Nani amelipa Tsh Milioni 200 tangazo la Tanzania kwenye jengo la Burj Khalifa, Dubai?

Nani amelipa Tsh Milioni 200 tangazo la Tanzania kwenye jengo la Burj Khalifa, Dubai?

Acha ujinga kijana, mnataka maendeleo ila kuumia hamtaki.

Hilo ni tangazo la muhimu kama ya nchi nyingine tu.

USIJE NIITA CCM, SIJAWAHI IPENDA CCM TOKA NIZALIWE lakini tusiwe wajinga wa kubisha tu hata jambo lenye manufaa kwa taifa kama hilo.
Kwahio kuwekwa kwenye mataa ya burj khalifa ni maendeleo?
 
Bendera ya Tanzania inapepea UN na kwenye balozi zetu duniani kote, Leo lipi jipya kuonesha bendera kwa dakika 3?
Huko UN inalipiwa kama burj khalifa? Au unafikiri imeekwa bure pale
 
Kwa Hilo tangazo tu,watu watajenga mahekalu mbezi beach,njiro,Shangani,mbweni(Dar na Zenj)uzunguni dodoma.na magari ya kifahari yatanunuliwa
Kama dkk 3 ni milion 157 likikaa siku nzima do the maths😅
 
Hata ingekuwa fedha nyingi zaidi ya hiyo imetumika, kuitangaza nchi ni jambo zuri sana. Matokeo ya hizo dakika tatu ni zaidi ya hizo fedha kiduchu zilizotumika, binafsi nimpongeze aliyosuggest hilo jambo.
 
Baadhi ya watanzania,kazi yao kulalamika,fursa za kupata kipato,zikija anabakia kulalamika.Wageni wanazitumia hizo fursa,mpaka wao wanashangaa wanasema watanzania ni watu wa ajabu,wakati nchi ina fursa nyingi za kufuatilia ofisi zinazohusika,wao ni kulalamika.Leo mgeni,anakuja Tanzania anazifuatilia fursa,na kuzifanyia kazi.Utamkuta mgeni ndio anasafirisha bidhaa kadhaa nje,madini,mazao kama katani,leo katani inakwenda falme za kiarabu,wamegundua katani ya Tanzania ndio nzuri,kutengeneza jipsum,wasafirishaji wa hiyo katani,ni wageni sio watanzania,sisi ni kulalamika tu,kwa jambo hata mtu hana ushahidi nalo.
Hio process ya kusafirisha katani unafikiri ni jambo rahisi? Unafikiri kwa nini fursa hizo wanazifaidi wageni na viongozi mafisadi tu!

Mchina akija bongo anakuja kuangalia gepu kisha anarudi serikalini nchini kwao na kuomba support wanapewa mipunga ya kueleweka wakija huku ni kuwekeza chap kupitia viwanda na kuanza uzalishaji mara moja bila kuchelewa.

Serikali ya TZ inaweza kumpa nani billion 5 aanzishe kiwanda? Ila billion 70 za kukodisha system ya Tanesco kifisadi zipo.

Haya ndo mnasema wananchi wanalalamika huku fursa zipo mtu mwenye uchumi wa laki 5 kwa mwezi anasafirishaje katani?
 
200m tu jamani? Zamaradi aliweza serikali inashindwaje sasa, watu mna umasikini wa akili.
 
Umelipa wewe,

Unajua faida ya kilichofanyika hapo au ndio "Join the Chain "🤣🤣🤣

Nikusaidie tu, Tanzania haijatoa hata Mia,

#HAKUNA KAMA SAMIA
Ungeweka tu majibu bila kuhemka..!! Mara umelipa wewe, mara hajui faida ya kilichofanyika, mara Tanzania haijalipa chochote... Ungeeleza tu hizo faida na kusema nani kalipa tungeelewa... UMEJIGAMBA KUUWA ADUI KWA KUMPIGA BOMU MOCHWARE KAHIFADHIWA BAADA YA KUFA
 
200m tu jamani? Zamaradi aliweza serikali inashindwaje sasa, watu mna umasikini wa akili.
Umasikini wa akili ni huu unaoonesha wewe hapa. Kuziona mil.200 zinzoweza kujenga madarasa 6 au madawati 10,000 Kwa shule ya kijijini kuwa ni fedha ndogo wakati hutuelezi impact ya tangazo la bendera ya Taifa ni ipi Kwa utalii au uwekezaji?
 
Kama dkk 3 ni milion 157 likikaa siku nzima do the maths[emoji28]
Nimemsikia waziri wa kazi asubui hii Clouds FM Power breakfast akisema kuwa Mama amepewa offer ya bure kuonekana picha ya bendera yetu , sura yake na maneno Tanzania is ready for taking off, kawaida ya matangazo kama hayo yanapokezana matangazo mbali mbali
 
Nimemsikia waziri wa kazi asubui hii Clouds FM Power breakfast akisema kuwa Mama amepewa offer ya bure kuonekana picha ya bendera yetu , sura yake na maneno Tanzania is ready for taking off, kawaida ya matangazo kama hayo yanapokezana matangazo mbali mbali
Kama bure sawa
 
Mamlaka ya uendeshaji wa jengo refu zaidi duniani la Burji Khalifa lililoko Dubai hutoza kati ya dola 67,000 hadi 87,000 ambazo kwa ubadilishaji fedha kwa haraka haraka inafiki Tshs. Milioni 157 hadi 200 hivi kwa dakika 3 kuweka tangazo kwenye jengo lote la Burji Khalifa.

Fedha hii kwa nchi masikini kama hii bado ni kubwa na ingeweza kufanya jambo la maana. Jana Februari 28 jengo hilo limetangaza bendera ya Tanzania kwa dakika 3 na wenye Serikali yao wakatutangazia neema kwamba nasi tumeonekana Dubai.

Hebu tuzionee huruma fedha za walipa kodi wanaojikamua huku sisi viongozi tukiishi kwa anasa.

View attachment 2134765
Hio Hela so V8 Moja tu ya serikali au ? Nilijua Billion I mbili ila kama ni hiyo kwa nchi kama hii ni hela ya kawaida Sana.
 
Back
Top Bottom