Nani aliwadanganya Watanzania kuwa maziwa ni tiba ya mtu aliyemeza sumu?

Nani aliwadanganya Watanzania kuwa maziwa ni tiba ya mtu aliyemeza sumu?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Huu uongo umekuwepo miaka mingi sana. Ukweli ni kuwa maziwa hayana nguvu yoyote ya kutibu sumu. Mtu anayekunywa maji na anayekunywa maziwa baada ya kunywa sumu wote wapo sawa.

Unakuta mtu anafanya kazi kiwandani, mgodini au sehemu yenye vumbi, jioni anapiga maziwa kwamba anazuia sumu. Na wenye viwanda nao wanatoa maziwa eti kuua sumu! Tiba sahihi ya kuaminika ya haraka kwa mtu aliyekunywa sumu ni unga fulani maalumu wa makaa(Activated charcoal) huu ni mkaa ambao umechomwa kwenye hewa.

Huu mtu aliyenyweshwa sumu akibugia unaenda kuibana sumu na kuifanya isiingie kwenye damu. Huu hutengenezwa kwa hata kwa vifuu vya nazi.

Kama unafanya kazi sehemu yenye vumbi kali au hewa yenye sumu ni vema ukatumia barakoa, maziwa hayatakusaidia kitu

Mkaa huo huwa namna hii.

productimg

aktiivsuse-pulber-centralsun-1-e1644948360623.jpg


2003-Activated_Charcoal-732x549-thumbnail-732x549.jpg


=======
Kupata majibu sahihi tembelea Jamiicheck: UZUSHI - Maziwa fresh ni tiba ya sumu, yanaweza kutumika kwenye mazingira ya dharura kuokoa uhai
 
Nimesoma kwa makini kumbe ni swaga za biashara. Ila maziwa nadhani, hata kama hayana nguvu kwenye sumu, yanao msaada fulani.

Ninakumbuka nikiwa mdogo niliwahi kung’oa mhogo shambani kwa mtu ni kaula wote japo ulikuwa mchungu hatari ila njaa ili sababisha uchungu nisiusikie. Baada ya kuumaliza nikaanza kusikia kizunguzungu, hisia za kutapika, nguvu kuisha na kichwa kuuma. Nikasema huu mhogo ulivyokuwa mchungu itakuwa sumu yake imeingia mwilini. Mfukoni nilikuwa na tshs. 500 nikaenda kununua maziwa mara, sijui siku hizi yako wapi, baada ya kuyanywa nikapata nafuu. Hivyo maziwa yanasaidia kama sumu siyo kali na nadhani ni baadhi ya sumu. Mfano siamini kama maziwa yanaweza kukusaidia dhidi ya sumu ya nyoka.
 
Ngoja kwanza!

Acid + Base > Maji + chumvi

Sumu ni (Acid) + Maziwa ni (base) > baada ya kunywa maziwa molecule za ACID huvunjwa na kugeuka Maji na jasho unazikojoa kama mkojo au kuharisha!

Maziwa yanayozungumziwa hapo ni Yale ORIGINAL AMBAYO HAYAJACHANGANYWA NA MAJI
wanashauri ng'ombe wa kenyeji au mama anayenyonyesha

Note! siyo kwa kila sumu utapona, huwa Inategemea na aina ya sumu zingine hutoboi hata nusu SAA unakata
 
Ngoja kwanza!

Acid + Base > Maji + chumvi

Sumu ni (Acid) + Maziwa ni (base) > baada ya kunywa maziwa molecule za ACID huvunjwa na kugeuka Maji na jasho unazikojoa kama mkojo au kuharisha!

Note! siyo kwa kila simu utapona, huwa Inategemea na aina ya sumu zingine hutoboi hata nusu SAA unakata
milk is a weak acid not base
 
Kumbe unatangaza biashara.....
Me nataka mkaa kwakuwa nishawah kuutumia kwenye kupunguza mwili na kweli ulifanya kazii..
Sasa kuna vikilo nimeongeza nataka mkaa nivipunguze fasta
Unatumiaje na unafanyaje kazi?
 
Unapigia dawa promo yako.wazungu wenyewe wanatumia kusaidia mtu aliyekunywa sumu.
Ndo nyie mnaoichambua teknolojia utazani mlitunga wote
 
Nimesoma kwa makini kumbe ni swaga za biashara. Ila maziwa nadhani, hata kama hayana nguvu kwenye sumu, yanao msaada fulani.

