Nani adui wa vijana katika Kujiajiri. Ni Uthubutu, Serikali, au Malezi na Mazingira?

Nani adui wa vijana katika Kujiajiri. Ni Uthubutu, Serikali, au Malezi na Mazingira?

MTAJI

Mengine ngonjera tu.
Mtaji wako ni uthubutu wako unaeza anza na kidogo ulichonacho sema sisi huwa tunataka hadi tufikishe kiwango fulani ndipo tuanze rasmi kujiajiri jambo ambalo ni mtihani kulitekeleza,. Sema kikwazo pia ni mazingira si rafiki kwa biashara rasmi tozo zinazidi uhalisia, pia mfumo wa elimu haumjengi mtu kujiajiri bali kuwa mtumishi jambo linalopekea mhitimu kuona aibu na kuwa selective kuchagua kazi badala ya kujiajiri.
 
Mkuu
Mimi nimejiajiri tangu 2014
Ni mjasiriamali mdogo
Nilikataa kuajiriwa na Polisi
Sijawahi kujutia maamuzi yangu

Bado sijafikia malengo kwa 100% lakini naona milango ikifunguka siku hadi siku

Nimejifunza uthubutu, kupambana, uvumilivu na kusimamia ninachokiamini bila kuyumba ( Consistence) na vimenisaidia Sana.

Mwanzo ndugu zangu hawakunielewa, walitaka niajiriwe lakini niliweka msimamo sihitaji kuajiriwa lakini sasa wameelewa nilichokuwa namaanisha.





Sent using Jamii Forums mobile app
Huna tofauti na Mimi aisee nilipo maliza chuo nili wambia nyumbani sihitaji kuajiriwa hawa kuni elewa kabisa ila nili wambia msimamo wangu ndo huo na utabaki kuwa hivyo nashukuru Mungu toka nimalize chuo mpaka sasa sijawahi omba ajira na sijawahi ajiriwa maisha yana kwenda Mungu ni mwema sana sana kwangu nafanya biashara zangu ndogo ndogo Mungu ni mkubwa tatizo co mtaji tatizo kubwa ni uoga na uthubutu
 
Tatizo ni uthubutu tu!. Watu wanashindwa kuchukua hatua katika maamuzi mengine kama biashara, kilimo nk. Wanachotaka ni ajira tu. Pooole kijana mwenzangu.
 
Mimi siku zote naamini kwenye FAIDA kuliko MSHAHARA
Huna tofauti na Mimi aisee nilipo maliza chuo nili wambia nyumbani sihitaji kuajiriwa hawa kuni elewa kabisa ila nili wambia msimamo wangu ndo huo na utabaki kuwa hivyo nashukuru Mungu toka nimalize chuo mpaka sasa sijawahi omba ajira na sijawahi ajiriwa maisha yana kwenda Mungu ni mwema sana sana kwangu nafanya biashara zangu ndogo ndogo Mungu ni mkubwa tatizo co mtaji tatizo kubwa ni uoga na uthubutu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SABABU KUBWA NI MINDSET

Asilimia kubwa ya vijana mfano hapa Tanzania tunaishi chini ya utamaduni na mfumo wa maisha unaofanana kwa wengi. Kutokana na hali hii, wazazi/walezi wanaandaa vijana kusoma ili wapate kazi nzuri kwa kuajiriwa. Hvyo kijana anaanza kusoma akilenga kuajiriwa sehemu fulani na sio kujiajiri sehemu fulani. Kutokana na % kubwa kuwa na Mindset inayofanana, ndiyo maana tatizo la ukosefu wa ajira linazidi kuwa kubwa kwa vijana wengi.

SABABU BAADHI NDOGO NDOGO ZINAZOUNDA SABABU KUBWA TAJWA HAPO JUU NI-:

1. Kijana Kutotambua wapi aanzie ili kujiajili.
2. Vijana wengi wanahisi hawana uwezo wa kufanya kazi fulani wakisema kazi hzo ni za watu fulani au ni za mataifa fulani na mwisho wa siku hukaa bila kuwa na kitu cha kufanya maana kila wanachofikiri wanaona kwao hakiwezekani.
3. Uzembe wa kuchukua hatua, yaani kijana anasema kesho nitafanya na kesho huzaa kesho bila kuanza anachokifikiri.
4. Kukosa plan B na hvyo Kupoteza muda mwingi kulaumu Serikali, ndugu na marafiki badala ya kuangalia nini cha kufanya.
5. Vijana wengi wanahisi kujiajiri ni kuuza bidhaa tu na kama hana fedha za kuanzisha biashara fulani basi anakaa wakati anaweza kuanzisha biashara inayouza huduma na akaingiza fedha nyingi bila hata mtaji wa fedha.
6. Baadhi walijaribu kujiajiri lakini walichagua mawazo ya biashara yasiyosahihi (WRONG BUSINESS MODELS) ambapo biashara zao zilikufa mapema na wakakata tamaa.

