Namna ya Kukuza Mtoto anayependa kusoma

Subscribed
Utanifaa Sana[emoji4][emoji120]
 
Umeandika point[emoji4][emoji106]
 
Mkuu una akili nyingi Sana. Much respect[emoji4][emoji120]
 
Sikuizi nakunywa Vladimir maana nashabikia Urusi. Kvant nimemwachia babu yangu Asprin maana zinapoteza kumbukumbu na huyu mzee hataki kukumbuka michepuko yake ya ujanani.
Aisee K Vant ni kifutio cha uhakika. Ukitaka kusahau shida zako, fanya mapenzi na K Vant kwa wingi
 
Napenda kusoma kuliko rafiki zangu wengi
Nadhani makuzi yalichangia
kabla sijaanza shule nilikuwa najua stori za vitabu vingi vya shule kaka na dada zangu walikuwa wanatusomea kwa sauti siyo kutusomea bali ni stori zilizokuwa zinawavutia pia na walikuwa wanatusomea Kama kushare na sisi

kwa kuwa tulikuwa hatujui kusoma hatujaanza shule lakini nadhani ilitujenga kiasi chake
Stori kama kambi ya kaboya, bida na kacha, safari ya masasi,siku ya gulio Katerero,Kibanga ampiga mkoloni na nyingine nyingi sikuvikuta hivi vitabu wakati nasoma havikuwepo lakini ni kama nilivisoma kabla sijaanza shule
Nilikuwa mpaka naweza kuwahadithia wenzangu na nilikuwa naomba nisomewe mara nyingi zile stori ambazo nimezipenda nisomewe tena
Nilianza la kwanza nikiwa na miaka 8

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Pole saivi tuletee faida ya hivyo vitabu sio kwa ugomvi lakini
 
Pole saivi tuletee faida ya hivyo vitabu sio kwa ugomvi lakini
Tatizo lenu wabongo Mmekalili kufanikiwa ni kuwa na pesa tu au kupata kazi. kuna maarifa mengi kwenye vitabu kama vile jinsi ya kuishi na watu, mahusiano, saikologia, elimu ya fedha, kujitambua nk. Kuna elimu ya darasani, mtaani na ya ulimwenguni, kuna maarifa huwezi kuyapata shuleni wala mtaani utayapata ulimwenguni, na ya ulimwenguni utayapata kwa kutumia vitabu vya watu tofauti tofauti ulimwenguni. Kuna watu wangapi wanapata fedha na kufirisika au kisa hawana elimu ya fedha, kuna watu wangapi maisha yao yamekuwa machungu kisa mahusiano mabovu. Mimi vitabu vimenisaidia sana nilimaliza degree sanaa lakini nikajisoemea vitabu na kupata idea kufanya biashara IT na nimefanikiwa sana tu.
Kupitia vitabu nimejifunza
Jinsi ya kuweza kuhimili stress za biashara, kutafuta wateja, kujiamini, kuweza ku control wafanyakazi wangu, kumanage pesa, kukuza mtaji, kuweza kuwa Hamble na mwelevu, kuishi na watu tofauti na pia kuweza kulea familia yangu.
Kusoma kutakupa maarifa ya kuweza kuhimili misukosuko mbalimbali ya maisha mf kuna wakati biashara zangu zilikuwa mbaya sana hadi nikahisi kukata tamaa ili nilisoma biography ya Elon Musk na nikagundua aliyopitia hiyo ilinipa nguvu ya kusonga mbele, Kuna kipindi mahusiano yangu yalikuwa mabaya sana ila nilisoma kitabu kimoja na nikifanya yale niliyosoma humo huwezi amini imenisaidia sana kuweza kuweka mahusiano yangu imara.
Kusoma sio kuwa na degree ni kujifunza mambo ya msingi kwenye maisha yetu. Matajiri na watu wengi waliofanikiwa huwa wanajifunza kila siku kwa vitendo na vitabu hii haijalisha wameishai darasa la 7 au chuo kikuu
 
Ukishamaliza sehemu yako, anza sasa kutafuta talanta ya mtoto ukimtafutia mentor wa kukuza talanta yake/lkn kama pia una uwezo huo ni vizuri. Dunia ilipofikia si elimu tu hata mtoto kuwa na elimu+skills inasaidia kumuingiza mtoto katika ushindani.

Mtoto akue huku akiwa anajua elimu ya fedha kidogo. Kujua matumizi ya kila siku,akiba,sadaka na zaka. Hapo sasa tunaangalia miaka 7 kuendelea mbele polepole anaanza ku_adapt mfumo.

Sahivi tunaeleweshana na vijana kuhusu wao walichoelewa na kile walichokielewa na wanachopaswa kuwasilisha kile wanachokijua.
 
