Nani aliyepanga haya mauaji ya hawa Marais Abraham Lincoln na John Kennedy?

Nani aliyepanga haya mauaji ya hawa Marais Abraham Lincoln na John Kennedy?

Ulimwengu hautokuja kufahamu Kua Ni nani alitoa Amri ya kiofisi kwamba JFK auwawe! Na hii inatokana Na sababu hao watu waliopanga Hilo swala huenda wameshakufa kutokana Na UMRI Na hofu, Au wamekaribia kufa Au wameamua kukaa kimya!
 
Eiyer huku nikutafuta umaarufu wa chee unavyokoments as if umefanya strong research umetafsiri hii story hadi nukta najua nachoongea hii sio mpya man

Eiyer kama unapenda umaarufu wa chee lata na hii UTATA WA TAREHE 11NOV utapata habari nyingi tu nenda kakusanye secondary data njoo tililika watu huwa hawasomi itawapata tu na utaonekana great thinker

njoo na CD mpya hii ime exp man si wote wajinga hivo Eiyer

mi nadhani hoja kubwa si kucopy ila hoja kubwa hapa je hiko mnachodai kakikopi kina ukweli kiasi gani? hivyo nashauri kwa lengo la kujifunza basi ni vema tukajikita kwenye kujadili yaliyomo kwenye taarifa yake pasipo kuzingatia amecopy au ni andiko lake binafsi
 
Mkuu Eiyer safi sana kwa Uzi wako uliokwenda shule sio mambo ya kila siku KURIDHISHANA sijui na nini huko..l
 
Last edited by a moderator:
Eiyer huku nikutafuta umaarufu wa chee unavyokoments as if umefanya strong research umetafsiri hii story hadi nukta najua nachoongea hii sio mpya man

kuCopy nako ni njia ya kufikisha ujumbe kwani sio wote tulioiona hiyo nakala, hata we ungefanya msaada mkubwa km ungeCopy na kutuletea. Maudhui ni kujibu yaliyomo
 
Mkuu Eiyer kuna sababu kadhaa zinatajwa Kua zilipelekea kuuwawa Hawa Marais. Lkn sababu iliyokubwa ambayo inafanana Kwa marais wote, Ni ile ya kutaka kubadilisha mfumo Wa sheria wa kimabenki Au Wa kifedha kutoka KTK mabwanyenye wachache Na kuhodhiwa Na wamarekani wote!

Na KTK Hili kumetajwa mpk benki ya Uvaticano ambayo inaonekana Kua Ndio yenye nguvu za mambo ya uchumi Kwa USA NA Kwa Dunia nzima Kwa ujumla! Kwahiyo Hawa mabwanyenye Au Magodfather hawakukubaliana Na huo mpango!

Na kuna Note ambaza zilikua mpya zilikua zimechapishwa wakati Wa utawala Wa JFK zenye kumilikiwa Na raia wote Wa USA Na zilianza kutumika wakati huo! Lkn alipokufa tu JFK, HIZO note zilipigwa marufuku kutumika Na kukusanywa zote!
 
Last edited by a moderator:
Sababu zingine Mkuu Eiyer Ni kwamba JFK alitaka kurudisha vikosi Vya majeshi ya Marekani nyumbani kutoka Vietnam. Kitu ambacho watendaji wengine Wa Serikali ya USA walikua hawataki. Yeye akawa anataka kutumia nafasi yake ya urais kuwarudisha.


Kitu kingine JFK hakutaka kuivamia Cuba, ikumbukwe Kua wakati huo kulikua Na vita baridi na wakati huo Propaganda zilikua kubwa sn mpk Kusema kwamba ndani ya CIA Au FBI kuna makachero Wa Kirusi. Kwahiyo JFK akawa analazimishwa kuipiga Cuba lkn yeye akawa hataki! Kwa hiyo KTK Hili system ilimchukia!
 
Last edited by a moderator:
Kitu kingine mkuu Eiyer JFK alitaka kulifuta shirika la CIA kutokana Na namna ya utendaji wake na namna linavyotumia Pesa nyingi sn! Kwahiyo wengi hawakukubaliana KTK Hilo swala Na ikapelekea mipango ya chini Kwa chini kumuua JFK!

CIA na FBI wanahusika KTK Haya mauaji Kwa asilimia 80 kutokana Na wao kutokushughulika kuwaokoa Hawa marais kabla ya vifo Au baada ya vifo vyao Kwa kusaidia kikamilifu kupelekea kukamatwa Au kuwataja wahusika wazi wazi Na kuwafikisha KTK mikono ya sheria! Kwa hiyo hivi vyombo Vya usalama Ndio vilipanga mauaji haya kikamilifu Na Ndio Maana Hadi Leo wamepiga kimyaaaa!


Kuna dalili za Magodfather Wa kimarekani Na duniani KTK mauaji ya JFK ata Lincon Na KTK haya hili swala halikupangwa tu ndani ya USA.


