Namna Watanzania wanavyotapeliwa na Waganga wa Kienyeji nchini Kongo

Namna Watanzania wanavyotapeliwa na Waganga wa Kienyeji nchini Kongo

SEHEMU YA TATU



Baada ya muda kupita bwana Seif alirejea akiwa ameambata na watu huku wengine wakiwa na mafurushi ya mizigo.

Kamugisha alimfuata akaanza kuzungumza nae na ndipo alimwambia asubiri kwanza kwakuwa kuna watu alikuwa anawafanyia taratibu za kusafiri;Alipomalizana na watu wake hao takribani yapata saa 8 mchana mchana,alitufuata tulipo kisha akawa anahitaji tumapatie maelekezo ni wapi tulikuwa tunaelekea .

Kamugisha " Tunaelekea Congo mkuu"

Seif "Congo sehemu gani?"

Kamugisha "Moba"

Seif "Ok usafiri wa Kuelekea Moba hadi kesho kutwa,kuna ile boti pale ndiyo mtakayoondoka nayo!"

Aliendelea "Congo mnaenda kufanyaje ndugu zangu"

Kamugisha "Kwenye mambo ya biashara tu kaka"

Seif "Kuweni wakweli,unajua watanzania sijui tukoje,mara kibao wanapita wanashindwa kusema ukweli ili kama ni msaada wapewe wao wanajifanya wajanja wakifika huko mambo yakiwagomea wanarudi na manung'uniko"

Kamugisha "Hahaha hahaha kaka bhana"

Seif "Nakwambia ukweli ndugu zangu,nyie kama mnaenda kwa waganga semeni niwaambie waganga wazuri msije mkatapeliwa!"

Jamaa alikuwa anaongea kwa ujasiri sana na pia mbele za watu,kitu ambacho mimi na mshikaji hatukukipenda hata kidogo,jamaa alimuomba kama inawezekana tutafute sehemu ambayo tutakuwa sisi watu watatu tuzungumze!.Seif alituchukua hadi maeneo ya nyumbani kwake ambako pembeni kulikuwa na Grosary ya kwake tukakaa hapo.

Sasa tukiwa pale kuna mtu alimpigia simu akamwambia amletee samaki wakubwa 3,haukupita muda boda boda mmoja alikuja na samaki wakubwa akiwa amewaning'niza mbele ya taa.

Seif "Ngojeni kwanza wawakaangie samaki hawa mle kisha ndiyo tuongee,mimi hapa kwangu huwa siwezi kuongewa na watu bila kula kwanza"


Baada ya muda wale samaki waliletwa wakiwa wamekaangwa,tulianza kuwatafuna huku tukiendelea kupiga stori za hapa na pale.Tulipomaliza kula wale samaki jamaa ndipo akaanzisha stori na alihitaji kufahamu tunaelekea Congo kufanya kitu gani!.

Kamugisha "Yes kaka unajua mficha uchi kifo umuumbua,sisi tunaelekea Congo kwa ajili ya matibabu"

Seif "Eeeh huo ndiyo uanaume,niambieni sasa mnaenda kwenye matibabu ya aina gani,Je mnaumwa ?"

Aliendelea "Msije mkaona nawauliza sana maswali,nyinyi ni watanzania wenzangu na kule mimi napafahamu vizuri sana na hata waganga wengi wazuri nawajua na ndiyo maana nataka nijue tatizo lenu kisha nitawaambia mtu sahihi atakaye wafaa!"

Seif "Hivyo msione aibu niambieni"

Kamugisha "Kaka sisi tulikuwa tunaelekea kwenye ishu za mali!"

Seif "Kwahiyo mlikuwa mnataka pesa,si ndiyo!"

Kamugisha "Ndiyo,brother!"

Seif "Sasa hayo ndiyo maneno,hapo nitajua sasa namna ya kuwasaidia!"

Aliendelea "Ngoja nimpigie bwana mmoja,aje muongee nae yaani kwa huyu niaminini tatizo lenu limepata tiba sahihi!"


Jamaa alinyanyua simu yake akapiga,ilipopokelewa wakaanza kuongea kwa lugha ya huko(Kiha au Kifipa).

Seif "Kuna jamaa nimemuita anakuja,huyu yeye ni mtaalamu wa maradhi ya kawaida na kuna kipindi mke wangu alikuwa akiumwa alinisaidia sana,huyu yeye ni mkongomani ila ameshazamia Tanzania muda mrefu na kaoa mwanamke wa Kiha,atawasaidia sana!"

Tulikaa tukiendelea kumsubiri huyo jamaa aliyeitwa aje tuzungumze ili tujue wapi pa kuanzia;Seif alikuwa ni muongeaji sana na kiukweli jamaa alibarikiwa kipaji cha kuongea.

Haukupita muda huyo jamaa alifika akiwa anavuta tumbaku,baada ya kufika bwana Seif alianza kumueleza kila kitu tulichokuwa tumezungumza nae.Baada ya kuelezwa jambo letu,jamaa alituambia wabongo wengi huwa wanafeli kwasababu ya ujuaji wa kijinga.

Jamaa "Unajua watanzania wengi huwa hawajui chochote,na hata hao mnaowaona wanasimulia huwa ni uongo tu,ukweli wa huku tunaujua sisi"

Aliendelea "Mmeaga?"

Kamugisha "Mimi sijamuaga mtu,sijui kwa upande wako mwanangu!"

Mimi "Mimi pia sijamuaga mtu"

Jamaa "Kuaga simaanishi hivyo mnavyofikiria nyie,kuaga maana yake mmeongea na mizimu ya wazee wenu?"

Baada ya kutuambia hiyo kauli tulibaki tunaangaliana na kamugisha kwasababu lilikuwa ni jambo jipya ambalo tulilisikia kwa jamaa.

Kamugisha "Sasa hao mizimu tungewaaga vipi?"

Jamaa "Hamuwezi kwenda huko bila kuaga mizimu,au mnadhani mnaweza kufanikisha mambo yenu bila kuaga mizimu?"

Aliendelea "Sasa sijui nyie mnasemaje,muage kwanza kabla ya kuondoka au muondoke bila kuaga!"

Kamugisha "Kwakuwa nia na lengo ni pesa,nadhani kuaga ni bora zaidi!"

Jamaa "Pale Moba Pol kuna jamaa yangu huyu ni mtaalamu sana kwa kazi yenu hiyo mnayoitaka,na yeye huwa hachukui pesa mpaka afanye kazi kwanza,sasa kama mko tayari tuvuke wote niwapeleke kwake kisha nikisha wafikisha mimi nitarudi nitawaacha ila mtanipa ka hela kadogo tu"

Kamugisha "Hayo sasa ndiyo mambo,tunaomba utusaidie!"

