Namsaidiaje mdogo wangu huyu angalau awe msafi?

Namsaidiaje mdogo wangu huyu angalau awe msafi?

Hello members!!!

Ni mdogo wangu wa mwisho wa kiume miaka 17+ Nashindwa kuelewa ni malezi au nini. Ila mbona sie wengine ndugu zake hatuko hivyo.
Naanza kuhofia asije kuona namnyanyasa.
Yaani unaweza kurudi home unakuta kakaa na mavyombo machafu hana habari. Vitu viko hovyo, kupangilia kila kitu kiwe pahala pake, mfano amekula mavyombo kaacha hapo. Kupika anajua ila usafi wa pale anakopikia ni hadi umkumbushe wee naniii embu safisha safisha kidogo hapo sehemu ya kupikia. Hapo nje anaingia na kutoka ndani, unarudi unakuta mamchanga yamejaa, kabla sijaingia ndani nafanya kuyafagia kidogo mazingira ya nje. Unaweza kuta kitanda hakijatandikwa na yupo tu kashinda nyumbani sijui ni uvivu au ndio uchafu wenyewe. Siku narudi naingia chumbani nakuta kitanda kiko vururuvururu alivyoamka ndivyo hvyo hivyo,(kidogo nimzabe makofi) hapa alijirekebisha. Mbaya zaidi kila siku namsema. Sio kwamba me ni msafi saaana ila kiukweli me angalau.

Kuhusu usafi wake binafsi hana shida sana.

Nashindwa kuelewa kimalezi mzee alifariki akiwa bado mdogo kama 2-3yrs hivi. Alilelewa zaidi na mama pekee. Nawaza labda malezi ya mzazi mmoja ndio sababu.

Sasa naanza kuona huyu dogo labda anaona tu broo wake nina nongwa.😄
Mnunulie toys achezee kwani kuna kila dalili kuwa huyo hajakuwa kiakili, yaani akili yake bado iko kwenye status ya loading.....
 
Aisee acha kumsimanga huyo dogo, Mimi Nimekuwa kwenye Mikono ya Wazazi wote wawili mpaka sasa Nipo kwangu ila still kuna wakati demu anaweza kuja geto akapakuta pachavu kinoma, Yani inafika time narudi safari naona geto pachafu sirudi nachukua lodge nalala pasafi.

Imebidi sasa nitafute mdada wa kazi walau aje twice per week kupiga usafi heavy
Imefika time nikihama kwanza sitaki makorokocho ndani kabisa kutoka na najua hali yangu huwa napanga nyumba nzima naweka vitu essential tu Kabati, Fridge, Kitenga cha nguo chafu mziki, TV na Sofa moja pamoja na Godoro nene nalala chini tu vinakuwa spaced kiasi kwamba sitaki ujinga wa vyombo wala manguo mengi na viatu
 
Aisee acha kumsimanga huyo dogo, Mimi Nimekuwa kwenye Mikono ya Wazazi wote wawili mpaka sasa Nipo kwangu ila still kuna wakati demu anaweza kuja geto akapakuta pachavu kinoma, Yani inafika time narudi safari naona geto pachafu sirudi nachukua lodge nalala pasafi. Imebidi sasa nitafute mdada wa kazi walau aje twice per week kupiga usafi heavy
Imefika time nikihama kwanza sitaki makorokocho ndani kabisa kutoka na najua hali yangu huwa napanga nyumba nzima naweka vitu essential tu Kabati, Fridge, Kitenga cha nguo chafu mziki, TV na Sofa moja pamoja na Godoro nene nalala chini tu vinakuwa spaced kiasi kwamba sitaki ujinga wa vyombo wala manguo mengi na viatu
Hongera kwa kupanga nyumba nzima.
 
Yupo mi ninakaa nae anapolala kufanya usaf labda umwambie mpaka huwa nakaa kmya tu
 
Hello members!!!

Ni mdogo wangu wa mwisho wa kiume miaka 17+ Nashindwa kuelewa ni malezi au nini. Ila mbona sie wengine ndugu zake hatuko hivyo.
Naanza kuhofia asije kuona namnyanyasa.
Yaani unaweza kurudi home unakuta kakaa na mavyombo machafu hana habari. Vitu viko hovyo, kupangilia kila kitu kiwe pahala pake, mfano amekula mavyombo kaacha hapo. Kupika anajua ila usafi wa pale anakopikia ni hadi umkumbushe wee naniii embu safisha safisha kidogo hapo sehemu ya kupikia. Hapo nje anaingia na kutoka ndani, unarudi unakuta mamchanga yamejaa, kabla sijaingia ndani nafanya kuyafagia kidogo mazingira ya nje. Unaweza kuta kitanda hakijatandikwa na yupo tu kashinda nyumbani sijui ni uvivu au ndio uchafu wenyewe. Siku narudi naingia chumbani nakuta kitanda kiko vururuvururu alivyoamka ndivyo hvyo hivyo,(kidogo nimzabe makofi) hapa alijirekebisha. Mbaya zaidi kila siku namsema. Sio kwamba me ni msafi saaana ila kiukweli me angalau.

Kuhusu usafi wake binafsi hana shida sana.

Nashindwa kuelewa kimalezi mzee alifariki akiwa bado mdogo kama 2-3yrs hivi. Alilelewa zaidi na mama pekee. Nawaza labda malezi ya mzazi mmoja ndio sababu.

Sasa naanza kuona huyu dogo labda anaona tu broo wake nina nongwa.😄
Tatizo hamkumpeleka shule . Mpeleke memkwa atabadilika
 
Ni madeko tu hayo hana ile munkari ya kujishughulisha
 
Nenda nae taratibu Kuna muda ukifika atakaa sawa tu...
 
Mtoto wa Miaka 17 sio wa kufundishwa usafi huyo ni kijana wa form four

Mnase makofi akili itakaa sawa asijione special.
 
Role model atoke wapi [emoji1787][emoji1787] ye mwenyewe kama mtu alikuwa anajiita trouble maker mtu wa mavurugu

Kuna comment alishawahi andika alimtega mtu na mguu aanguke bar makusudi
mkuu bado unskumbuka tu ule mkasa.😂😂😂
 
Imagine mwanaume unajua hadi kupika chapati...kuna kuoa kweli hapo?
🤣🤣🤣 Ila me vitu vya ngano siwezi bana kupika kulwa we mwenyewe wajua.
 
Back
Top Bottom