Ninakumbuka nikiwa mdogo niliwahi kung’oa mhogo shambani kwa mtu ni kaula wote japo ulikuwa mchungu hatari ila njaa ili sababisha uchungu nisiusikie. Baada ya kuumaliza nikaanza kusikia kizunguzungu, hisia za kutapika, nguvu kuisha na kichwa kuuma. Nikasema huu mhogo ulivyokuwa mchungu itakuwa sumu yake imeingia mwilini. Mfukoni nilikuwa na tshs. 500 nikaenda kununua maziwa mara, sijui siku hizi yako wapi, baada ya kuyanywa nikapata nafuu. Hivyo maziwa yanasaidia kama sumu siyo kali na nadhani ni baadhi ya sumu. Mfano siamini kama maziwa yanaweza kukusaidia dhidi ya sumu ya nyoka.
Hayasaidii, hata ungekunywa maji ungepona. Ni sumu tu haikuwa kali hivyo nguvu yake ikaisha yenyewe.
 
Ngoja kwanza!

Acid + Base > Maji + chumvi

Sumu ni (Acid) + Maziwa ni (base) > baada ya kunywa maziwa molecule za ACID huvunjwa na kugeuka Maji na jasho unazikojoa kama mkojo au kuharisha!

Maziwa yanayozungumziwa hapo ni Yale ORIGINAL AMBAYO HAYAJACHANGANYWA NA MAJI
wanashauri ng'ombe wa kenyeji au mama anayenyonyesha

Note! siyo kwa kila sumu utapona, huwa Inategemea na aina ya sumu zingine hutoboi hata nusu SAA unakata
Huu ni uongo sana
 
Nimesoma kwa makini kumbe ni swaga za biashara. Ila maziwa nadhani, hata kama hayana nguvu kwenye sumu, yanao msaada fulani.

Ninakumbuka nikiwa mdogo niliwahi kung’oa mhogo shambani kwa mtu ni kaula wote japo ulikuwa mchungu hatari ila njaa ili sababisha uchungu nisiusikie. Baada ya kuumaliza nikaanza kusikia kizunguzungu, hisia za kutapika, nguvu kuisha na kichwa kuuma. Nikasema huu mhogo ulivyokuwa mchungu itakuwa sumu yake imeingia mwilini. Mfukoni nilikuwa na tshs. 500 nikaenda kununua maziwa mara, sijui siku hizi yako wapi, baada ya kuyanywa nikapata nafuu. Hivyo maziwa yanasaidia kama sumu siyo kali na nadhani ni baadhi ya sumu. Mfano siamini kama maziwa yanaweza kukusaidia dhidi ya sumu ya nyoka.
Sumu inayozungumziwa hapa Ni POISON sumu ya nyoka sio aina ya sumu inayozungumziwa hapa yaani sumu ya nyoka ni VENOM
 
Huu uongo umekuwepo miaka mingi sana. Ukweli ni kuwa maziwa hayana nguvu yoyote ya kutibu sumu. Mtu anayekunywa maji na anayekunywa maziwa baada ya kunywa sumu wote wapo sawa. unakuta mtu anafanya kazi kiwandani, mgodini au sehemu yenye vumbi, jioni anapiga maziwa kwamba anazuia sumu. Na wenye viwanda nao wanatoa maziwa eti kuua sumu! Tiba sahihi ya kuaminika ya haraka kwa mtu aliyekunywa sumu ni unga fulani maalumu wa makaa(Activated charcoal) huu ni mkaa ambao umechomwa kwenye hewa. Huu mtu aliyenyweshwa sumu akibugia unaenda kuibana sumu na kuifanya isiingie kwenye damu. Huu hutengenezwa kwa hata kwa vifuu vya nazi. Kama unafanya kazi sehemu yenye vumbi kali au hewa yenye sumu ni vema ukatumia barakoa, maziwa hayatakusaidia kitu

Mkaa huo huwa namna hii.

productimg

aktiivsuse-pulber-centralsun-1-e1644948360623.jpg


2003-Activated_Charcoal-732x549-thumbnail-732x549.jpg

Usiwachafue wengine ili wewe ufanikiwe
Fanikiwa kwa ubora na uwezo ulionao

Kila la heri
 
Back
Top Bottom