Kamugisha "Ujatuambia lakini jina lako kaka"

Jamaa "Mimi naitwa Jentre"

Kamugisha "Ok, sasa tunafanyaje?"

Jentre "Kuaga maana yake ni kuiaga mizimu ya ndugu zenu waliokufa,wawe mababu,mababa,wamama,au watoto;ili mradi wawe wamekufa hao ndiyo tunaita mizimu!"

Aliendelea "Kwakuwa hamkuaga huko mtokako,tutatafuta makaburi hapa jirani mkaage huko,kwanza nipeni hela nikachukue pemba nyeupe na udi kwa ajili ya kuagia!"


Kamugisha alichomoa noti ya shilingi elfu 5 akawa amempatia bwana Jentre ili akanunue mahitaji yaliyokuwa yanahitajika kwa ajili ya kuagia mizimu.

Jentre "Hili zoezi litafanyika usiku siyo muda huu lakini"

Seif "Ok kama ndivyo nadhani hawa mabwana waende wakatafute Guest House waweke mizigo yao kisha watarudi hapa ili ikifika jioni iwe rahisi"


Basi,bwana Seif alituchukua pale kwake akatupeleka kwenye Guest moja ambayo haikuwa mbali sana tukawa tumechukua vyumba kwa ajili ya kuweka mizigo,baada ya hapo tulirudi kwa bwana Seif kupumzika huku tukipiga stori za hapa na pale kupoteza muda.

Ilipofika jioni Seif alimuelekeza jamaa makaburi yaliyokuwa jirani na makazi ya watu,hata hivyo jamaa alimwambia pale itakuwa si pazuri kwasababu ni sehemu ambayo watu walikuwa wanapita masaa 24 na sisi tulipaswa kuvua nguo na kubaki uchi!.

Seif alimuelekeza makaburi ambayo yalikuwa mbali kidogo na mji ule mdogo na yalikuwa makaburi yaliyokuwa yanamilikiwa na kanisa la Roman Katholic,alimuita yule bodaboda aliyeleta wale samaki akamuambia aje na mwenzie ili watupeleke kwenye hayo makaburi ili kazi ya kuaga mizimu ichukue nafasi.


Inaendelea.................
Hi Ni nzuri nitasoma hii ila ile nyingine no plz utoniona kamwe

Tena harakisha Hadi jmos ikwishe hi[emoji120]

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Hiy

Hiyo nyingine ni ipi?
 
Haya mambo yakuchokozwa na kutukanwa na baadhi ya members humu halafu mimi nikimjibu nakula BAN sidhani kama imekaa sawa.Haiwezekani mtu anatoka huko anakokujua yeye anaanza kuniporomoshea matusi mazito halafu nimuangalie tu!.

Bado sijafikia kiwango hicho cha Utakatifu,kama ni nginja acha iwe nginja.

Wengine hatujaumbwa kuwa watukanaji,mimi nipo kuwaburudisha na kuwaelimisha hadhira yangu na umma wa watanzania wengi wanaojitambua,sasa anatokea mtu anaanza kukuporomoshea matusi ya nguoni kisa tu alikuja Inbox akaomba jambo fulani ukamnyima,ukimjibu kidogo tu anapelekea na wewe kufungiwa,hii siyo sawa moderators,wengine mnatuonea bila sababu ya msingi.

Kama nyuzi zangu zinakupa kero na huzipendi kwanini usipite ukatazame nyuzi zinazokufurahisha?,Kila mtu hapa anasoma anachoona kwake kina manufaa na anachokipenda,kama unaona hutaki usumbufu una-Block au Una - Ignore unaendelea na mishe zako,waachieni watu wanaotaka kujifunza na kuburudika wasome nyuzi zangu.

Hadhira yangu kwa muda wa siku zisizopungua 5 imeshindwa kupata simulizi nzuri na yenye mafunzo kwasababu tu ya watu fulani wajinga ambao hawataki kuniheshimu na kuanza kuniporomoshea matusi mazito,mimi kuwajibu imekuwa nongwa,hili halikubaliki hata kidogo moderators!.

Kuna muda tunachokozwa na kupandishwa hasira na wajinga kadhaa humu JF,sasa ajabu ni kwamba,mtu anapokutukana mara ya kwanza unamripoti hakuna hatua anayochukuliwa,mara ya pili pia ni vivyo hivyo,akikutukana mara ya tatu uzalendo unakushinda unamjibu,ukisha mjibu tu hapo ndipo Moderators wanakuja kuwaadhibu,wanashindwa kumuadhibu toka awali ulipomripoti wao wanakuja kumuadhibu ulipomjibu ambapo wanawaadhibu wote wanashindwa kumuadhibu mtoa matusi au muanzilishi wa matusi,hili halikubariki na nitaendelea kulipigia kelele.

Nimewahi kutoa mapendekezo kwenye uzi wangu mmoja uko kwenye Jukwaa la COMPLAINTS, APPRECIATION AND ADVICE(TO JF) nikasema tuwekeeni Blocking Button yenye nguvu na siyo hiyo Ignore iliyopo sasa,kwasababu kama nikishaona mtu ananitukana nitampiga Block ili aende akawatukane wazazi wake huko kwasababu wao ndiyo walimfundisha ujinga huo.

Aisee nimesikitishwa sana kupigwa BAN kwakosa ambalo limesabishwa na moja ya wapumbavu hapa JF.Wengine tunakiuka taratibu kwasababu ya kuchokozwa na siyo kwamba taratibu hatuzijui!.


Mimi ni mwema na nitaendelea kuwa mwema ila nikitukanwa lazima nijibu mapigo,kama ni kufungiwa nitafungiwa sana na nipo tayari kwa hilo!.

NIMESHINDWA KUSIMULIA STORI KWA SABABU YA WAJINGA KADHAA HAPA JF,HILI HALIKUBALIKI HATA KIDOGO NA NAUMIA SANA.

Huu ni ujumbe wenu Moderators najua uzi huu mnaupitia.


Ni hayo tu.
 
Haya mambo yakuchokozwa na kutukanwa na baadhi ya members humu halafu mimi nikimjibu nakula BAN sidhani kama imekaa sawa.Haiwezekani mtu anatoka huko anakokujua yeye anaanza kuniporomoshea matusi mazito halafu nimuangalie tu!.

Bado sijafikia kiwango hicho cha Utakatifu,kama ni nginja acha iwe nginja.

Wengine hatujaumbwa kuwa watukanaji,mimi nipo kuwaburudisha na kuwaelimisha hadhira yangu na umma wa watanzania wengi wanaojitambua,sasa anatokea mtu anaanza kukuporomoshea matusi ya nguoni kisa tu alikuja Inbox akaomba jambo fulani ukamnyima,ukimjibu kidogo tu anapelekea na wewe kufungiwa,hii siyo sawa moderators,wengine mnatuonea bila sababu ya msingi.

