Namna wanahabari wanavyoharibu lugha ya Kiswahili

Namna wanahabari wanavyoharibu lugha ya Kiswahili

Haya mambo tumeyasoma shule, tena primary. Lakini watu wakimaliza mtihani basi wanasahau. Kizazi cha sasa ni bure kabisa. Lugha za makabila ziro, Kiingereza ziro, Kiswahili ziro!!!
Kiswahili ni kipana sana na kitamu. Niliwahi kusoma mahala matumizi na tofauti ya maneno 'ndio' na 'ndiyo' pia 'sio' na 'siyo'. Maneno ambayo tunayatumia tu bila kujali usahihi wa matumizi yake
 
Haya mambo tumeyasoma shule, tena primary. Lakini watu wakimaliza mtihani basi wanasahau. Kizazi cha sasa ni bure kabisa. Lugha za makabila ziro, Kiingereza ziro, Kiswahili ziro!!!
Hatuna lugha, hatuna utamaduni...tumekuwa Taifa lisilojua kwao.
 
Kwan matumizi ya lugha n nn?si kufanikisha mawasiliano baina ya watu..sasa kama alichodhamiria mtu kukisema mm nimekielewa hayo mengine yananisaidia nn..namrekebisha tu mambo mengine yaende

Na hakuna ambaye ni mkamilifu ktk lugha..tuvumiliane tu
 
Ingekuwa simplistic hivyo, kungekuwa na haja gani ya kwenda shule na kujifunza lugha? Utakuwa chinga wewe!!
Kwan matumizi ya lugha n nn?si kufanikisha mawasiliano baina ya watu..sasa kama alichodhamiria mtu kukisema mm nimekielewa hayo mengine yananisaidia nn..namrekebisha tu mambo mengine yaende

Na hakuna ambaye ni mkamilifu ktk lugha..tuvumiliane tu
 
Haya mambo tumeyasoma shule, tena primary. Lakini watu wakimaliza mtihani basi wanasahau. Kizazi cha sasa ni bure kabisa. Lugha za makabila ziro, Kiingereza ziro, Kiswahili ziro!!!
Karibu tuungane kuiokoa lugha yetu adhimu
 
Nashukuru nami nitupie kero zangu kadhaa ambazo naziona kwa watu wakubwa kabisa katika maongezi au maandishi

Ahueni... auheni/haueni nk
Ahirisha... hairisha
Tasfida... tafsida
Uhuru... huuru/uuru/uhulu nk
Halafu/hapo/hapendi... alafu/apo/apendi
Mambo... mamb
Vipi... vip/vp
Ndiyo... ndy
Safi sana... xaf xn/saf xan/xafi xana nk
Uppercut... ambakati
Niambie...namby
Huyu ndiye... huyu ndo/huyu ndio nk
Hawa ndio... hawa ndo/hawa ndiyo nk
Kwaheri... kwaeri/kwaheli nk
Tu... tyuu/2
Riziki... ridhiki
Afadhali... afazali/ asavali nk
Zorotesha... dhorotesha
Nimemdhibiti... nimemthibiti
Thibitisha...dhibitisha

Bora uchanganye maneno ambayo yamethibitishwa kuwa hayana shida kuchanganya mfano
ramba... lamba
Karibu tuungane kuiokoa lugha yetu adhimu
 
Mtu mmoja amefariki dunia na wengine watatu kujeruhiwa (wamejeruhiwa)! Swali, kwanini wajeruhiwe? Neno kujeruhiwa siku hizi limekuwa ndilo neno rasmi!
Mkutano uta ahairishwa badala ya utaahirishwa.
Kwa ujumla watanzania wengi hawajui matumizi ya maneno sahihi ya kiswahili.
Baadhi yao hutangaza.... "mtu mmoja ameweza kufariki na wengine... kujeruhiwa"!!!
 
Nashukuru nami nitupie kero zangu kadhaa ambazo naziona kwa watu wakubwa kabisa katika maongezi au maandishi

Ahueni... auheni/haueni nk
Ahirisha... hairisha
Tasfida... tafsida
Uhuru... huuru/uuru/uhulu nk
Halafu/hapo/hapendi... alafu/apo/apendi
Mambo... mamb
Vipi... vip/vp
Ndiyo... ndy
Safi sana... xaf xn/saf xan/xafi xana nk
Uppercut... ambakati
Niambie...namby
Huyu ndiye... huyu ndo/huyu ndio nk
Hawa ndio... hawa ndo/hawa ndiyo nk
Kwaheri... kwaeri/kwaheli nk
Tu... tyuu/2
Riziki... ridhiki
Afadhali... afazali/ asavali nk
Zorotesha... dhorotesha
Nimemdhibiti... nimemthibiti
Thibitisha...dhibitisha

Bora uchanganye maneno ambayo yamethibitishwa kuwa hayana shida kuchanganya mfano
ramba... lamba
Mbaka..... Mpaka
Nimemdhibiti.... Nimemzibiti
 
Alusi badala ya Harusi.