NINI KIFANYIKE KAMA SULUHU

Suluhu kubwa ya tatizo la ajira ni jamii kwa ujumla kubadili MINDSET zao ili mtu awe na mawazo ya kujiajiri tokea akiwa mdogo.

MAMBO MENGINE YA KUZINGATIA KAMA SULUHU NI KAMA

1. Jambo la kwanza ni kuepuka vikwazo kama hivyo nilivyovitaja hapo juu.
2. Vijana watambue mtaji mkubwa ni akili na uwezo waliopewa na mwenyezi Mungu wala sio pesa.
3. Vijana wasiwe wabinafsi. Mfano, mtu anawazo zuri la biashara na hana pesa na anashindwa kumshirikisha mwenzake mwenye pesa ili waanzishe biashara na hivyo anakaa na wazo lake hadi linakufa bila mafanikio.
4. Vijana wasikimbilie kuuliza biashara gani inalipa wataangukia shimoni maana mahesabu ya kwenye karatasi ni tofauti na mahesabau halisia. Hivyo vijana wajikite katika kutatua matatizo ya watu hapo ndipo kuna biashara inayolipa maana mtu akitatuliwa tatizo lake yuko tayari kulipa kiasi chochote.
5. Kila kijana aamini kuwa anauwezo wa kufanya jambo fulani hata kama anahisi hana uwezo wa kufanya. Imani inaweza kufanya mambo makubwa.
Mkuu Umeandika Points.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ni mtu mzima. Nilikuwa kijana miaka ya mwanzoni mwa 2000. Nimejaribu kujiajiri, kuajiri na kuajiriwa. Naweza kusema kuna matatizo katika kila nyanja...kuanzia malezi, mazingira (sera) na mitaji.

1. Kwanza unapoongelea vijana inabidi uwagawe katika makundi matatu...kundi la kwanza ninwale wanaoishi elimu ya msingi au hawamalizi kabisa elimu ya msingi. Kundi la pili ninwale wanaomaliza elimu ya kati (form 4 au 6). Kundi la pili ninwale wanaohitimu vyuo (diploma/ degree). Haya makundi yana mahitaji tofauti na yana takiwa yawe treated tofauti. Kuwaweka vijana wote katika kapu moja ndo mwanzo wa kushindwa kutatua changamoto.za ajira.


Kundi la kwanza ni vijana ambao wanarudi kufanya shughuli za kiuchumi.zinazopatikana katika maeneo yao. Kwa mfano kama kuna machimbo wataenda kuchimba, kama kuna ziwa au bahari wataenda kuvua samaki na kama kuna mifugo wataanza kufuga....na kilimo.

Kwenye biashara hawa mara nyingi wanakuwa wachuuzi. Wachukue bidhaa sehemu A wauze sehemu B.

Kinacho wakwamisha vijana kwenye kundi hili ni ukosefu wa elimu za kazi wanazofanya. Wanavua samaki bila kiwa ana elimu ya uvuvi, wanalima bila kuwa na elimu ya kilimo n.k. Hivyo hujikuta hawana tija.

Kinachotakiwa hapa ni elimu juu ya kazi wanazozifanya. Bahati mbaya hakuna vyuo ambavyo vipo kwa ajili yao..ukiacha vyuo vya vyeta ambavyo vimejikita kwenye skills fulani fulani kama ujenzi, uashi, ufundi umeme n.k.

Tunahitaji kuwa na vyuo vya kila fani kutokana na shughuli za kiuchumi katika maeneo husika. Kwa mfano kama tungekuwa na vyuo vya uvivi kanda ya ziwa...acha kile cha nyegezi ambacho kinachukua watu wachache...ili kila mtu anaye vua awe na elimu ya uvuvi, kila anaye lima nyanya awe na elimu ya kuzalisha nyanya, kila.anaye lima mahindi awe na elimu ya kuzalisha mahindi Ili watu wasifanye kazi kwa mazoea ambazo hazina tija.

2. Vijana wa elimu ya kati...hawa mara nyingi wanatakiwa kuwa kama wa kundi la kwanza au kuwa ma supervisor. Hawa nao wanahitaji elimu kama kundi la kwanza ili wawasimamie au waajiri kundi la kwanza.

3. Vijana wa elimu ya juu hawa tatizo lao kubwa ni mfumo wa elimu. Wanamaliza wakiwa na vyeti lakini hawajui kazi walizosomea. Unakuta mtu ana vyeti say vya degree ya business administration halafu unamuuliza anaweza kufanya nini...hakuna. Hawa mara nyingi wanaandaliwa kuajiriwa na kupata additional on job training ndo wanaweza kufanya kitu.