Kama nyuzi zangu zinakupa kero na huzipendi kwanini usipite ukatazame nyuzi zinazokufurahisha?,Kila mtu hapa anasoma anachoona kwake kina manufaa na anachokipenda,kama unaona hutaki usumbufu una-Block au Una - Ignore unaendelea na mishe zako,waachieni watu wanaotaka kujifunza na kuburudika wasome nyuzi zangu.

Hadhira yangu kwa muda wa siku zisizopungua 5 imeshindwa kupata simulizi nzuri na yenye mafunzo kwasababu tu ya watu fulani wajinga ambao hawataki kuniheshimu na kuanza kuniporomoshea matusi mazito,mimi kuwajibu imekuwa nongwa,hili halikubaliki hata kidogo moderators!.

Kuna muda tunachokozwa na kupandishwa hasira na wajinga kadhaa humu JF,sasa ajabu ni kwamba,mtu anapokutukana mara ya kwanza unamripoti hakuna hatua anayochukuliwa,mara ya pili pia ni vivyo hivyo,akikutukana mara ya tatu uzalendo unakushinda unamjibu,ukisha mjibu tu hapo ndipo Moderators wanakuja kuwaadhibu,wanashindwa kumuadhibu toka awali ulipomripoti wao wanakuja kumuadhibu ulipomjibu ambapo wanawaadhibu wote wanashindwa kumuadhibu mtoa matusi au muanzilishi wa matusi,hili halikubariki na nitaendelea kulipigia kelele.

Nimewahi kutoa mapendekezo kwenye uzi wangu mmoja uko kwenye Jukwaa la COMPLAINTS, APPRECIATION AND ADVICE(TO JF) nikasema tuwekeeni Blocking Button yenye nguvu na siyo hiyo Ignore iliyopo sasa,kwasababu kama nikishaona mtu ananitukana nitampiga Block ili aende akawatukane wazazi wake huko kwasababu wao ndiyo walimfundisha ujinga huo.

Aisee nimesikitishwa sana kupigwa BAN kwakosa ambalo limesabishwa na moja ya wapumbavu hapa JF.Wengine tunakiuka taratibu kwasababu ya kuchokozwa na siyo kwamba taratibu hatuzijui!.


Mimi ni mwema na nitaendelea kuwa mwema ila nikitukanwa lazima nijibu mapigo,kama ni kufungiwa nitafungiwa sana na nipo tayari kwa hilo!.

NIMESHINDWA KUSIMULIA STORI KWA SABABU YA WAJINGA KADHAA HAPA JF,HILI HALIKUBALIKI HATA KIDOGO NA NAUMIA SANA.

Huu ni ujumbe wenu Moderators najua uzi huu mnaupitia.


Ni hayo tu.
Mkuu karibu
Sisi kama fans wako tumekusubiria sana
Naomba tuendelee na story
 
SEHEMU YA NNE




Tulipanda kwenye zile bodaboda na safari ya kuelekea makaburini ili kazi ya kuanza kuaga mizimu ya mababu zetu wa kitanzania ichukue nafasi.Tulipofika jirani na lile eneo la makaburi,Jentre aliwaambia Bodaboda wasimame tushuke kisha watusubiri tukakamilishe jambo letu halafu tuondoke.

Tulipofika pale makaburini Jentre alituambia kila mtu atafute kaburi ambalo lilikuwa bado halijasakafiwa na ambalo bado lilikuwa halina siku nyingi tangu shughuli ya mazishi ifanyike.Baada ya kuwa kila mtu amepata kaburi lake,ndipo Jentre akatupa ishara ya kwamba tuvue nguo na tubaki kama tulivyozaliwa.

Jentre "Kamata hii"

Aliendelea "Naomba uniambie ndugu zako waolikwisha kufa"

Mimi "Babu,Baba wakubwa kadhaa,Bibi mzaa mama,mama wadogo pamoja na wajomba ikiwemo watoto na ndugu kadhaa"

Jentre "Sasa chukua hicho kijiti nilichokupatia kisha utahesabu kutoka miguuni mwa hili kaburi hatua kumi,kisha utachukua hicho kijiti utachimba hapohapo ulipofikia kuhesabu hatua zako hizo kumi"


Aliendelea "Hakikisha shimo utakalo chimba liwe saizi ya kiganja cha mkono wako"


Baada ya kutamka maneno hayo aliondoka kwangu akaelekea kwa Kamugisha ambaye alikuwa mbali kidogo na mimi,sasa mkononi Jentre alinipatia Pemba nyeupe pamoja na kijiti kidogo chenye makadirio kama Centimeter 15.Sasa kwenye Kaburi lolote lile huwa kuna ile sehemu ambayo misalaba huwekwa na kuandikwa majina,hapo mara zote huwa tunaita kichwani na kule ambako hakuna kibao cha majina wala msalaba huwa tunaita miguuni,sasa jamaa akawa ameniambia nichukue kile kijiti cha senitimita 15 alichokuwa amenipatia nikipime kuanzia sehemu ya miguu ya lile kaburi kwa hatua ya vijiti kumi,yaani Sentimita 150 kisha hapo katikati zitakapofikia hizo hatua za vijiti ndipo nichimbe kishimo kidogo ambacho nikizamisha kiganja cha mkono wangu kiishilie chote.

Hivyo ndivyo nilivyofanya na baada ya kumaliza niliendelea kuchuchumaa pale chini nikimsubiri aje anipe maelekezo ya kufanya;Alipomalizana na Kamugisha alinirudia ndipo akaanza kuniambia nitamke maneno kadhaa atakayonielekeza yeye.

Jentre "Naomba unifuatishe maneno haya,Babu zangu,Bibi zangu,wajomba zangu,ndugu zangu wote mliofikwa na mauti,kijana wenu ninarudi kwenu naombeni baraka zenu,nimekuja kuwaaga mimi nasafiri kuelekea Congo,hivyo ninaomba baraka zenu ili nivuke salama na nikafanikishe mambo yangu"

Baada ya kuyatamka maneno hayo na mimi niliyarudia kama alivyokuwa ameniambia,nilipomaliza kuyatamka maneno hayo alichukua ile pemba nyeupe aliyokuwa nayo mkononi akanipatia akaniambia niitupe kwenye kile kishimo nilichokuwa nimekichimba pamoja na kile kijiti kisha nifukie.

Jentre "Haya lizunguke hilo kaburi mara kumi ukirudi kinyumenyume"

Nilifanya kama alivyoniambia na baada ya kumaliza aliniambia nisimame niende nikavae nguo kisha nimsubiri akamlizane na Kamugisha kisha tuondoke zetu.Baada ya lile zoezi kuwa limekamilika kwa wote wawili,jamaa alitushika mikono kwa pamoja kisha akaanza kuongea maneno aliyokuwa akiyafahamu yeye kwa lugha ya Lingala na French.