Kitu kingine JFK alisahau maisha yake binafsi Au alisahau uhai wake Ni muhimu kuliko kuwatumikia hao wamarekani Na kutaka kuwatumikia Kwa Haki NA uadilifu na kutaka kuwapa haki sn raia kitu ambacho kilikua Ni kero Kwa Magodfather wachache na kuanza kupanga mipango ya kumuua!

Nitakuja tena KTK Hilo swala la miaka 100.
 
Last edited by a moderator:
kuCopy nako ni njia ya
kufikisha ujumbe kwani sio wote tulioiona hiyo nakala, hata we ungefanya
msaada mkubwa km ungeCopy na kutuletea. Maudhui ni kujibu
yaliyomo
Stata Mzuka nakubaliana na wewe lakini jamaa angeeleza kua hii ni nukuu kuliko yeye amekazana et kafanya tafiti yeye wakati najua hakufanya hiyo tafiti nandio kanuni ya nukuu taja wote ulinukuu
 
hii ni copy and past toka gazet rai no 686 la feb 2007 alhamis mwandish
WILLIAM SHAO heading WANAOTAKA KUONA YALIOFICHIKA zaid soma hum the
secret behind science milacle,na how to secceed Eiyer njoo ubishe hujaumiza kichwa.....
Huenda Eiyer mwenyewe ndio mwandishi wa hiyo makala ya gazetini.
 
Last edited by a moderator:
Wakuu tujikite kwenye kujadili hoja Na si kujadili Eiyer katoa wapi hiyo habari!

Kuna vyanzo Vya habari vingi sn Na kuna habari nyingi sn juu ya Haya matukio! Mtu Unaweza ukasoma habari zote Na kuziunga Au kuzifanyia utafiti na ukaja NA habari yako Au maelezo yako! Kwahiyo KTK Hilo Mkuu Eiyer yuko sawa Kabisa! Sisi tujikite KTK kujadili Mada!
 
Last edited by a moderator:
Misingi ya taifa la Marekani inafahamika na jamii ya watu wanaoiendesha hii Dunia. ILLIMINATI at work.
 
Stata Mzuka nakubaliana na wewe lakini jamaa angeeleza kua hii ni nukuu kuliko yeye amekazana et kafanya tafiti yeye wakati najua hakufanya hiyo tafiti nandio kanuni ya nukuu taja wote ulinukuu

Msamehe mkuu may be kasahau kuandika kuwa kanukuu.
 
Mkuu Eiyer kwanza Kabisa nikupongeze kwa habari yako nzuri Na yenye changamoto nyingi Na yenye kuitaji kufikiria Kwa kina sn Na Kua Na ushahidi Wa kutosha!


Taifa la Marekani limepitia mambo mengi sn mpk kufikia hapo lilipo! Na kiasi Fulani hao marais wote wawili vifo vyao vilikua Ni Vya kupanga! Na waliohusika Ni System yenyewe KTK kutekereza Hayo mauaji! NA Ndio Maana wale walioua hao marais na wao waliuawa ili kufuta ushahidi Kabisa!

Ngoja niongeze kidogo Kwa kusoma vyanzo mbalimbali Vya hao marais then Nitakuja Na mchango mwingine kidogo! Lkn Kwa sasa hivyo Ndio navyoweza Kusema!

Pamoja sana mkuu!!!!!!!!!
 
Mmh! Watu hao wapange kitu kwa miaka mia moja!!!
Who know? Ok!

Kwenye kupangwa hakuna kinachoshindikana mkuu

La msingi ni kujiuliza kama yamepangwa ni nani aliyepanga na kwanini!
 
Misingi ya taifa la Marekani
inafahamika na jamii ya watu wanaoiendesha hii Dunia. ILLIMINATI at
work.
Eiyer kubali kwanza copy &pest kama kweli ungefanya tafiti ushiriki wako usinge kua hafifu hivi ungekua na mchango mkubwa kutokana changamoto ulizopiti wakati wa tafiti.
 
hata kama ni copy and paste bado hatujajikita kwenye mada husika sijui wa tanzania tunashida gani kwani huwezi fanya research kwa kutumia vyanzo vya wengine na isitoshe kama alisoma kwenye links mbalimbali na akakitafsiri kile kilichopo huko akakileta hapa hiyo ni research. sio lazima ukahoji watu au ubebe vifaa. mi nazani njia bora kukosoa kile alicho andika ni kupinga kwa kutoa facts na kuthibitisha yale aliyoongea kama ni uongo lakini sio kusema mtu hajafanya research. kama we uliisoma sehemu na ukuona haja ya ku share na wenzio basi usiwakatishe tamaa wanaotamani kujua sio kila links unazozisoma basi na wengine wanapenda kuzisoma kuna watu internet ni social networks na some of links mkuu Eiyer hata mimi bado najiuliza hawa watu wana nguvu kiasi gani, huwa wanakutania wapi, na mission yao ifuatayo ni ipi
 
Last edited by a moderator:
Huwa nasikitika zaidi kuhusu JFK sijui aliikpsea nini Marekani hebu Google hii, The Kennedy curse
 
Back
Top Bottom