Namuokoaje rafiki yangu ambaye ni Mwalimu Kijijini, michezo ya wabaya usiku inamnyima raha

Kuna jamaa anayo dawa ya watu Kama hao jichangeni mkachukue kile kimbao huko kwa kina konde boy
 
Ngoja nikamuite jamaa flani ana kibao icho hataari
 
Mkuu Upo seriously au unatangaza biashara?
 
Simshauri kuhonga, juzi kuna ticha katiwa ndani Tabora alimhonga 90000 katibu tawala ili ahamie Tabora mjini kutoka kijijini
Unamhongaje Katibu tawala?wanahongwa wa chini yake njaà Kali ili wakamshawoshi Katibu tawala
 
Huo ni mpango wa kijiji kizima

Hawataki ELIMU na maendeleo

Suluhisho ni kuhama tu hakuna lingine, hauwezi kushindana na mchawi

Mchawi anarithisha uchawi wake hadi kwa kizazi chake cha tatu mbele

Atafute mtu wa kubadilishana nae/ atumie mate mate bomani kwa wakuu wake.
 
Imekuwa bahati mbaya sana kwa sasa siko Bongo lakini imani na simulizi kama hizi huwa zinanivutia sana. Zinanivutia kwa sababu huwa napenda kuhakikisha mwenyewe hizo nguvu za uchawi live. Ningekuwa karibu sasa hivi ningeomba tuwasiliane ili uniungashe na hao waathirika ili nipate kwenda (kwa gharama zangu) mpaka wanapoishi niwaombe waniachie hiyo nyumba kwa muda hata wa mwezi nilale ndani ili nijionee mwenyewe. Au hata kama watakubali niishi nao sina tatizo ila nia yangu ni kuona tu kama hizi imani zina ukweli wowote. Hata kama nitawapa kifuta machozi niko tayari. Siku nikirudi kama bado tatizo lipo naomba sana mnipe hiyo chance.
 
Msha Jr on the beat [emoji443][emoji444][emoji443]
 
Mpeleke kwa psychiatrist yeye ndo ana matatizo, Sio masihara ni science iyo.
 
Kuna sehemu hazipendi kbs elimu.
 
Aisee we kweli 'MACHO MDILIKO'

Sent from my SM-N910W8 using JamiiForums mobile app
 
Mungu ndio kilakitu, anunue biblia Kama Ni muislam awe na msaafu awe anasali usiku, hakuna mchawi anayefurukuta mbele ya mungu,,,
 
Je, amejaribu kusali kwa kumaanisha? tatizo sio kubwa sana mbele ya Mungu endapo akilipeleka mbele za Mungu kwa maombi.....
Kabisa,ajitahidi kusali,ikibidi afunge maombi ya siku mbili kavu bila kula Wala kunywa chochote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…