Tulipomaliza huo mchakato tuliondoka zetu kurudi hotelini na jamaa yeye aliondoka kwenda kwake.

Asubuhi kulivyopambazuka Seif alimpigia simu Kamugisha na kumwambia inabidi tufanye harakati za kuvuka kwasababu ile Boti ambayo tulipaswa kuondoka nayo ilikuwa inaondoka baada ya kukamilisha zoezi la upakiaji wa mizigo.Tuliondoka tukaelekea zilipo ofisi za uhamiaji na kuacha documenti zetu pale tukaambiwa tutaletewa kwenye boti ambayo tulikuwa tukisafiri nayo.

Ilipofika muda wa saa 8 mchana,Seif alitubeba kwenye mtumbwi wake uliokuwa umefungwa injini kutuvusha kuelekea kisiwani ambako ndiko ile boti kubwa tuliyokuwa tunaondoka nayo ingetukuta hapo,kwenye ule mtumbwi wa Seif kulikuwa pia na abiria wengine ukiacha sisi.

Seif "Nawapeleka kwenye kile kisiwa pale,jamaa wanaenda kupakia mizigo mingine kwenye bandari ya Kipili,wakimaliza watawachukulia pale muondoke zenu!"

Kamugisha "Hakuna tatizo"


Kulikuwa kuna kisiwa kikubwa sana kinaitwa Mandakerege ambacho ndicho bwana Seif alituacha hapo akatuambia wale jamaa wa ile Boti wangemaliza kupakia mizigo pale bandari ya Kirando walikuwa wanaelekea bandari ya Kipili iliyokuwa kushoto mwa Kirando wakapakie mzigo mwingine kisha ndiyo tusepe zetu Congo.

Kwakuwa tuliambiwa ziwani tungekaa siku zaidi ya moja kulingana na hali ya hewa,tulichukua soda za kopo pamoja na maandazi ya kutosha kama dharura endapo kungetokea jambo lolote.Kiukweli ndugu zangu kwakuwa ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika ziwa Tanganyika na kuliona,asikwambie mtu si ziwa la kawaida hata kidogo,kwa wale waliofanikiwa kuliona hata kulipita watakubaliana nami!.

Ingawa wajuvi wa mambo ya majini wanasema ziwa lile lina unafuu mkubwa kuliko ziwa Victoria lakini mimi kwakuwa maziwa yote mawili nimeshayashuhudia kwa macho;kwa upande wangu ziwa Tanganyika ni hatari kuliko ziwa Victoria,nina maana yangu kusema hivyo.

Basi bhana,tulikaa pale Mandakerege hadi mida ya saa 11 jioni,baada ya ile boti kumaliza kupakia shehena ya mzigo pale Kipili ilikuja kutuchukua pale.Kiukweli sikuwahi kuona Boti limebeba shehena ya mzigo kama lile,nilipoliona kwanza nikaingiwa na hofu nikajikuta tu nauliza wenzangu!.

Mimi "Sasa lilivyojaza mzigo hivyo tutakaa wapi?,au kwachini kuna nafasi ya abiria kukaa?"

Jamaa mmoja "Ndiyo mara yako ya kwanza kusafiri nini!"

Mimi "Yes,hii ndiyo mara ya kwanza"

Jamaa "Abiria wote wanakaa juu ya huo mzigo"

Baada ya jamaa kuniambia vile nilitaka kabisa kugoma kupanda lile boti,roho yangu ilijaa hofu sana na kiukweli nilivyokuwa nikidhani ndivyo ilivyokuwa.Basi nilipiga moyo konde na nikajikaza kisabuni kijana wa Kikurya kisha baada ya kuitwa majina nikazama kwenye chombo.Ile boti ilikuwa imekula mzigo hadi ule mstari wa ujazo ukawa umepitwa na maji,ilikuwa ukiinama kidogo unayashika maji na mkono.Kiukweli mimi ni jasiri lakini hofu kuu ilitanda ndani ya moyo wangu,nilikuwa nikimuangalia Kamugisha yeye hakuwa na hofu yeyote kana kwamba alikuwa akiifurahia ile safari.

Jamaa wa Boti "Jamani nadhani muanze kunipatia nauli"

Kila mmoja alimpatia nauli ambayo ilikuwa shilingi elfu 30 kwa mtu mmoja.Baada ya kukamilisha mambo yao Boti iling'oa nanga mida ya saa 12 jioni kuelekea upande wa Congo.

Kadiri tulivyokuwa tukiyakata maji ndivyo hali ya hewa nayo ilianza kubadirika na kusababisha mawimbi makubwa yaliyokuwa yakiyumbisha ile boti kwa kiasi kikubwa;Upande wangu kiukweli nilikuwa napata taabu sana kwa hofu hadi upumuaji ukawa ni changamoto,sikuwahi kushuhudia hali kama ile tangu nimezaliwa.

Muendeshaji wa ile Boti alipoona hali imeanza kuwa mbaya aliipelekea kando ya kile kisiwa cha Mandakerege kwa upande wa nyuma kwasababu tulikuwa tushaviacha vijiji kadhaa nyuma,alipofika hapo alianza kuwasiliana na watu wa upande wa Congo kuwauliza kama kwa upande ule hali ya hewa inaweza kuwa nzuri tuondoke mdogo mdogo,sasa nadhani wale jamaa wa Moba walimwambia aende mdogo mdogo hali ya hewa si nzuri kwasababu kulikuwa kuna kitu wanakiita wao "KUSI".

Sasa hiyo KUSI ilikuwa ni aina ya upepo mbaya sana ambao ulikuwa unapiga kutokea Kusini kuelekea Kaskazini na Mashariki,Upepo huu ni mbaya zaidi kwa mujibu wao na wajuvi walikuwa wanasema ni heri ukutwe na Upepo utokao KASKAZ kuliko kukutwa na hiyo kitu iitwayo KUSI,ilikuwa ni hatari sana.

Basi baada ya jamaa muendesha chombo kujiridhisha aliamua kuondoa chombo mdogo mdogo,kadiri tulivyokuwa tunaviacha visiwa vya Tanzania giza totoro na upepo mkali vilikuwa vikitusumbua kwa sana tu.

Tuliyakata maji kwa shida sana usiku huo kwa kuwa kulikuwa na mawimbi makali mno,ilipofika mida ya saa 6 usiku tukafika sehemu ambayo wao wanaiita GEZI,hiyo GEZI ni katikati ya TANZANIA na CONGO na ndipo kwenye mkondo mkali mno wa maji,huwa mkivuka salama eneo hilo mnapaswa kumshukuru Mungu kwa kuwavusha salama na kama wewe ni muabudu mizimu basi inapaswa uishukuru Mizimu ya kwenu.