Mwingine ana andika ela badala ya hela huku akiamini kua, kuandika hivyo ndio kwenda na wakati,mimi hua najiuliza,hivi na huko ofisini au Shuleni hua wana andika hivyo?
 
Kiswahili ni kipana sana na kitamu. Niliwahi kusoma mahala matumizi na tofauti ya maneno 'ndio' na 'ndiyo' pia 'sio' na 'siyo'. Maneno ambayo tunayatumia tu bila kujali usahihi wa matumizi yake

Unataka kuniambia kuwa katika lugha ya Kiswahili kuna neno "ndio" na "sio?
 
Watanzania hatuko makini na vitu vya msingi.

Halafu watu wamekuwa ni wabishi hawataki kukosolewa.
 
Na waimbaji wa bongoflava nao ni majanga, hasa kubadili penye l kuweka r na kinyume chake.
 
Miaka ya hivi karibuni limeibuka wimbi kubwa la uharibifu wa lugha ya kiswahili (nchini Tanzania). Baadhi ya watu wamekuwa wakipotosha matumizi sahihi ya kiswahili ama kwa kujua au kwa kutokujua kama wanakosea.

Kumeibuka dosari nyingi katika uandishi na utamkaji wa baadhi ya maneno ya kiswahili. Mathalani, baadhi ya watu wanafanya substitution na omission kwenye baadhi ya maneno. Kwa mfano, utasikia/ona mtu ameandika
Hasubuhi badala ya asubuhi,
Hafadhali badala ya afadhali,
Hamka badala ya amka,
Hendelea badala ya endelea,
Humoja badala ya umoja,
Bahadhi badala ya baadhi, yani wana
substitute sound /h/ kwenye sound /a/.

Hali kadhalika wanafanya omission kwenye baadhi ya maneno mfano,
Ela badala ya hela
Alafu badala ya halafu
Angaika badala ya hangaika
Abari badala ya habari, hapa wanafanya complete omission of sound /h/. Makosa ni mengi sana na mbaya zaidi wanaofanya hivyo wengi wao hufanya makusudi wakichukulia kuwa ni swaga kumbe shit.

Sasa turudi kwa wana habari,
Nikiwa kama mfuatiliaji mkubwa wa habari za michezo, kuna baadhi ya wachambuzi hasa kwenye channel yetu pendwa wamekuwa wakinikata mood kutokana na uharibifu wa lugha ya kiswahili wanaoufanya. Inawezekana wanakosea kutokana na haraka wanayokuwanayo wakati wa kuchambua soka, hata hivyo kama baadhi yao watabahatika kupitia uzi huu basi ni vema wajirekebishe.

Sio ajabu kusikia mchambuzi akisema sentensi hizi;
1. Miongoni mwa kitu ambacho kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa mchezaji ambaye...
3. Moja ya kitu ambacho...

Tukianza na sentensi ya kwanza, neno miongoni linatumika kutaja kitu kimoja kati ya vingi, sentensi ya pili vilevile.

Sentensi ya tatu nayo ina dosari kubwa, unaposema 'moja ya' tunakusudia kuona idadi kubwa ya vitu ambapo hicho kimoja ulichokitaja ni exceptional.

Kwa minajili hiyo basi, sentensi hizo hapo juu usahihi wake ni huu ufuatao;

1. Miongoni mwa vitu ambavyo kocha amefanikiwa...
2. Jonas Mkude ni miongoni mwa wachezaji ambao...
3. Moja ya vitu ambavyo...

Lengo la kusoma ni kuelimika na tunapoelimika hatuna budi kuielimisha jamii.
Mimi nimetimiza wajibu wangu sasa ni zamu yako,
Naomba kuwasilisha.
Kuna gazeti moja la Mtanzania ndio walikuwa kinara wa kuharibu Kiswahili, wahariri walishindwa kutofautisha wapi watumie 'ha' na wapi watumie 'a'.

Huwa najiuliza hivi hawa waandishi wa habari na wahariri wao walisomea nchi gani, tumefika mahali kizazi hiki Kiswahili hawajui na Kiimgereza nacho ni taabu vilevile. Kiswahili kinatishiwa na uharibifu kuliko wakati mwingine wowote.

Vv
 
Back
Top Bottom