Namna wanahabari wanavyoharibu lugha ya Kiswahili

Bado tuna safari ndefu sana na tutafika tukiwa tumechoka sana
 
Wengi ni vilaza waganga njaa tu
 
Utawasikia baadhi yao wakiwa studio nanukuu " Ali Kiba ametoa 'nyimbo' kali sana" mwisho wa kunukuu✍️

Halafu cocastic na kampani yako, acheni mara moja kutumia hili neno "tyuu" !! Kwani ugumu uko wapi kutumia neno hili 'tu'?
kuna wale wamichezo na uchambuz wao wa kule Planet ...shida tupu!
 

na wale wamatumizi ya L kwenye R mfano barabara wao watasema balabala habari/ habali wamerudi/ wameludi
 
Unataka kuniambia kuwa katika lugha ya Kiswahili kuna neno "ndio" na "sio?
Ndiyo na nakuandikia na mifano kabisa hapa chini


Ndio= wingi wa ndiye
Mfano "Huyu ndiye aliyekula" (umoja)
"Hawa ndio waliokula" (wingi)

Sio= wingi wa siye (yaani kinyume cha ndio)
Mfano "Huyu siyeninayemtaka" (umoja)
"Hawa sio ninaowataka" (wingi)

Kwahiyo
'Ndiye' wingi wake ni 'ndio' na ukanushi wake kwa ndiye ni 'siye' na kwa ndio ni 'sio'
 
Wengine eti 'hiko' badala ya 'hicho'. Hao wote ni waandishi wa habari waliojiriwa katika radio na TV stations mbalimbali.
 
Umechambua ya ndani sana. Mkuu kuna makosa mengine ya nje sana lakini mtu hajui kama anaharibu lugha yetu. Alipokuwa shule na hata anaposoma maandiko mbalimbali, kitabu kimeandikwa kwa mfano "dharau". Badala ya kusoma kilichoandikwa, atasoma "zarau". Jitu zima na ni msomi huyu. "Thelathini" atatamka "selasini". Jamani tutamke kadri ya maandishi. Kwani hugharimu shilingi ngapi kuzingatia matamshi kwa sahihi?
 
Kama mimi ndiye mwalimu wako hapa nakupa [emoji817]%
 
Nionyeshe badala ya nioneshe, apendi, hapendi, hivi sasa vijana wanatumia sana x badala ha s. Noma sana.
Hili la nionyeshe vs nioneshe, bado lina utata juu ya usahihi wake!
 
Wachambuzi wa soka wa redio fulani wananikera wanaposema "timu haikuweza kupata matokeo" wakimaanisha haijashinda.

Matokeo ya mchezo ni aidha kushinda, kushindwa au suluhu. Bure kabisa wachambuzi wa redio hii.
 
Tatizo ni serikali kupenda kufumbia macho masuala ya taaluma ya uandishi kwa kudhani wanalinda ajira kwa vijana kumbe wanabomoa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…