Haikuchukua muda hali ikabadirika sana na kupitia mawimbi yale makali yaliyokuwa yakiipiga ile boti,nahodha wa chombo aliamua kuzima injini kwasababu hali ilikuwa mbaya,sasa kumbe kuzima injini jamaa ni kama alifanya makosa makubwa mno,Kuna Wimbi lilikuja likatuchota likatuzungusha ile boti ikaangalia ilipotokea,kiukweli kila mtu alikuwa anamuomba Mungu kwa namna alivyokuwa anajua yeye,jamaa muendesha chombo alipoona boti imegeuzwa na mawimbi alikiwasha chombo tukawa tunarudi tena Tanzania,sasa kumbe yale mawimbi yalitikisa ubao ukawa unapitisha maji kwa chini kwa kasi ya ajabu.Wale wasaidizi wake wakaanza kupiga kelele kwa nguvu sana.

Wasaidizi "Mwambieni Ustaadhi maji yanaingia ndaniiiiii !"

Waliendelea "Mwambie ustadhi maji yanaingia ndaniiiiiiii !"

Kwakuwa wao walikuwa mbele kabisa walitaka tupaze sauti kumwambia muendesha chombo aliyekuwa akiitwa Ustadhi,ya kwamba ajaribu kuwa makini kwasababu maji yanaingia ndani.Watu waliokuwa nyuma kwenye injini walijaribu kumwambia jamaa na yeye akawaambia wawashe majenereta ya kuvuta maji na kuyatoa nje.

Wasaidizi " Maji ni mengi mno na mashine zinazidiwa"

Baada ya kuona hali inakuwa mbaya,kuna jamaa ambao walikuwa na mizigo yao kwenye ile boti walianza kuvua nguo wakabaki na kaptura pekee kisha wakaanza kupiga kelele ya kwamba wanaume wote tuingie chini tukasaidie kutoa maji kwa nguvu zote kupitia ndoo zilizokuwa huko kwasababu ile mashine iliilemewa.


Inaendelea......................
 
SEHEMU YA NNE




Tulipanda kwenye zile bodaboda na safari ya kuelekea makaburini ili kazi ya kuanza kuaga mizimu ya mababu zetu wa kitanzania ichukue nafasi.Tulipofika jirani na lile eneo la makaburi,Jentre aliwaambia Bodaboda wasimame tushuke kisha watusubiri tukakamilishe jambo letu halafu tuondoke.

Tulipofika pale makaburini Jentre alituambia kila mtu atafute kaburi ambalo lilikuwa bado halijasakafiwa na ambalo bado lilikuwa halina siku nyingi tangu shughuli ya mazishi ifanyike.Baada ya kuwa kila mtu amepata kaburi lake,ndipo Jentre akatupa ishara ya kwamba tuvue nguo na tubaki kama tulivyozaliwa.

Jentre "Kamata hii"

Aliendelea "Naomba uniambie ndugu zako walikwisha kufa"

Mimi "Babu,Baba wakubwa kadhaa,Bibi mzaa mama,mama wadogo pamoja na wajomba ikiwemo watoto na ndugu kadhaa"

Jentre "Sasa chukua hicho kijiti nilichokupatia kisha utahesabu kutoka miguuni mwa hili kaburi hatua kumi,kisha utachukua hicho kijiti utachimba hapohapo ulipofikia kuhesabu hatua zako hizo kumi"


Aliendelea "Hakikisha shimo utakalo chimba liwe saizi ya kiganja cha mkono wako"


Baada ya kutamka maneno hayo aliondoka kwangu akaelekea kwa Kamugisha ambaye alikuwa mbali kidogo na mimi,sasa mkononi Jentre alinipatia Pemba nyeupe pamoja na kijiti kidogo chenye makadirio kama Centimeter 15.Sasa kwenye Kaburi lolote lile huwa kuna ile sehemu ambayo misalaba huwekwa na kuandikwa majina,hapo mara zote huwa tunaita kichwani na kule ambako hakuna kibao cha majina wala msalaba huwa tunaita miguuni,sasa jamaa akawa ameniambia nichukue kile kijiti cha senitimita 15 alichokuwa amenipatia nikipime kuanzia sehemu ya miguu ya lile kaburi kwa hatua ya vijiti kumi,yaani Sentimita 150 kisha hapo katikati zitakapofikia hizo hatua za vijiti ndipo nichimbe kishimo kidogo ambacho nikizamisha kiganja cha mkono wangu kiishilie chote.

Hivyo ndivyo nilivyofanya na baada ya kumaliza niliendelea kuchuchumaa pale chini nikimsubiri aje anipe maelekezo ya kufanya;Alipomalizana na Kamugisha alinirudia ndipo akaanza kuniambia nitamke maneno kadhaa atakayonielekeza yeye.

Jentre "Naomba unifuatishe maneno haya,Babu zangu,Bibi zangu,wajomba zangu,ndugu zangu wote mliofikwa na mauti,kijana wenu ninarudi kwenu naombeni baraka zenu,nimekuja kuwaaga mimi nasafiri kuelekea Congo,hivyo ninaomba baraka zenu ili nivuke salama na nikafanikishe mambo yangu"

Baada ya kuyatamka maneno hayo na mimi niliyarudia kama alivyokuwa ameniambia,nilipomaliza kuyatamka maneno hayo kuna alichukua ile pemba nyeupe aliyokuwa nayo mkononi akanipatia akaniambia niitupe kwenye kile kishimo nilichokuwa pamoja na kile kijiti kisha nifukie.

Jentre "Haya lizunguke hilo kaburi mara kumi ukirudi kinyumenyume"

Nilifanya kama alivyoniambia na baada ya kumaliza aliniambia nisimame niende nikavae nguo kisha nimsubiri akamlizane na Kamugisha kisha tuondoke zetu.Baada ya lile zoezi kuwa limekamilika kwa wote wawili,jamaa alitushika mikono kwa pamoja kisha akaanza kuongea maneno aliyokuwa akiyafahamu yeye kwa lugha ya Lingala na French.

Tulipomaliza huo mchakato tuliondoka zetu kurudi hotelini na jamaa yeye aliondoka kwenda kwake.

Asubuhi kulivyopambazuka Seif alimpigia simu Kamugisha na kumwambia inabidi tufanye harakati za kuvuka kwasababu ile Boti ambayo tulipaswa kuondoka nayo ilikuwa inaondoka baada ya kukamilisha zoezi la upakiaji wa mizigo.Tuliondoka tukaelekea zilipo ofisi za uhamiaji na kuacha documenti zetu pale tukaambiwa tutaletewa kwenye boti ambayo tulikuwa tukisafiri nayo.

Ilipofika muda wa saa nane mchana,Seif alitubeba kwenye mtumbwi wake uliokuwa umefungwa injini,kwenye mtumbwi huo tulikuwa abiria wengi.

