Nani adui wa vijana katika Kujiajiri. Ni Uthubutu, Serikali, au Malezi na Mazingira?

MTAJI

Mengine ngonjera tu.
Mtaji wako ni uthubutu wako unaeza anza na kidogo ulichonacho sema sisi huwa tunataka hadi tufikishe kiwango fulani ndipo tuanze rasmi kujiajiri jambo ambalo ni mtihani kulitekeleza,. Sema kikwazo pia ni mazingira si rafiki kwa biashara rasmi tozo zinazidi uhalisia, pia mfumo wa elimu haumjengi mtu kujiajiri bali kuwa mtumishi jambo linalopekea mhitimu kuona aibu na kuwa selective kuchagua kazi badala ya kujiajiri.
 
Huna tofauti na Mimi aisee nilipo maliza chuo nili wambia nyumbani sihitaji kuajiriwa hawa kuni elewa kabisa ila nili wambia msimamo wangu ndo huo na utabaki kuwa hivyo nashukuru Mungu toka nimalize chuo mpaka sasa sijawahi omba ajira na sijawahi ajiriwa maisha yana kwenda Mungu ni mwema sana sana kwangu nafanya biashara zangu ndogo ndogo Mungu ni mkubwa tatizo co mtaji tatizo kubwa ni uoga na uthubutu
 
Tatizo ni uthubutu tu!. Watu wanashindwa kuchukua hatua katika maamuzi mengine kama biashara, kilimo nk. Wanachotaka ni ajira tu. Pooole kijana mwenzangu.
 
Mimi siku zote naamini kwenye FAIDA kuliko MSHAHARA
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Umeandika Points.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ni mtu mzima. Nilikuwa kijana miaka ya mwanzoni mwa 2000. Nimejaribu kujiajiri, kuajiri na kuajiriwa. Naweza kusema kuna matatizo katika kila nyanja...kuanzia malezi, mazingira (sera) na mitaji.

1. Kwanza unapoongelea vijana inabidi uwagawe katika makundi matatu...kundi la kwanza ninwale wanaoishi elimu ya msingi au hawamalizi kabisa elimu ya msingi. Kundi la pili ninwale wanaomaliza elimu ya kati (form 4 au 6). Kundi la pili ninwale wanaohitimu vyuo (diploma/ degree). Haya makundi yana mahitaji tofauti na yana takiwa yawe treated tofauti. Kuwaweka vijana wote katika kapu moja ndo mwanzo wa kushindwa kutatua changamoto.za ajira.


Kundi la kwanza ni vijana ambao wanarudi kufanya shughuli za kiuchumi.zinazopatikana katika maeneo yao. Kwa mfano kama kuna machimbo wataenda kuchimba, kama kuna ziwa au bahari wataenda kuvua samaki na kama kuna mifugo wataanza kufuga....na kilimo.

Kwenye biashara hawa mara nyingi wanakuwa wachuuzi. Wachukue bidhaa sehemu A wauze sehemu B.

Kinacho wakwamisha vijana kwenye kundi hili ni ukosefu wa elimu za kazi wanazofanya. Wanavua samaki bila kiwa ana elimu ya uvuvi, wanalima bila kuwa na elimu ya kilimo n.k. Hivyo hujikuta hawana tija.

Kinachotakiwa hapa ni elimu juu ya kazi wanazozifanya. Bahati mbaya hakuna vyuo ambavyo vipo kwa ajili yao..ukiacha vyuo vya vyeta ambavyo vimejikita kwenye skills fulani fulani kama ujenzi, uashi, ufundi umeme n.k.

Tunahitaji kuwa na vyuo vya kila fani kutokana na shughuli za kiuchumi katika maeneo husika. Kwa mfano kama tungekuwa na vyuo vya uvivi kanda ya ziwa...acha kile cha nyegezi ambacho kinachukua watu wachache...ili kila mtu anaye vua awe na elimu ya uvuvi, kila anaye lima nyanya awe na elimu ya kuzalisha nyanya, kila.anaye lima mahindi awe na elimu ya kuzalisha mahindi Ili watu wasifanye kazi kwa mazoea ambazo hazina tija.

2. Vijana wa elimu ya kati...hawa mara nyingi wanatakiwa kuwa kama wa kundi la kwanza au kuwa ma supervisor. Hawa nao wanahitaji elimu kama kundi la kwanza ili wawasimamie au waajiri kundi la kwanza.

3. Vijana wa elimu ya juu hawa tatizo lao kubwa ni mfumo wa elimu. Wanamaliza wakiwa na vyeti lakini hawajui kazi walizosomea. Unakuta mtu ana vyeti say vya degree ya business administration halafu unamuuliza anaweza kufanya nini...hakuna. Hawa mara nyingi wanaandaliwa kuajiriwa na kupata additional on job training ndo wanaweza kufanya kitu.

Kwa hiyo kujaribu kutaka kundi hili wajiajiri kwa fani zao mara baada ya kuhitimu ni kitu ambacho hakiwezekani. Maana wanahitaji additional training ili kuwafanya wawe na fani. Elimu ya vyuo ni kama ya ku wa expose tu kwenye mambo mengi bila kuwajengea specific proffession. Hawawezi kujiajiri kamwe.

Therefore
1. Serikali na wadau wanahitaji kujenga kuwa na njia za kuwapa ujuzi watu wa kundi la kwanza na la pili.

2. Serikali inahitaji kuwapa incentive wataalamu ili waanzishe biashara ambazo zitaajiri watu wa kundi la tatu. Ni rahisi kwa mtu aliyekuwa kwenye ajira kwa miaka 10 kuanzisha biashara ambayo itaajiri vijana 20 kuliko kuwapa hela kikundi cha vijana 20 kuanzisha biashara. Hivyo basi naamini kabisa kama tunge twist sera kidogo tu..badala ya kutenge fedha kwa vikundi vya vijana katika halmashauri kama inavyofanyika sasa hivi na kusema watu wenye experience ya 10+ wapeleke mapendekezo ya miradi ya biashara wapewe fedha na waajiri vijana 10+ tatizo la ajira lingepungua sana.


Wahitimu wa chuo mara nyingi wanajiingiza kwenye uchuuzi badala ya kuzalisha. Hatuwezi kujenga uchumi.kwa kila mtu akiwa mchuuzi. Tutajenga uchumi.kama tutazalisha products ili tupunguze products tunazoagiza nje ya nchi na kuongeza products tunazo export. Hili haliwezi kufanywa na vijana wanaohitimu, ila watu wenye experience...wawezeshwe kuajairi vijana.

Mitaji bado ni tatizo kwa watu wazima wengi ambao wana mawazo na idea nzuri za uzalishaji.

So my advice is tu invest kwa watu wazima experinced proffesionals ili waajiri vijana wa makundi yote matatu
 
Nilikuwa nawaza kama wewe,bila shaka wewe ni Engineer mwenzangu,hii approach huwa tunaitumia kwenye troubleshooting of machineries failure.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
tupe jibu sahihi la hayo maswali
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante boss. Wachache Sana watakuelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…