Namshauri Jaji Mkuu ajiuzulu

Namshauri Jaji Mkuu ajiuzulu

Kinachofanyika mahakamani kwa miezi mitatu mfululizo Ni ishara kwa muhimili wa mahakama kushindwa kutekeleza wajibu wake na kutekeleza maelekezo ya serikali.

Kwa kuwa mkuu wa muhimili wa mahakama Ni yule yule aliyekuwepo wakati watu wanaonewa na kubambikiwa kesi na kwa kipindi chote hicho alikaa kimya, naomba busara imwelekeze Jaji Mkuu kuachia ngazi na kuruhusu usukaji upya wa muhimili wa mahakama unaoweza kusimamia haki.

Muhimili huu ukiendelea kusikiliza serikali inataka nini na kutekeleza dhana ya separation of power haitakuwa na maana nchini.

Mzee nikuombe utafakari Kama uliyowafanyia wananchi wa Tanzania kwa miaka mitano yanakushuhudia kuendelea kukalia hicho kiti. Najua ulisukumwa kuminya haki na ukatekeleza kinyume na kiapo chako. Kukaa pembeni si dalili ya kushindwa Bali nikuiombea mahakama msamaha kwa wannchi na kupunguza lawama na dhambi ulizochuma ukiwa hapo juu.

Watanzania wanalia na kuumia kwa kupoteza wapendwa wao wakiwa jela au wengine kufariki kwa presha kwa kusikia wapendwa wao wapo ndani. Wengine Ni walemavu na baadhi familia zimesambaratika, jitafakari
Mnapenda kuangushia jumba bovu kwa wenzenu..mbona wew hutukukuona hata sku1 ukiandamana kwenda ikulu kudai hO haki...au kukuona hata ukitoa maoni kwenye video ya kulaan uonevu huo?kwan we si ni raia wa Tz...?
 
Kiukweli wengi walihusika sijui kwa nini. Kama kujiuzulu ni wengi. Hata wale waliogizwa wawatupe nje na kisha wakutane na mkono mwingine. Hata wale waliotishiwa kushikishwa adabu mashangazi. Hata wale waliotoeroka ofisi au kukatalia fomu za wagombea. Ni wengi ni wengi mno kusema jaji mkuu ni kumtwika mzigo peke yake. Yaani yanotokea utafikkiri yamepangwa kumbe sio ila tu tumeingia ndani na kuyaona live.
Ni vizueri walioshiriki dhuluma wakaungama hadfharani. Mbowe aliitisha maridhiano hapo unaona umuhimu wake
 
Mafanikio ya Samia ni habari mbaya sana kwa Lisu maana 2025 hana chake tena.

Ccm itaendelea kupeta
 
Naunga mkono hoja hii, alinde heshima
 
Mafanikio ya Samia ni habari mbaya sana kwa Lisu maana 2025 hana chake tena.

Ccm itaendelea kupeta
Umebaki kukariri tuu huna point yeyote kila thread una copy na paste haya maneno tuu,safar hii lazima upewe mimba na vijana wa bavicha
 
jaji mkuu mnafiki kabisa kila shuhuli ya mzee pombe yupo utadhani hana majukumu.

Kuna siku Mzee Pombe alimuahidi atampa fungu la kuboresha majengo ya mahakama na mkumsisitiza ahakikishe eti kesi zote zinazohusu jamhuhuri lazima jamhuhuri ishinde.
 
Naunga mkono hoja. Pia Ndugu gay na IGP Sirro nao wajiuzulu. It's shame!
 
Mnapenda kuangushia jumba bovu kwa wenzenu..mbona wew hutukukuona hata sku1 ukiandamana kwenda ikulu kudai hO haki...au kukuona hata ukitoa maoni kwenye video ya kulaan uonevu huo?kwan we si ni raia wa Tz...?
Maadili ya Mahakama yaliwekwa kando na kutekeleza maagizo ya Mtu.
 
Naunga mkono. Jaji Mkuu hawezi kutenganishwa na ubinyaji haki uliofanyika 2015-21. Ni sehemu ya ufedhuli huo. The same can be said about AG, Jaji Kaijage, Jaji Mutungi, Mahera, Ndugu-gay, IGP, na DPP aliyepandishwa cheo na kuwa Jaji. Lakini kama DPP alipandishwa cheo, unafikiri Jaji Mkuu ana sababu ya kujali?
Naunga mkono hoja, jaji mkuu na mkuu wa jeshi la polisi ziro lazima wawajibike na jinsi vyombo vyao vilivyokuwa vinafuata amri kutoka kwa meko.
 
Kinachonisikitisha ni kuwa Nchi yetu inaongozwa kwa utashi wa mtu alie madarakani!Kama tulikosea tukampa kichaa nchi mjue ni pale tu Mungu atakapomchukua ndio nchi itapona!!TZ HAKUNA UHURU WA KIMAMLAKA KUDHIBITI MAMLAKA NYINGINE!!!!KATIBA MPYA NDIO SULUHISHO PEKEE!!
 
Mungu anatupenda sana, katolewa mmoja ili Taifa lipate uhuru....
 
dah, nina mashaka sana uachiaji huu holela (horera?) wa hawa wahuni.........mama awe makini sana. hakuna watu wasiokuwa na shukrani km hawa. halafu kwani ni lazima ku.......?!! dah, ngoja ninyamaze kwanza ila kulaumika ni sehemu ya oungozi pia hivyo lisiogopwe hilo!
 
Back
Top Bottom