Seif "Nawapeleka kwenye kile kisiwa pale,jamaa wanaenda kupakia mizigo mingine kwenye bandari ya Kipili,wakimaliza watawachukulia pale muondoke zenu!"

Kamugisha "Hakuna tatizo"


Kulikuwa kuna kisiwa kikubwa sana kinaitwa Mandakerege ambacho ndicho bwana Seif alituacha hapo akatuambia wale jamaa wa ile Boti wangemaliza kupakia mizigo pale bandari ya Kirando walikuwa wanaelekea bandari ya Kipili iliyokuwa kushoto mwa kirando wakapakie mzigo mwingine kisha ndiyo tusepe zetu Congo.

Kwakuwa tuliambiwa ziwani tungekaa siku zaidi ya moja kulingana na hali ya hewa,tulichukua soda za kopo pamoja na maandazi ya kutosha kama dharura endapo kungetokea jambo lolote.Kiukweli ndugu zangu kwakuwa ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika ziwa Tanganyika na kuliona,asikwambie mtu si ziwa la kawaida hata kidogo,kwa wale waliofanikiwa kuliona hata kulipita watakubaliana nami!.

Ingawa wajuvi wa mambo ya majini wanasema ziwa lile lina unafuu mkubwa kuliko ziwa Victoria lakini mimi kwakuwa maziwa yote mawili nimeshayashuhudia kwa macho,kwa upande wangu ziwa Tanganyika ni hatari kuliko ziwa Victoria,nina maana yangu kusema hivyo.

Basi bhana,tulikaa pale Mandakerege hadi mida ya saa 11 jioni,baada ya ile boti kumaliza kupakia shehena ya mzigo pale Kipili ilikuja kutuchukua pale.Kiukweli sikuwahi kuona Boti limebeba shehena ya mzigo kama lile,nilipoliona kwanza nikaingiwa na hofu nikajikuta tu nauliza wenzangu!.

Mimi "Sasa lilivyojaza mzigo hivyo tutakaa wapi?,au kwachini kuna nafasi ya abiria kukaa?"

Jamaa mmoja "Ndiyo mara kwanza nini kusafiri"

Mimi "Yes,hii ndiyo mara ya kwanza"

Jamaa "Abiria wote wanakaa juu ya huo mzigo"

Baada ya jamaa kuniambia vile nilitaka kabisa kugoma kupanda lile boti,roho yangu ilijaa sana hofu na kiukweli nilivyokuwa nikidhani ndivyo ilivyokuwa.Basi nilipiga moyo konde na nikajikaza kisabuni kijana wa Kikurya kisha baada ya kuitwa majina nikazama kwenye chombo.Ile boti ilikuwa imekula mzigo hadi ule mstari wa ujazo ukawa umepitwa na maji,ilikuwa ukiinama kidogo unayashika maji na mkono.Kiukweli mimi ni jasiri lakini hofu kuu ilitanda ndani ya moyo wangu,nilikuwa nikimuangalia Kamugisha yeye hakuwa na hofu yeyote kana kwamba alikuwa akiifurahia ile safari.

Jamaa wa Boti "Jamani nadhani muanze kunipatia nauli"

Kila mmoja alimpatia nauli ambayo ilikuwa shilingi elfu 30 kwa mtu mmoja.Baada ya kukamilisha mambo yao Boti iling'oa nanga mida ya saa 12 jioni kuelekea upande wa Congo.

Kadiri tulivyokuwa tukiyakata maji ndivyo hali ya hewa nayo ilianza kubadirika na kusababisha mawimbi makubwa yaliyokuwa yakiyumbisha ile boti kwa kiasi kikubwa;Upande wangu kiukweli nilikuwa napata taabu sana kwa hofu hadi upumuaji ukawa ni changamoto,sikuwahi kushuhudia hali kama ile tangu nimezaliwa.

Muendeshaji wa ile Boti alipoona hali imeanza kuwa mbaya aliipelekea kando ya kile kisiwa cha Mandakerege kwa upande wa nyuma kwasababu tulikuwa tushaviacha vijiji kadhaa nyuma,alipofika hapo alianza kuwasiliana na watu wa upande wa Congo kuwauliza kama kwa upande ule hali ya hewa inaweza kuwa nzuri tuondoke mdogo mdogo,sasa nadhani wale jamaa wa Moba walimwambia aende mdogo mdogo hali ya hewa si nzuri kwasababu kulikuwa kuna kitu wanakiita wao "KUSI".

Sasa hiyo KUSI ilikuwa ni aina ya upepo mbaya sana ambao ulikuwa unapiga kutokea Kusini kuelekea Kaskazini na Mashariki,Upepo huu ni mbaya zaidi kwa mujibu wao na wajuvi walikuwa wanasema ni heri ukutwe na Upepo utokao KASKAZ kuliko kukutwa na hiyo kitu iitwayo KUSI,ilikuwa ni hatari sana.

Basi baada ya jamaa muendesha chombo kujiridhisha aliamua kuondoa chombo mdogo mdogo,kadiri tulivyokuwa tunaviacha visiwa vya Tanzania giza totoro na upepo mkali vilikuwa vikitusumbua kwa sana tu.

Tuliyakata maji kwa shida sana usiku huo kwa kuwa kulikuwa na mawimbi makali mno,ilipofika mida ya saa 6 usiku tukafika sehemu ambayo wao wanaiita GEZI,hiyo GEZI ni katikati ya TANZANIA na CONGO na ndipo kwenye mkondo mkali mno wa maji,huwa mkivuka salama eneo hilo mnapaswa kumshukuru Mungu kwa kuwavusha salama na kama wewe ni muabudu mizimu basi inapaswa uishukuru Mizimu ya kwenu.

Haikuchukua muda hali ikabadirika sana na kupitia mawimbi yale makali yaliyokuwa yakiipiga boti ile,nahodha wa chombo aliamua kuzima injini kwasababu hali ilikuwa mbaya,sasa kumbe kuzima injini jamaa ni kama alifanya makosa makubwa mno,Kuna Wimbi lilikuja likatuchota likatuzungusha ile boti ikaangalia ilipotokea,kiukweli kila mtu alikuwa anamuomba Mungu kwa namna alivyokuwa anajua yeye,jamaa muendesha chombo alipoona boti imegeuzwa na mawimbi alikiwasha chombo tukawa tunarudi tena Tanzania,sasa kumbe yale mawimbi yalitikisa ubao ukawa unapitisha maji kwa chini kwa kasi ya ajabu.Wale wasaidizi wake wakaanza kupiga kelele kwa nguvu sana.

Wasaidizi "Mwambieni Ustaadhi maji yanaingia ndaniiiiii "

Waliendelea "Mwambie ustadhi maji yanaingia ndaniiiiiiii !!"

