi karibuni limeibuka wimbi kubwa la uharibifu wa lugha ya kiswahili (nchini Tanzania). Baadhi ya watu wamekuwa wakipotosha matumizi sahihi ya kiswahili ama kwa kujua au kwa kutokujua kama wanakosea.

Kumeibuka dosari nyingi katika uandishi na utamkaji wa baadhi ya maneno ya kiswahili. Mathalani, baadhi ya watu wanafanya substitution na omission kwenye baadhi ya maneno. Kwa mfano, utasikia/ona mtu ameandika
Hasubuhi badala ya asubuhi,
Hafadhali badala ya afadhali,
Hamka badala ya amka,
Hendelea badala ya endelea,
Humoja badala ya umoja,
Bahadhi badala ya baadhi, yani wana
substitute sound /h/ kwenye sound /a/.

Hali kadhalika wanafanya omission kwenye baadhi ya maneno mfano,
Ela badala ya hela
Alafu badala ya halafu
Angaika badala ya hangaika
Abari badala ya habari, hapa wanafanya complete omission of sound /h/. Makosa ni mengi sana na mbaya zaidi wanaofanya hivyo wengi wao hufanya makusudi wakichukulia kuwa ni swaga kumbe shit.

Sasa turudi kwa wana habari,
Nikiwa kama mfuatiliaji mkubwa wa habari za michezo, kuna baadhi ya wachambuzi hasa kwenye channel yetu pendwa wamekuwa wakinikata mood kutokana na uharibifu wa lugha ya kiswahili wanaoufanya. Inawezekana wanakosea kutokana na haraka wanayokuwanayo wakati wa kuchambua soka, hata hivyo kama baadhi yao watabahatika kupitia uzi huu basi ni vema wajirekebishe.

Sio ajabu kusikia mchambuzi akisema sentensi hizi;
1. Miongoni mwa kitu ambacho kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa mchezaji ambaye...
3. Moja ya kitu ambacho...

Tukianza na sentensi ya kwanza, neno miongoni linatumika kutaja kitu kimoja kati ya vingi, sentensi ya pili vilevile.

Sentensi ya tatu nayo ina dosari kubwa, unaposema 'moja ya' tunakusudia kuona idadi kubwa ya vitu ambapo hicho kimoja ulichokitaja ni exceptional.

Kwa minajili hiyo basi, sentensi hizo hapo juu usahihi wake ni huu ufuatao;

1. Miongoni mwa vitu ambavyo kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa wachezaji ambao...
3. Moja ya vitu ambavyo...

Lengo la kusoma ni kuelimika na tunapoelimika hatuna budi kuielimisha jamii.
Mimi nimetimiza wajibu wangu sasa ni zamu yako,
Naomba kuwasilisha.
Hongera sana mkuu[emoji122][emoji122][emoji122]
 
Miaka ya hivi karibuni limeibuka wimbi kubwa la uharibifu wa lugha ya kiswahili (nchini Tanzania). Baadhi ya watu wamekuwa wakipotosha matumizi sahihi ya kiswahili ama kwa kujua au kwa kutokujua kama wanakosea.

Kumeibuka dosari nyingi katika uandishi na utamkaji wa baadhi ya maneno ya kiswahili. Mathalani, baadhi ya watu wanafanya substitution na omission kwenye baadhi ya maneno. Kwa mfano, utasikia/ona mtu ameandika
Hasubuhi badala ya asubuhi,
Hafadhali badala ya afadhali,
Hamka badala ya amka,
Hendelea badala ya endelea,
Humoja badala ya umoja,
Bahadhi badala ya baadhi, yani wana
substitute sound /h/ kwenye sound /a/.

Hali kadhalika wanafanya omission kwenye baadhi ya maneno mfano,
Ela badala ya hela
Alafu badala ya halafu
Angaika badala ya hangaika
Abari badala ya habari, hapa wanafanya complete omission of sound /h/. Makosa ni mengi sana na mbaya zaidi wanaofanya hivyo wengi wao hufanya makusudi wakichukulia kuwa ni swaga kumbe shit.

Sasa turudi kwa wana habari,
Nikiwa kama mfuatiliaji mkubwa wa habari za michezo, kuna baadhi ya wachambuzi hasa kwenye channel yetu pendwa wamekuwa wakinikata mood kutokana na uharibifu wa lugha ya kiswahili wanaoufanya. Inawezekana wanakosea kutokana na haraka wanayokuwanayo wakati wa kuchambua soka, hata hivyo kama baadhi yao watabahatika kupitia uzi huu basi ni vema wajirekebishe.

Sio ajabu kusikia mchambuzi akisema sentensi hizi;
1. Miongoni mwa kitu ambacho kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa mchezaji ambaye...
3. Moja ya kitu ambacho...

Tukianza na sentensi ya kwanza, neno miongoni linatumika kutaja kitu kimoja kati ya vingi, sentensi ya pili vilevile.

Sentensi ya tatu nayo ina dosari kubwa, unaposema 'moja ya' tunakusudia kuona idadi kubwa ya vitu ambapo hicho kimoja ulichokitaja ni exceptional.

Kwa minajili hiyo basi, sentensi hizo hapo juu usahihi wake ni huu ufuatao;

1. Miongoni mwa vitu ambavyo kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa wachezaji ambao...
3. Moja ya vitu ambavyo...

Lengo la kusoma ni kuelimika na tunapoelimika hatuna budi kuielimisha jamii.
Mimi nimetimiza wajibu wangu sasa ni zamu yako,
Naomba kuwasilisha.
Mtu mmoja amefariki dunia na wengine watatu kujeruhiwa (wamejeruhiwa)! Swali, kwanini wajeruhiwe? Neno kujeruhiwa siku hizi limekuwa ndilo neno rasmi!
Mkutano uta ahairishwa badala ya utaahirishwa.
Kwa ujumla watanzania wengi hawajui matumizi ya maneno sahihi ya kiswahili.
 
Back
Top Bottom