Nampa maua yake DTO wa Korogwe ila Kampuni ya BM ijitafakari kuhusu huduma zao

Nampa maua yake DTO wa Korogwe ila Kampuni ya BM ijitafakari kuhusu huduma zao

Kayugumis

Senior Member
Joined
Jun 6, 2022
Posts
107
Reaction score
97
Basi.jpg

Basi tulilolitumia ambalo lilikwama njiani tukasaidiwa na RTO (Regional Traffic Officers)
Nikiwa mmoja wa Wasafiri katika Basi la BM, tukitoka Dar kuelekea Arusha, ambapo liliondoka Dara majira ya Saa Nane Mchana jana Mei 19, 2024, tulikutana na changamoto ya kiufundi njiani.

Picha linaanza kwanza basi lilichelewa kuondoka, badala ya Saa Nane Kamili, tuliondoka Nane na Nusu Mchana.

Pili namba ya gari iliyoandikwa kwenye tiketi tulizokata ni tofauti na basi tulilolikuta kituoni na kutakiwa kusafiri nao.

Majira ya Saa Mbili Kasoro Usiku, gari ikazimika tukiwa Korogwe mkoani Tanga

Baada ya kukaa pale kwa takribani saa mbili yaani dakika 180 bila kupata muafaka, wawakilishi wa Kampuni ya BM wakawasiliana na bosi wao ambaye aligoma kulet basi lingine, badala yake akataka atafute Coaster mbili ndio zije zitubebe.

Baada ya muda dereva naye akapotea katika mzingira tata, ilipofika 3 hours tangu tulipokwamba, ikabidi tuwasiliane na DTO wa Korogwe, Mshangama Nyangasa ambaye tunashukuru aliagiza vijana wake Askari mafundi waje kutoa msaada.

Ndani ya dakika 15 tu basi likawaka na tukatakiwa kuendelea na safari, wakati wale staff wa BM walipambana kwa saa tatu bila mafanikio huku bosi wao akileta porojo nyingi.

Nitumie nafasi hii kupitia JamiiForums kumpongeza DTO wa Korogwe na Askari wake kwa kutupa msaada, lakini niwaambie tu BM wajitafakari kwa kilichotokea.
WhatsApp Image 2024-05-19 at 22.13.24_f2609dec.jpg
 
View attachment 2994821
Basi tulilolitumia ambalo lilikwama njiani tukasaidiwa na RTO (Regional Traffic Officers)
Nikiwa mmoja wa Wasafiri katika Basi la BM, tukitoka Dar kuelekea Arusha, ambapo liliondoka Dara majira ya Saa Nane Mchana jana Mei 19, 2024, tulikutana na changamoto ya kiufundi njiani.

Picha linaanza kwanza basi lilichelewa kuondoka, badala ya Saa Nane Kamili, tuliondoka Nane na Nusu Mchana.

Pili namba ya gari iliyoandikwa kwenye tiketi tulizokata ni tofauti na basi tulilolikuta kituoni na kutakiwa kusafiri nao.

Majira ya Saa Mbili Kasoro Usiku, gari ikazimika tukiwa Korogwe mkoani Tanga

Baada ya kukaa pale kwa takribani saa mbili yaani dakika 180 bila kupata muafaka, wawakilishi wa Kampuni ya BM wakawasiliana na bosi wao ambaye aligoma kulet basi lingine, badala yake akataka atafute Coaster mbili ndio zije zitubebe.

Baada ya muda dereva naye akapotea katika mzingira tata, ilipofika 3 hours tangu tulipokwamba, ikabidi tuwasiliane na RTO wa Korogwe, ambaye tunashukuru aliagiza vijana wake Askari mafundi waje kutoa msaada.

Ndani ya dakika 15 tu basi likawaka na tukatakiwa kuendelea na safari, wakati wale staff wa BM walipambana kwa saa tatu bila mafanikio huku bosi wao akileta porojo nyingi.

Nitumie nafasi hii kupitia JamiiForums kumpongeza RTO wa Korogwe na Askari wake kwa kutupa msaada, lakini niwaambie tu BM wajitafakari kwa kilichotokea.
RTO Korogwe×××
DTO Korogwe✓✓✓ au..
RTO Tanga ✓✓✓
 
Hii biashara ya usafirishaji abiria nadhani ina shida.

Kampuni zote zinaanzaga vizuri sana,halafu sijui kinatokea nini zinaanza sarakasi.
 
Back
Top Bottom