Namungo FC yazuiwa Uwanja wa Ndege Angola

Namungo FC yazuiwa Uwanja wa Ndege Angola

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Namungo FC imezuiliwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Luanda nchini Angola baada ya mamlaka kudai wachezaji watatu na kiongozi mmoja wana virusi vya Corona.

Mpaka wakati wa kuandika taarifa hii timu ipo uwanja wa ndege huku utata ukitawala kutokana na mamlaka za nchi hiyo kutaka msafara mzima ama urudi Tanzania au uende karantini.

Namungo ipo Angola kuchuana na Clube Desportivo 1º de Agosto katika mechi ya kombe la shirikisho.

Taarifa zaidi zitafuata.

===========

NAMUNGO YAZUILIWA UWANJA WA NDEGE

Kikosi cha wachezaji wa Namungo fc wamezuiliwa uwanja wa ndege wa Luanda nchini Angola baada ya maafisa nchini humo kudai kuwa wachezaji watatu na kiongozi mmoja wana virus vya Corona.

Maafisa hao wamesema kuwa Namungo watatakiwa kufanya moja kati ya kurudi Tanzania au waende Quarantine.

Klabu hiyo yenye maskani yake huko Lindi iliondoka kuelekea Angola kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Primeiro De Agosto mchezo ambao utachezwa tarehe 14 Februari.

Namungo chini ya kocha wake Hemed Morocco inashika nafasi ya 13 katika msimamo wa ligi kuu soka Tanzania bara ikiwa na alama 21 na kucheza michezo 16.

De Agosto iliingia kwenye kombe la shirikisho baada ya kushuka kutoka michuano ya klabu bingwa barani Afrika, baada ya kufungwa na Kaiser chiefs ya Afrika kusini.

Ni moja kati ya michezo miwili ya hatua ya mtoano ambapo mshindi wa matokeo ya ujumla kwamaana ya Nyumbani na Ugenini atafuzu hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
 
Msafara mzima wa Klabu ya Namungo FC umezuiliwa uwanja wa Ndege wa Luanda nchini Angola baada ya mamlaka kudai wachezaji watatu na kiongozi mmoja wana virusi vya Corona.

Taarifa zaidi zinasema kuwa mpaka sasa timu ipo uwanja wa Ndege huku utata ukitawala kutokana na mamlaka za nchi hizo kutaka msafara mzima urudi Tanzania ama uwekwe Kalantini kwa siku tatu, wao wamegoma.

Kumbuka mtanange huu wa michuano ya kombe la shirikisho unapigwa kesho dhidi ya Clube Desporvtivo do 1°Agosto.

.



NAMUNGO YAZUILIWA UWANJA WA NDEGE

Kikosi cha wachezaji wa Namungo fc wamezuiliwa uwanja wa ndege wa Luanda nchini Angola baada ya maafisa nchini humo kudai kuwa wachezaji watatu na kiongozi mmoja wana virus vya Corona.

Maafisa hao wamesema kuwa Namungo watatakiwa kufanya moja kati ya kurudi Tanzania au waende Quarantine.

Klabu hiyo yenye maskani yake huko Lindi iliondoka kuelekea Angola kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Primeiro De Agosto mchezo ambao utachezwa tarehe 14 Februari.

Namungo chini ya kocha wake Hemed Morocco inashika nafasi ya 13 katika msimamo wa ligi kuu soka Tanzania bara ikiwa na alama 21 na kucheza michezo 16.

De Agosto iliingia kwenye kombe la shirikisho baada ya kushuka kutoka michuano ya klabu bingwa barani Afrika, baada ya kufungwa na Kaiser chiefs ya Afrika kusini.

Ni moja kati ya michezo miwili ya hatua ya mtoano ambapo mshindi wa matokeo ya ujumla kwamaana ya Nyumbani na Ugenini atafuzu hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
 
Kwan hawakupiga nyungu kabla hawajaondoka!!?😂
Tatizo na mashaka na vipimo vyetu kama wanapima au wanachukuwa pesa tu na ku save chem za kupimia wakiandika negative tu. ndio maana hata Dubai Tanzania wako katika list hata kama umeonesha umepima ukifika ni lazima upime tena ni kama vile hatuamini.
 
Back
Top Bottom