Kwakuwa wao walikuwa mbele kabisa walitaka tupaze sauti kumwambia muendesha chombo aliyekuwa akiitwa Ustadhi,ya kwamba ajaribu kuwa makini kwasababu maji yanaingia ndani.Watu waliokuwa nyuma kwenye injini walijaribu kumwambia jamaa na yeye akawaambia wawashe majenereta ya kuvuta maji na kuyatoa nje.

Wasaidizi " Maji ni mengi mno na mashine zinazidiwa"

Baada ya kuona hali inakuwa mbaya,kuna jamaa ambao walikuwa na mizigo yao kwenye ile boti walianza kuvua nguo wakabaki na kaptura pekee kisha wakaanza kupiga kelele ya kwamba wanaume wote tuingie chini tukasaidie kutoa maji kwa nguvu zote kupitia ndoo zilizokuwa huko kwasababu ile mashine iliilemewa.


Inaendelea......................
Daaah, poleni sana mkuu, utafutaji ndivyo ulivyo.
 
SEHEMU YA NNE




Tulipanda kwenye zile bodaboda na safari ya kuelekea makaburini ili kazi ya kuanza kuaga mizimu ya mababu zetu wa kitanzania ichukue nafasi.Tulipofika jirani na lile eneo la makaburi,Jentre aliwaambia Bodaboda wasimame tushuke kisha watusubiri tukakamilishe jambo letu halafu tuondoke.

Tulipofika pale makaburini Jentre alituambia kila mtu atafute kaburi ambalo lilikuwa bado halijasakafiwa na ambalo bado lilikuwa halina siku nyingi tangu shughuli ya mazishi ifanyike.Baada ya kuwa kila mtu amepata kaburi lake,ndipo Jentre akatupa ishara ya kwamba tuvue nguo na tubaki kama tulivyozaliwa.

Jentre "Kamata hii"

Aliendelea "Naomba uniambie ndugu zako walikwisha kufa"

Mimi "Babu,Baba wakubwa kadhaa,Bibi mzaa mama,mama wadogo pamoja na wajomba ikiwemo watoto na ndugu kadhaa"

Jentre "Sasa chukua hicho kijiti nilichokupatia kisha utahesabu kutoka miguuni mwa hili kaburi hatua kumi,kisha utachukua hicho kijiti utachimba hapohapo ulipofikia kuhesabu hatua zako hizo kumi"


Aliendelea "Hakikisha shimo utakalo chimba liwe saizi ya kiganja cha mkono wako"


Baada ya kutamka maneno hayo aliondoka kwangu akaelekea kwa Kamugisha ambaye alikuwa mbali kidogo na mimi,sasa mkononi Jentre alinipatia Pemba nyeupe pamoja na kijiti kidogo chenye makadirio kama Centimeter 15.Sasa kwenye Kaburi lolote lile huwa kuna ile sehemu ambayo misalaba huwekwa na kuandikwa majina,hapo mara zote huwa tunaita kichwani na kule ambako hakuna kibao cha majina wala msalaba huwa tunaita miguuni,sasa jamaa akawa ameniambia nichukue kile kijiti cha senitimita 15 alichokuwa amenipatia nikipime kuanzia sehemu ya miguu ya lile kaburi kwa hatua ya vijiti kumi,yaani Sentimita 150 kisha hapo katikati zitakapofikia hizo hatua za vijiti ndipo nichimbe kishimo kidogo ambacho nikizamisha kiganja cha mkono wangu kiishilie chote.

Hivyo ndivyo nilivyofanya na baada ya kumaliza niliendelea kuchuchumaa pale chini nikimsubiri aje anipe maelekezo ya kufanya;Alipomalizana na Kamugisha alinirudia ndipo akaanza kuniambia nitamke maneno kadhaa atakayonielekeza yeye.

Jentre "Naomba unifuatishe maneno haya,Babu zangu,Bibi zangu,wajomba zangu,ndugu zangu wote mliofikwa na mauti,kijana wenu ninarudi kwenu naombeni baraka zenu,nimekuja kuwaaga mimi nasafiri kuelekea Congo,hivyo ninaomba baraka zenu ili nivuke salama na nikafanikishe mambo yangu"

Baada ya kuyatamka maneno hayo na mimi niliyarudia kama alivyokuwa ameniambia,nilipomaliza kuyatamka maneno hayo kuna alichukua ile pemba nyeupe aliyokuwa nayo mkononi akanipatia akaniambia niitupe kwenye kile kishimo nilichokuwa pamoja na kile kijiti kisha nifukie.

Jentre "Haya lizunguke hilo kaburi mara kumi ukirudi kinyumenyume"

Nilifanya kama alivyoniambia na baada ya kumaliza aliniambia nisimame niende nikavae nguo kisha nimsubiri akamlizane na Kamugisha kisha tuondoke zetu.Baada ya lile zoezi kuwa limekamilika kwa wote wawili,jamaa alitushika mikono kwa pamoja kisha akaanza kuongea maneno aliyokuwa akiyafahamu yeye kwa lugha ya Lingala na French.

Tulipomaliza huo mchakato tuliondoka zetu kurudi hotelini na jamaa yeye aliondoka kwenda kwake.

Asubuhi kulivyopambazuka Seif alimpigia simu Kamugisha na kumwambia inabidi tufanye harakati za kuvuka kwasababu ile Boti ambayo tulipaswa kuondoka nayo ilikuwa inaondoka baada ya kukamilisha zoezi la upakiaji wa mizigo.Tuliondoka tukaelekea zilipo ofisi za uhamiaji na kuacha documenti zetu pale tukaambiwa tutaletewa kwenye boti ambayo tulikuwa tukisafiri nayo.

Ilipofika muda wa saa nane mchana,Seif alitubeba kwenye mtumbwi wake uliokuwa umefungwa injini,kwenye mtumbwi huo tulikuwa abiria wengi.

Seif "Nawapeleka kwenye kile kisiwa pale,jamaa wanaenda kupakia mizigo mingine kwenye bandari ya Kipili,wakimaliza watawachukulia pale muondoke zenu!"

Kamugisha "Hakuna tatizo"


Kulikuwa kuna kisiwa kikubwa sana kinaitwa Mandakerege ambacho ndicho bwana Seif alituacha hapo akatuambia wale jamaa wa ile Boti wangemaliza kupakia mizigo pale bandari ya Kirando walikuwa wanaelekea bandari ya Kipili iliyokuwa kushoto mwa kirando wakapakie mzigo mwingine kisha ndiyo tusepe zetu Congo.

Kwakuwa tuliambiwa ziwani tungekaa siku zaidi ya moja kulingana na hali ya hewa,tulichukua soda za kopo pamoja na maandazi ya kutosha kama dharura endapo kungetokea jambo lolote.Kiukweli ndugu zangu kwakuwa ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika ziwa Tanganyika na kuliona,asikwambie mtu si ziwa la kawaida hata kidogo,kwa wale waliofanikiwa kuliona hata kulipita watakubaliana nami!.