Kwa kusoma vitabu kumenisaidia si kila kitu naweza kuchangia hata kama nakijua. Think & Grow Rich ni kitabu kilichonijenga sana kwenye kujiajiri na mpaka leo kinanipa nguvu sana yakuendelea kusimamia ninachokiamini. Unaposoma kitabu ni sawa na kufanya convo na author kwa ndani ya maono yake.
 
Mtoto kucheza ni muhimu kama sehemu ya kujifunza stadi za kijamii, lakini mtoto kusoma vitabu vya ziada nje ya vile anavyosoma shuleni ni muhimu ili aweze kuuelewa ulimwengu.
Utashangaa wenzetu wanavumbua vitu vingi tu ila sisi hata kutengeneza sindano hatuwezi kwa nini?
Kwa sababu hatujifunzi nje ya tunachofundiswa darasani na nje ya tunachojifunza kwenye mazingira tunayoishi. mf kama mimi nimezaliwa na kukulia Dar sitaweza kujua fursa za biashara ya misitu Iringa nitajua either kwa kwenda huko au kwa kusoma, wenzetu ngozi nyeupe huwa wanapenda kusafiri na kusoma kwa ajili ya kujifunza ndio maana waliweza kufika Africa na wakaweza kututawala.
Mtoto kusoma haimaanishi awe anasoma vitu vya shuleni ni kumfundisha kusoma vitu vinavyohusu maisha kwa mfumo wa hadithi kuendana na umri wake, atajijengea utamaduni wa kujifunz maarifa mengine nje ya darasani na kuwa mtafiti.
Hiyo ya kuchelewa kimaisha na kuanzisha familia sijaielewa....kusoma na kuchelewa kimaisha mmh!!
hakunaga kuchelewa wala kuwahi kimaisha kuna waliowahi kuoa/kuolewa ndoa zimavunjika au wenzi wao wamefariki, walowahi kuzaa watoto wamewashinda, waliowahi kupata kazi nzuri wakafukuzwa , waliotajirika wakafirisika, waliowahi kuwa na familia na familia imesambaratika. Hakunaga kuwahi wala kuchelewa kila kitu huja kwa wakati.

Labda hapa kama unamaanisha kusoma ile elimu ya darasani na kusahau mambo mengine ya maisha maana kuwa watu hujifunza elimu ya darasani na kujaza vyeti bila kujifunza maarifa mengine ya maisha.
Kwenye vitabu utajifunza maarifa ya mahusiano, pesa, saikologia, kujiamini, kujitambua, afya na hata kila kitu kinachokuzunguka. Kukosa maarifa hayo kunaweza kukupelekea usiwe na uwezo wa kuhimili stress na matatizo ya akili hivyo kugombana na watu au kachanhanyikiwa, utaweza kudanganyika kirahisi na kutapeliwa kirahisi, usijue tabia za watu na kuwa na mahusiano mabovu, usijue jinsi ya kutumia pesa na kuwa mtumwa wa madeni, usijuie jinsi ya kulinda afya yako ya mwili na akili nk.
Ni machache ila kama ukiamua kumlea mwanao hivyo huo ni uamuzi wako, japo ni muhimu kueleawa vizuri faida na harasa za maamuzi yako.
 
This is so warped! Tena dada nahisi unachanganya na effects za matumizi yaliyokithiri ya digital devices. Mimi nasoma vitabu sana, baba yangu aliniambukiza nafikiri. Ukiacha kwamba ni starehe yangu, kusoma hakujanifanya niwe mtu wa kujitenga, kwa taarifa yako sababu ya kupenda kusoma sana masomo ya historia, uraia na general studies sikuwahi kukaa chini kusoma sababu tayari nilishasoma hivyo vitu kama sehemu ya starehe yangu.

Hata mbele za watu sikosi cha kuchangia, yaani mimi sio mtu wa "mhh.." kuguna guna tu na kukubaliana au kukataa hoja bila sababu za msingi. Kusoma kumenifanya niwe mtu anayependa kusafiri kwa sababu ndani yangu huwa natamani kujua wengine wanaishije. Sasa hiyo ni kwa vitabu vya leisure tu .. bado vile vya self development, aisee nimekuwa mtu bora zaidi ukiongezea na miongozo ya wazazi na dini. Nimejifunza discipline, focus na kusamehe kupitia vitabu. Ukipata wasaa soma kitabu cha 7 Habits of Highly Effective People, you just might be a little bit better as a human

Mwishowe uelewa wangu mpana wa vitu na kupenda kwangu kusoma kumenifikisha nilipofika hapa kwa maana ya career yangu. I am first and foremost a proud bookworm, an interpreter, translator and editor and I love my life and those that I love, love me back!
 
Mwanangu bado mdogo lakini tunapenda kukaa pamoja na kusoma then baadae anaendelea na michezo yake. Thanks for this
 
Ungedokezea na umri wa kuwasomea kwenye mada yako ingependeza zaidi. Mimi nilishauriwa kuanza kuwasomea watoto vitabu wakiwa na miezi sita.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…