Trubetzkoy
JF-Expert Member
- Oct 31, 2018
- 349
- 678
Miaka ya hivi karibuni limeibuka wimbi kubwa la uharibifu wa lugha ya kiswahili (nchini Tanzania). Baadhi ya watu wamekuwa wakipotosha matumizi sahihi ya kiswahili ama kwa kujua au kwa kutokujua kama wanakosea.
Kumeibuka dosari nyingi katika uandishi na utamkaji wa baadhi ya maneno ya kiswahili. Mathalani, baadhi ya watu wanafanya substitution na omission kwenye baadhi ya maneno. Kwa mfano, utasikia/ona mtu ameandika
Hasubuhi badala ya asubuhi,
Hafadhali badala ya afadhali,
Hamka badala ya amka,
Hendelea badala ya endelea,
Humoja badala ya umoja,
Bahadhi badala ya baadhi, yani wana
substitute sound /h/ kwenye sound /a/.
Hali kadhalika wanafanya omission kwenye baadhi ya maneno mfano,
Ela badala ya hela
Alafu badala ya halafu
Angaika badala ya hangaika
Abari badala ya habari, hapa wanafanya complete omission of sound /h/. Makosa ni mengi sana na mbaya zaidi wanaofanya hivyo wengi wao hufanya makusudi wakichukulia kuwa ni swaga kumbe shit.
Sasa turudi kwa wana habari
Nikiwa kama mfuatiliaji mkubwa wa habari za michezo, kuna baadhi ya wachambuzi hasa kwenye channel yetu pendwa wamekuwa wakinikata mood kutokana na uharibifu wa lugha ya kiswahili wanaoufanya. Inawezekana wanakosea kutokana na haraka wanayokuwanayo wakati wa kuchambua soka, hata hivyo kama baadhi yao watabahatika kupitia uzi huu basi ni vema wajirekebishe.
Sio ajabu kusikia mchambuzi akisema sentensi hizi;
1. Miongoni mwa kitu ambacho kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa mchezaji ambaye...
3. Moja ya kitu ambacho...
Tukianza na sentensi ya kwanza, neno miongoni linatumika kutaja kitu kimoja kati ya vingi, sentensi ya pili vilevile.
Sentensi ya tatu nayo ina dosari kubwa, unaposema 'moja ya' tunakusudia kuona idadi kubwa ya vitu ambapo hicho kimoja ulichokitaja ni exceptional.
Kwa minajili hiyo basi, sentensi hizo hapo juu usahihi wake ni huu ufuatao;
1. Miongoni mwa vitu ambavyo kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa wachezaji ambao...
3. Moja ya vitu ambavyo...
Lengo la kusoma ni kuelimika na tunapoelimika hatuna budi kuielimisha jamii.
Mimi nimetimiza wajibu wangu sasa ni zamu yako,
Naomba kuwasilisha.
Kumeibuka dosari nyingi katika uandishi na utamkaji wa baadhi ya maneno ya kiswahili. Mathalani, baadhi ya watu wanafanya substitution na omission kwenye baadhi ya maneno. Kwa mfano, utasikia/ona mtu ameandika
Hasubuhi badala ya asubuhi,
Hafadhali badala ya afadhali,
Hamka badala ya amka,
Hendelea badala ya endelea,
Humoja badala ya umoja,
Bahadhi badala ya baadhi, yani wana
substitute sound /h/ kwenye sound /a/.
Hali kadhalika wanafanya omission kwenye baadhi ya maneno mfano,
Ela badala ya hela
Alafu badala ya halafu
Angaika badala ya hangaika
Abari badala ya habari, hapa wanafanya complete omission of sound /h/. Makosa ni mengi sana na mbaya zaidi wanaofanya hivyo wengi wao hufanya makusudi wakichukulia kuwa ni swaga kumbe shit.
Sasa turudi kwa wana habari
Nikiwa kama mfuatiliaji mkubwa wa habari za michezo, kuna baadhi ya wachambuzi hasa kwenye channel yetu pendwa wamekuwa wakinikata mood kutokana na uharibifu wa lugha ya kiswahili wanaoufanya. Inawezekana wanakosea kutokana na haraka wanayokuwanayo wakati wa kuchambua soka, hata hivyo kama baadhi yao watabahatika kupitia uzi huu basi ni vema wajirekebishe.
Sio ajabu kusikia mchambuzi akisema sentensi hizi;
1. Miongoni mwa kitu ambacho kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa mchezaji ambaye...
3. Moja ya kitu ambacho...
Tukianza na sentensi ya kwanza, neno miongoni linatumika kutaja kitu kimoja kati ya vingi, sentensi ya pili vilevile.
Sentensi ya tatu nayo ina dosari kubwa, unaposema 'moja ya' tunakusudia kuona idadi kubwa ya vitu ambapo hicho kimoja ulichokitaja ni exceptional.
Kwa minajili hiyo basi, sentensi hizo hapo juu usahihi wake ni huu ufuatao;
1. Miongoni mwa vitu ambavyo kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa wachezaji ambao...
3. Moja ya vitu ambavyo...
Lengo la kusoma ni kuelimika na tunapoelimika hatuna budi kuielimisha jamii.
Mimi nimetimiza wajibu wangu sasa ni zamu yako,
Naomba kuwasilisha.