Nani anaestahili kuchukua nafasi ya IGP kumrithi Sirro endapo mabadiliko yakitokea?

Nani anaestahili kuchukua nafasi ya IGP kumrithi Sirro endapo mabadiliko yakitokea?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Iwapo Raisi Samia ataridhia kufanya mabadiliko katika Jeshi la Polisi kwa kumuondoa IGP Sirro, unadhani ni nani atafaa kukabidhiwa mikobo ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini?

Inawezekana tunaona wengi wao ni tatizo, ila ukweli ni kwamba kuna mmoja,wawili au watatu miongoni mwao wanaweza kuwa na afadhali au hata kufaa kabisa kwa nafasi hiyo.

Hivyo, wadau kupitia hapa JF, tutoe mapendekezo ya nani anafaa kumrithi Sirro iwapo ataondoka, ataondolewa au kustaafu kwa mujibu wa sheria.

Kwa mnaowajua vizuri vigogo wa hili Jeshi, msaidieni Mama kujua ni yupi anafaa kuwa IGP baada ya Sirro(tumshauri).

Karibuni kwa mapendekezo (vetting isiyo rasimi).
 
Iwapo Raisi Samia ataridhia kufanya mabadiliko katika Jeshi la Polisi kwa kumuondoa IGP Sirro, unadhani ni nani atafaa kukabidhiwa mikobo ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini?

Inawezekana tunaona wengi wao ni tatizo, ila ukweli ni kwamba kuna mmoja,wawili au watatu miongoni mwao wanaweza kuwa na afadhali au hata kufaa kabisa kwa nafasi hiyo.


Hivyo, wadau kupitia hapa JF, tutoe mapendekezo ya nani anafaa kumrithi Sirro iwapo ataondoka, ataondolewa au kustaafu kwa mujibu wa sheria.

Kwa mnaowajua vizuri vigogo wa hili Jeshi, msaidieni Mama kujua ni yupi anafaa kuwa IGP baada ya Sirro(tumshauri).

Karibuni kwa mapendekezo( vetting isiyo rasimi).
Hayupo mpaka tuwe na katiba mpya, viongozi wengi kwenye jeshi wapo kichama kuliko viapo vyao chini ya katiba ya Sasa , msitegemee jipya chini ya katiba hii na sheria hizi za kikoloni za jeshi la police
 
Hayupo mpaka tuwe na katiba mpya, viongozi wengi kwenye jeshi wapo kichama kuliko viapo vyao chini ya katiba ya Sasa , msitegemee jipya chini ya katiba hii na sheria hizi za kikoloni za jeshi la police
Hilo nalijua ,ila tupendeleze wa afadhali maana lazima tu atoke humo humo.

Naamini humu wako watu wanaowaju vizuri sana viongozi wa hili Jeshi hivyo wanaweza kusaidia.
 
Kwanza IGP, makamishina wote na ma-RPC wote wastaafishwe kwa manufaa ya umma. Pili achukuliwe mjeda mmoja aliyesomea sheria ateuliwe kuwa IGP. Halafu baadhi ya polisi waliosomea sheria na utawala wapandishwe vyeo wawe makamishina na ma-RPC.
 
Mkuu jeshi la police linawatu wazuri Sana , ila wanaalibiwa na mfumo ,hata IGP wasasa sio kwamba ni mbaya ila amealibiwa na mfumo tu , ukimchukua leo IGP wetu wa Sasa ukampeleka ZAMBIA utashangaa
Hivi yule OCD alemwambia Mbowe hatoshinda ubunge,ameharibiwa na mfumo au nae ni kada tangu siku nyingi?

Na unaweza kupewa cheo kama sio kada?

Hapa inawezekana ndio penye tatizo la msingi.
 
Mkuu jeshi la police linawatu wazuri Sana , ila wanaalibiwa na mfumo ,hata IGP wasasa sio kwamba ni mbaya ila amealibiwa na mfumo tu , ukimchukua leo IGP wetu wa Sasa ukampeleka ZAMBIA utashangaa
Sirro huyu aliyezoea kufukuzana na Panya Road ndiyo umpeleke nchi za watu! Unataka Watanzania wote tuonekane vituko!
 
Zirro aondolewe maana kuali zake zile ni za kuleta maafa ,yaani ameruhusu polisi waue watu wa hovyo hovyo.
 
Kwanza IGP, makamishina wote na ma-RPC wote wastaafishwe kwa manufaa ya umma. Pili achukuliwe mjeda mmoja aliyesomea sheria ateuliwe kuwa IGP. Halafu baadhi ya polisi waliosomea sheria na utawala wapandishwe vyeo wawe makamishina na ma-RPC.
Hao ambao wengi wao wana stashahada na elimu ya kidato cha sita(wajeda) ila wanavyeo vikubwa hawawezi kupata hiyo bahati.
 
Hivi yule OCD alemwambia Mbowe hatoshinda ubunge,ameharibiwa na mfumo au nae ni kada tangu siku nyingi?

Na unaweza kupewa cheo kama sio kada?

Hapa inawezekana ndio penye tatizo la msingi.
Nimekuelewa Sana mkuu, mfumo ni pamoja kuingiza watu kwenye muhim Kama majeshi yetu, Ili kulinda madaraka yako Kama kiongozi, nao kukubali kutumiwa, nje ya viapo vyao ,hakuna katiba mpya Ili kutenganisha haya Mambo, hakuna jipya
 
Back
Top Bottom