Namna ya Kukuza Mtoto anayependa kusoma

Namna ya Kukuza Mtoto anayependa kusoma

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Kama wazazi, tunapenda kuona watoto wetu wakijifunza mambo mapya. Si ajabu kumuona mama akimuuliza mtoto maswali huku akijua mtoto atatoa jibu la kufurahisha.

Zifuatazo ni baadhi ya mbinu ambazo zinaweza kukusaidia kukuza mtoto anayependa kusoma.

Panga kusoma na mtoto wako iwe ratiba ya kila siku. Endapo mtasoma pamoja, mtoto wako ataona kuwa kusoma kuna umuhimu na ataungojea muda huu kwa hamu hata kama umepanga kusoma kwa nusu saa tu.

Mnapotaka kusoma, shirikiana na mtoto wako kuchagua vitabu. Maamuzi kama haya ni muhimu kwa mtoto wako na yatamuongezea shauku ya kusoma na kujifunza.

Msomee mtoto kwa sauti huku ukimwonesha unapopasoma. Unaweza pia ukapokezana kusoma na mwanao. Hii itamsaidia kujifunza maneno mapya kirahisi na kuyakumbuka.

Muoneshe mtoto picha mkiwa mnasoma. Hii itamsaidia kuelewa maneno mapya na magumu. Mnaweza kuangalia picha kabla ya kusoma hadithi na kukisia inahusu nini. Hii huleta tofauti katika simulizi na huweza kuchochea ubunifu wa mtoto.

Filamu na simulizi za redioni ni namna nyingine za kuleta tofauti katika kusimulia hadithi. Watoto hutofautiana na sio kila mtoto anapenda kusoma sana kwa hiyo kuangalia/kusikiliza simulizi wanazopenda huenda kukawapa hamasa ya kusoma hadithi hizo.

#Malezi
 
Wangu huo muda sintompa wakusoma hapana wangu atafanya vitu vingine vya msingi samahani ila nimeshaona adhari nyingi za watoto walioachiwa wasome huku eti wazazi wakiamini watafika mbali.
1.connection with real people .
Anaposoma vitamu muda mwingi hana muda wakukua kiafya nakiakili why.
Muda mwingi hujitenga mwenyewe nakujisomea wakati wenzake wakicheza wakifanya practise ya vitu vya kitoto.
Mtoto atajiendekeza kuishi mwenyewe na hii itamuadhiri kiakili kuwa hii nisasa hii kwa hiyo akiwa na watu huwa shy na kutojiamini kwani hakai na watu ajifunze the real world .
Sijui mnanielewa.

Akiuziwa yeye huenda kujifungia na kukaa chumbani kwake halafu anaendelea kujisomea zaidi na zaidi hii hali hata ukubwani atakuwa hana muda na watu yeye ni vitabu early kabisa unaona nisawa anajifunza mambo ila mbeleni hizo ndio madhara yake.

2. Atakuwa haoni umuhimu wa kupata familia kabisa wala mwanaume au mwanamke.

Hili linatokea kuwa ashajiwekea ratiba yake yakukaa na kusoma vitabu tu atafanya kazi, biashara ila siku ya siku atarudi kwake nakuendelea kusoma vitabu fanyeni utafiti wawatu waliosoma vitabu waliolewa au walioa haraka au walichelewa .

Mimi na experience . Watoto wacheze tu wafurahie dunia .
Wapelekwe kwenye real things kupractise wajue maisha vitabu kwa 20's ai hapana.
Humfanya mtoto kuchelewa mambo mengi mbeleni mf. Familia .
Hayo ni mawazo yangu
 
pambaneni kuwa somea vitabu... huku wahindi wakipambana kuwa hesabisha pesa madukani... na kuwa unganisha na wafanyabiashara wengine wakihindi ndani na nje...
Wanahesabiana pesa huku wakipelekana shule.
 
pambaneni kuwa somea vitabu... huku wahindi wakipambana kuwa hesabisha pesa madukani... na kuwa unganisha na wafanyabiashara wengine wakihindi ndani na nje...

Hao jamaa nawakubali Sana,Hawa potezi muda full kuambukiza watoto kazi zao.
 
Hao jamaa nawakubali Sana,Hawa potezi muda full kuambukiza watoto kazi zao.
Kuna jambo kubwa tuna takiwa kufanya zaidi ya kuwa somea vitabu... au kama vipi tuwa peleke wakasome ushehe na upadri ili wasome sana vitabu... na watavisoma kila siku ktk maisha yao hata kwa kuvi kurejerea
 
Wangu huo muda sintompa wakusoma hapana wangu atafanya vitu vingine vya msingi samahani ila nimeshaona adhari nyingi za watoto walioachiwa wasome huku eti wazazi wakiamini watafika mbali.
1.connection with real people .
Anaposoma vitamu muda mwingi hana muda wakukua kiafya nakiakili why.
Muda mwingi hujitenga mwenyewe nakujisomea wakati wenzake wakicheza wakifanya practise ya vitu vya kitoto.
Mtoto atajiendekeza kuishi mwenyewe na hii itamuadhiri kiakili kuwa hii nisasa hii kwa hiyo akiwa na watu huwa shy na kutojiamini kwani hakai na watu ajifunze the real world .
Sijui mnanielewa.

Akiuziwa yeye huenda kujifungia na kukaa chumbani kwake halafu anaendelea kujisomea zaidi na zaidi hii hali hata ukubwani atakuwa hana muda na watu yeye ni vitabu early kabisa unaona nisawa anajifunza mambo ila mbeleni hizo ndio madhara yake.

2. Atakuwa haoni umuhimu wa kupata familia kabisa wala mwanaume au mwanamke.

Hili linatokea kuwa ashajiwekea ratiba yake yakukaa na kusoma vitabu tu atafanya kazi, biashara ila siku ya siku atarudi kwake nakuendelea kusoma vitabu fanyeni utafiti wawatu waliosoma vitabu waliolewa au walioa haraka au walichelewa .

Mimi na experience . Watoto wacheze tu wafurahie dunia .
Wapelekwe kwenye real things kupractise wajue maisha vitabu kwa 20's ai hapana.
Humfanya mtoto kuchelewa mambo mengi mbeleni mf. Familia .
Hayo ni mawazo yangu
kwani kupanga muda maana yake nini?Unategemea haya uliyoyaeleza hayawezi kufanyika sambamba na hayo aliyoyaeleza mtoa kwa kupanga muda wa kila jambo?
 
kwani kupanga muda maana yake nini?Unategemea haya uliyoyaeleza hayawezi kufanyika sambamba na hayo aliyoyaeleza mtoa kwa kupanga muda wa kila jambo?
Mimi kwangu na katazaga watu kusoma vitabu kwa sababu watajitenga na ulimwengu .
Sitaki wawe wapweke kisa vitabu .

Muda wakucheza wacheze .
There is to different things kuelezewa story ili ulale na kuendekeza usomaji wa vitabu always mtoto yupo na vitabu break yake kitabu , after lunch kitabu eti mtoto atajua mengi je na maisha ya uhasilia atayamuduje naalikuwa kwenyw vitabu .
 
Back
Top Bottom