Kwa hiyo kujaribu kutaka kundi hili wajiajiri kwa fani zao mara baada ya kuhitimu ni kitu ambacho hakiwezekani. Maana wanahitaji additional training ili kuwafanya wawe na fani. Elimu ya vyuo ni kama ya ku wa expose tu kwenye mambo mengi bila kuwajengea specific proffession. Hawawezi kujiajiri kamwe.

Therefore
1. Serikali na wadau wanahitaji kujenga kuwa na njia za kuwapa ujuzi watu wa kundi la kwanza na la pili.

2. Serikali inahitaji kuwapa incentive wataalamu ili waanzishe biashara ambazo zitaajiri watu wa kundi la tatu. Ni rahisi kwa mtu aliyekuwa kwenye ajira kwa miaka 10 kuanzisha biashara ambayo itaajiri vijana 20 kuliko kuwapa hela kikundi cha vijana 20 kuanzisha biashara. Hivyo basi naamini kabisa kama tunge twist sera kidogo tu..badala ya kutenge fedha kwa vikundi vya vijana katika halmashauri kama inavyofanyika sasa hivi na kusema watu wenye experience ya 10+ wapeleke mapendekezo ya miradi ya biashara wapewe fedha na waajiri vijana 10+ tatizo la ajira lingepungua sana.


Wahitimu wa chuo mara nyingi wanajiingiza kwenye uchuuzi badala ya kuzalisha. Hatuwezi kujenga uchumi.kwa kila mtu akiwa mchuuzi. Tutajenga uchumi.kama tutazalisha products ili tupunguze products tunazoagiza nje ya nchi na kuongeza products tunazo export. Hili haliwezi kufanywa na vijana wanaohitimu, ila watu wenye experience...wawezeshwe kuajairi vijana.

Mitaji bado ni tatizo kwa watu wazima wengi ambao wana mawazo na idea nzuri za uzalishaji.

So my advice is tu invest kwa watu wazima experinced proffesionals ili waajiri vijana wa makundi yote matatu
 
Nilikuwa nawaza kama wewe,bila shaka wewe ni Engineer mwenzangu,hii approach huwa tunaitumia kwenye troubleshooting of machineries failure.
Kuna kitu kinaitwa root cause failure analysis (RCA)

bila ufaham mzuri kila mtu atazuka na visababu vyake kimtazamo ambavyo sio root cause.

lakini jibu sahihi lisilenge mtu mmoja ametokaje Bali asilimia mfano 50% au 70%

tunapotoa majibu tunatakiwa kutazama Wastani wa wahusika sio mafanikio ya mtu mmoja watatu au wanne sababu hawa hawawakilishi sample spaces or representative sample

vijana kwanini asilimia kubwa hawawezi kutoka/kufanikiwa/kupiga hatua/kujiajiri/kujitegemea/kujijenga ...... tatizo ni nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
tupe jibu sahihi la hayo maswali
1. Aibu...... nikweli nchi nzima vijana wanakwama sababu wanaaibu? Sio kweli

2. Uzembe .... nikweli vijana mikoa yote wazembe? Sio kweli

3. Elimu.... nikweli vijana wakitanzania asilimia kubwa Elimu haiwasaidii .... may be but not certainly

4. Malezi.... nikweli malezi yanawakwamisha maelfu ya vijana! Kwamba wazazi wanamalezi yakufanana nchi nzima? Kigoma, tanga, mtwara .... singida......shinyanga? Sio kweli

5. Mazingira... je mazingira yanaweza kuwa sababu? May be but not certainly kwa taifa zima

6. Uthubutu.... nikweli vijana wengi hawana uthubutu? Kivipi kama taifa tunaongelea asilimia kubwa ya vijana zaidi ya 50%

7. Uoga... kwamba zaidi ya 50% ya vijana wetu waoga? Sio kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye kujiajiri ni kutokufikiria zaidi na kufanya uchunguzi wa nini ambacho anaweza kukipeleka sokoni kikakubalika kirahisi.

Ila Mkuu tuache siasa nyingi pia

UVIVU TUU! na TAMAA za kijinga..

tukirudi kwenye kuajiriwa utakubaliana na mimi kuwa kila taasisi inahitaji watu wakugrow value ya shirika/kampuni sasa miongoni mwa vijana wengi wamejawa na uvivu+tamaa za haraka haraka anataka akipata hela tayari break yake ya kwanza kwenye gari na mademu! + MALEZI MABOVU.

Siku zote ukitaka kupima Inteligence test ya kijana mpe kazi bila pesa,hata ya kujitolea.

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante boss. Wachache Sana watakuelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom