Namna wanahabari wanavyoharibu lugha ya Kiswahili

Namna wanahabari wanavyoharibu lugha ya Kiswahili

Tena utakuta mwingine kasoma kiswahili mpaka ngazi ya shahada lakini uandishi wake ndio huo
Wanaonikera zaidi ni wanaotumia "ga" "ge" "gi" mfano "alikwendaga" badala ya "alikwenda" "sielewagi" badala ya "sielewi"
 
Nje ya wanahabari kidogo naomba mnisaidie hili,
Mshabiki wangu au Mashabiki zangu.Maana nalisikiaga sana kwenye interviews za wasanii wetu
 
Hili jambo nadhani usiishie kuwaangazia tu hao wachambuzi ila tuliweke Kitaifa. Kuna kaumbumbumbu ka kijinga sana kanaendelea ndani ya Taifa lwtu hili halafu wao wanajiona wako sahihi muda wote!

Mfano mtu anakwambia Mbaka badala ya Mpaka au anakuambia Ndakwambia badala ya Nitakuambia. Au wale wanaoweka x badala ya s.

Nazidi kumuelewa mzee Mkapa aliposema kuna haja ya kuangalia mustakabali wa elimu yetu. Tena hawa wanafunzi wa vyuoni wengi wao ndio Wapumbavu wahed kabisa katika kuzungumza na kuandika kiswahili. Unakuta hawezi kukiongea kiswahili wala hawezi kuongea kiingereza wanachotambia na maneno yao mawili mawili.
 
Je kiswahili fasaha ni
Kuroga au kuloga?
Kulamba au kuramba?

Watu wa pwani wanaharibu haya maneno
 
Nadhani kwa ukanda wa Afrika ya Mashariki, Kenya wanaongoza kwa kuongea kiswahili kibovu!

Ahueni Watanzania tuna unafuu! Ingawa ni kweli, tuna changamoto.
Mzaramo akikosea kuongea kisambaa sio tatizo. Tatizo ni msambaa akikosea kisambaa.
 
Madawa ya kulevya badala ya Dawa za kulevya.
Zote ni sahihi.

Neno "madawa" hutumika kutia msisitizo wa jinsi gani hizo dawa ni mbaya na zisizofaa.

"Dawa za kulevya" ni neno ambalo si kali sana. Na linaweza kutumika pia kulingana na muktadha au namna ambavyo muwasilishaji anataka kutia uzito ujumbe wake.
 
Sentensi 2 hivi kuna mtu anayejua kiswahili anaweza andika hivi kuchanganya ngeli kiasi hiki
 
Zote ni sahihi.

Neno "madawa" hutumika kutia msisitizo wa jinsi gani hizo dawa ni mbaya na zisizofaa.

"Dawa za kulevya" ni neno ambalo si kali sana. Na linaweza kutumika pia kulingana na muktadha au namna ambavyo muwasilishaji anataka kutia uzito ujumbe wake.
Dawa haina wingi,huwezi kusema Madawa,

Ndio ile ya kusema "Masaa" badala ya "Saa"
 
Watu wa kigoma,Bukoba na Mara wana lafudhi za hovyo sana wanatupa kazi ngumu sisi Wanapwani/wajuvi wa kiswahili kuwarekebisha.
Watu wa pwani mnanikera sana pale mnaposhindwa kutofautisha matumizi ya BAADA na BADALA, utasikia mzaramo anasema " baada atoe pasi anajivuta tu"
 
Hili jambo nadhani usiishie kuwaangazia tu hao wachambuzi ila tuliweke Kitaifa. Kuna kaumbumbumbu ka kijinga sana kanaendelea ndani ya Taifa lwtu hili halafu wao wanajiona wako sahihi muda wote!

Mfano mtu anakwambia Mbaka badala ya Mpaka au anakuambia Ndakwambia badala ya Nitakuambia. Au wale wanaoweka x badala ya s.

Nazidi kumuelewa mzee Mkapa aliposema kuna haja ya kuangalia mustakabali wa elimu yetu. Tena hawa wanafunzi wa vyuoni wengi wao ndio Wapumbavu wahed kabisa katika kuzungumza na kuandika kiswahili. Unakuta hawezi kukiongea kiswahili wala hawezi kuongea kiingereza wanachotambia na maneno yao mawili mawili.
Karibu tuungane kuiokoa lugha yetu adhimu
 
Back
Top Bottom