Namna ya kujenga nyumba ya ndoto yako kwa budget ndogo sana

Frank mtanganyika

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2018
Posts
497
Reaction score
785
Hivi unajua kuwa hiyo kodi ya nyumba unayoilipa kila siku kama ungeweza kusave. hicho kiwango unaweza kukamilisha nyumba ya ndoto yako bila kuamini kilichotokea?.

wengi watakuambia ujenzi si Lele mama. ni kweli; kujenga nyumba ya mil 40 km unakipato cha kawaida si kazi ndogo

ila nataka nikuambie kitu kimoja ambacho watu wengi hawakijui ukitaka ukamilishe malengo yako yeyote yake. fikiria kwa ukubwa ila chukua hatua ndogo

ukiuliza timu yoyote duniani ambayo imeshawahi kushinda taji siri ya mafanikio . watakuambia we take one match at a time

Vilevile kwenye ujenzi ukitaka kufikia malengo ya kujenga nyumba ya ndoto acha kufikiria wapi utatoa zaidi ya 40M kujenga nyumba ya ndoto yako.
bali anza kufikiria
1. kununua kiwanja
2.kununua tofali moja
3.kujenga msingi wa nyumba
- kuna jamaa alinifwata na kuniuliza namna gani angeweza kujenga nyumba ya ndoto yake na kuepukana na pango ikiwa ana kipato kidogo?!.

tulikaa chini tukajadiliana, na kutengeneza plan ya anachotaka kukifanya si pesa tu bali msukumo unahitajika.

tunavyoongea sasa hv tumeshamaliza phase ya kwanza ya nyumba yake na toyar tumepanga tarehe ya kuanza phase ya pili
- na wewe pia unaweza kujenga haijalishi kipato ulichokuwa nacho. nitafute tushauriane na tufanye kazi yenye ubora na kwa gharama nafuu
0765931771 au 0783166050
Frank
Fundi mchundo kwa sasa nafanyia kazi zangu arusha na moshi ila mikoa mingine nafika pia
 
Umeanza vizuri ila……..!!
Ameanzaje vizuri mkuu. Mbona nimesoma aya ya kwanza tu nikachanganyikiwa. Kasema hivi

"Hivi unajua kuwa hiyo kodi ya nyumba unayoilipa kila siku kama ungeweza kusave. hicho kiwango unaweza kukamilisha nyumba ya ndoto yako bila kuamini kilichotokea?."

Sasa sijui wakati mtu anasave hiyo kodi ya nyumba badala ya kuilipia pango atakuwa analala wapi
 

Nachomaanisha kiwango kile kile unacholipia pango ukipanga kusave kinakufikisha mahali. the goal ni kusave kwa mbinu zozote tu sijasema usilipe kodi.

Ila kwa ukiwa na mindset ya kusave kwa ajili ya nyumba ya ndoto yako itakusaidia hata kutafuta nyumba ya bei nafuu na budget yako ya pango ukaigawa pamoja na ya malengo ya nyumba yako.

lengo nikuelewa consept inayozungumziwa
 
Ndio amesema umuone akupe mbwinu
 
Nyumba kama hii kama una kiwanja kikubwa ijenge pembeni ya eneo la kiwanja chako huku ukijpanga kujenga nyumba kubwa halafu ukishahamia kwenye kubwa hii inabaki nyumba ya pembeni kama quarter halafu ile kubwa iwe main house
 
Wachaka lengo lao ni hela ya chapu chapu, wewe mchaka wa wapi umjengee mtu nyumba kwa awamu kumi? Au ndiyo mtindo mpya wa kutupiga sisi kyasaka?
 
Wachaka lengo lao ni hela ya chapu chapu, wewe mchaka wa wapi umjengee mtu nyumba kwa awamu kumi? Au ndiyo mtindo mpya wa kutupiga sisi kyasaka?
wachaka ni wakina nani hao?!. chief kiswahili unakijua kwanza?.nenda ujifunze kiswahili vizur alafu uje uulize wapi hujaelewa
 
Concept
 
Na mimi ambaye nataka kujenga ghorofa ya chumba kimoja unanishauri nianze foundation na Elfu ngapi kiongozi?[emoji276]
chief ujenzi wowote unaanza na hatua za planning kujua gharama yeyote ya ujenzi ni vyema utafute ramani ya kile unachotaka kukifanya. ukishapata ramani. ni rahisi kuandaa boq ambayo itaainisha garama za ujenzi katika kila hatua na idadi ya material yanayohitajika
so tukishapa hivi ni rahisi kujua huo msingi wako unagarimu kiasi gani
 
Haka kanyumba katamu....haka mil10 sii nahamia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…