Ingawa wajuvi wa mambo ya majini wanasema ziwa lile lina unafuu mkubwa kuliko ziwa Victoria lakini mimi kwakuwa maziwa yote mawili nimeshayashuhudia kwa macho,kwa upande wangu ziwa Tanganyika ni hatari kuliko ziwa Victoria,nina maana yangu kusema hivyo.

Basi bhana,tulikaa pale Mandakerege hadi mida ya saa 11 jioni,baada ya ile boti kumaliza kupakia shehena ya mzigo pale Kipili ilikuja kutuchukua pale.Kiukweli sikuwahi kuona Boti limebeba shehena ya mzigo kama lile,nilipoliona kwanza nikaingiwa na hofu nikajikuta tu nauliza wenzangu!.

Mimi "Sasa lilivyojaza mzigo hivyo tutakaa wapi?,au kwachini kuna nafasi ya abiria kukaa?"

Jamaa mmoja "Ndiyo mara kwanza nini kusafiri"

Mimi "Yes,hii ndiyo mara ya kwanza"

Jamaa "Abiria wote wanakaa juu ya huo mzigo"

Baada ya jamaa kuniambia vile nilitaka kabisa kugoma kupanda lile boti,roho yangu ilijaa sana hofu na kiukweli nilivyokuwa nikidhani ndivyo ilivyokuwa.Basi nilipiga moyo konde na nikajikaza kisabuni kijana wa Kikurya kisha baada ya kuitwa majina nikazama kwenye chombo.Ile boti ilikuwa imekula mzigo hadi ule mstari wa ujazo ukawa umepitwa na maji,ilikuwa ukiinama kidogo unayashika maji na mkono.Kiukweli mimi ni jasiri lakini hofu kuu ilitanda ndani ya moyo wangu,nilikuwa nikimuangalia Kamugisha yeye hakuwa na hofu yeyote kana kwamba alikuwa akiifurahia ile safari.

Jamaa wa Boti "Jamani nadhani muanze kunipatia nauli"

Kila mmoja alimpatia nauli ambayo ilikuwa shilingi elfu 30 kwa mtu mmoja.Baada ya kukamilisha mambo yao Boti iling'oa nanga mida ya saa 12 jioni kuelekea upande wa Congo.

Kadiri tulivyokuwa tukiyakata maji ndivyo hali ya hewa nayo ilianza kubadirika na kusababisha mawimbi makubwa yaliyokuwa yakiyumbisha ile boti kwa kiasi kikubwa;Upande wangu kiukweli nilikuwa napata taabu sana kwa hofu hadi upumuaji ukawa ni changamoto,sikuwahi kushuhudia hali kama ile tangu nimezaliwa.

Muendeshaji wa ile Boti alipoona hali imeanza kuwa mbaya aliipelekea kando ya kile kisiwa cha Mandakerege kwa upande wa nyuma kwasababu tulikuwa tushaviacha vijiji kadhaa nyuma,alipofika hapo alianza kuwasiliana na watu wa upande wa Congo kuwauliza kama kwa upande ule hali ya hewa inaweza kuwa nzuri tuondoke mdogo mdogo,sasa nadhani wale jamaa wa Moba walimwambia aende mdogo mdogo hali ya hewa si nzuri kwasababu kulikuwa kuna kitu wanakiita wao "KUSI".

Sasa hiyo KUSI ilikuwa ni aina ya upepo mbaya sana ambao ulikuwa unapiga kutokea Kusini kuelekea Kaskazini na Mashariki,Upepo huu ni mbaya zaidi kwa mujibu wao na wajuvi walikuwa wanasema ni heri ukutwe na Upepo utokao KASKAZ kuliko kukutwa na hiyo kitu iitwayo KUSI,ilikuwa ni hatari sana.

Basi baada ya jamaa muendesha chombo kujiridhisha aliamua kuondoa chombo mdogo mdogo,kadiri tulivyokuwa tunaviacha visiwa vya Tanzania giza totoro na upepo mkali vilikuwa vikitusumbua kwa sana tu.

Tuliyakata maji kwa shida sana usiku huo kwa kuwa kulikuwa na mawimbi makali mno,ilipofika mida ya saa 6 usiku tukafika sehemu ambayo wao wanaiita GEZI,hiyo GEZI ni katikati ya TANZANIA na CONGO na ndipo kwenye mkondo mkali mno wa maji,huwa mkivuka salama eneo hilo mnapaswa kumshukuru Mungu kwa kuwavusha salama na kama wewe ni muabudu mizimu basi inapaswa uishukuru Mizimu ya kwenu.

Haikuchukua muda hali ikabadirika sana na kupitia mawimbi yale makali yaliyokuwa yakiipiga boti ile,nahodha wa chombo aliamua kuzima injini kwasababu hali ilikuwa mbaya,sasa kumbe kuzima injini jamaa ni kama alifanya makosa makubwa mno,Kuna Wimbi lilikuja likatuchota likatuzungusha ile boti ikaangalia ilipotokea,kiukweli kila mtu alikuwa anamuomba Mungu kwa namna alivyokuwa anajua yeye,jamaa muendesha chombo alipoona boti imegeuzwa na mawimbi alikiwasha chombo tukawa tunarudi tena Tanzania,sasa kumbe yale mawimbi yalitikisa ubao ukawa unapitisha maji kwa chini kwa kasi ya ajabu.Wale wasaidizi wake wakaanza kupiga kelele kwa nguvu sana.

Wasaidizi "Mwambieni Ustaadhi maji yanaingia ndaniiiiii "

Waliendelea "Mwambie ustadhi maji yanaingia ndaniiiiiiii !!"

Kwakuwa wao walikuwa mbele kabisa walitaka tupaze sauti kumwambia muendesha chombo aliyekuwa akiitwa Ustadhi,ya kwamba ajaribu kuwa makini kwasababu maji yanaingia ndani.Watu waliokuwa nyuma kwenye injini walijaribu kumwambia jamaa na yeye akawaambia wawashe majenereta ya kuvuta maji na kuyatoa nje.

Wasaidizi " Maji ni mengi mno na mashine zinazidiwa"

Baada ya kuona hali inakuwa mbaya,kuna jamaa ambao walikuwa na mizigo yao kwenye ile boti walianza kuvua nguo wakabaki na kaptura pekee kisha wakaanza kupiga kelele ya kwamba wanaume wote tuingie chini tukasaidie kutoa maji kwa nguvu zote kupitia ndoo zilizokuwa huko kwasababu ile mashine iliilemewa.


Inaendelea......................
Tupe burudani mkuu, tupo tumeketi hapa na mfungo huu
 
Back
Top Bottom