Nani anafaa kuwa Spika mpya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Nani anafaa kuwa Spika mpya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Mussa Azan Zungu ni mtu sahihi kabisa kujaza nafasi ya spika wa Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania.

Uzoefu, kukubalika kwa wabunge na busara zake za kuongoza vikao vya bunge vinamfanya awe ni chaguo la wazi kabisa.

%5BUNSET%5D.jpg

Pichani Zungu akiongoza kikao cha bunge kama mwenyekiti.
 
Wana Jf

Kwa maslahi mabana ya nchi Tanzania namwona S.Masele akifaa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania. Mienendo yake na umaili katika siasa, bado ni Bora kuliko Dr. TULIA na Zungu, ili kupata spika aliye bora, wagombea wote wait we wajieleze kama Stev. atawatupa mbali sijui.

Bwana Steve akiwa anaongoza Bunge fulani aliwahi kuzushiwa sokoto fulani kulinda maslahi ya spika mwingine ambaye alikuwa mbadhirifu. Ndugai akqmfqnyiq finish wakamwondoa kwa Manufacturers yao wenyewe kulindana style.
 
Kwa wasio fahamu Ndugai alikuwa mtu muhimu sana kwa maslai mapana ya taifa na mbunge mmoja mmoja hakika walimpenda.

Pili ukiachia yeye kama yeye kuomba msamaha kauli yake au alichoongea Ndugai hakina ubaya wowote kwa wabunge na wananchi wa kawaida hata vyama pinzani, hivyo wabunge ambao siyo mawaziri wanaweza kuwa upande wa Ndugai. Na wabunge ambao mawaziri hawa watakuwa kimya kwa sababu ya kulinda uwaziri wao.

Lingine kupata spika mpya wa awamu mpya huwa kunakuwa na mikiki mikiki mingi sasa kupata Spika wa kuokota dodo katika msufi lazima kutatokea heka heka.

Lingine karibu wabunge wote ni ngumu wakajizungumzia kufika pale bila kumtaja Magufuli, kwani kuna wabunge wengi hata awakustahili na hawakuwa na sifa ya kuingia bungeni lakini kupitia Magu waliingia na hawa bado hawana mahaba na mama kivile wenyewe wanamahaba na mzimu.

Hapa swali la kujiuliza wote ni kuwa hivi ni kweli mizimu ipo au haipo inanguvu au haina nguvu? maana kanisani na msikitini wanakataa lakini dodoma itasema.
 
Huyo hana busara hata chembe, zamani niliamini katika utu uzima dawa yaani ni busara, lakini kwa ujinga wa baadhi ya wazew kama huyo siafiki kabisa
 
Kama ni uzoefu na kuheshimu kanuni za bunge ni Zungu.
Na zamani kulikuwepo na Janester Mhagama lakini alipoukwaa uwaziri hupinga kila kitu hoja zitolewazo na kambi ya upinzani.
Change nae angefaa.
Lakini Dr Tulia anaweza akatuliza bunge pia.
 
Chaguo la spika ni chaguo la Mwenyekiti wa CCM, tutaenda mbele tutarudi nyuma kama Mwenyekiti wa CCM hatoridhia basi kinachofanywa ni ramli tu.

Nilichogundua mpaka sasa kwa Mwenyekiti wa CCM anataka sura mpya lakini zenye uwezo na uthubutu hivyo tusishangae spika akawa ni mtu tofauti na wanaotajwa tajwa.

Jina la katibu mkuu wa CCM Ndg.Chongolo halikuwahi kufikiriwa hata kidogo lakini ndio akawa hivyo tusishangae hata sasa ikawa hivyo.
 
Mussa Azan Zungu ni mtu sahihi kabisa kujaza nafasi ya spika wa Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania.

Uzoefu, kukubalika kwa wabunge na busara zake za kuongoza vikao vya bunge vinamfanya awe ni chaguo la wazi kabisa.

View attachment 2073149
Pichani Zungu akiongoza kikao cha bunge kama mwenyekiti.

Sasa uenyekiti wa kamati atamuachia nani??
 
Chaguo la spika ni chaguo la Mwenyekiti wa CCM, tutaenda mbele tutarudi nyuma kama Mwenyekiti wa CCM hatoridhia basi kinachofanywa ni ramli tu.

Nilichogundua mpaka sasa kwa Mwenyekiti wa CCM anataka sura mpya lakini zenye uwezo na uthubutu hivyo tusishangae spika akawa ni mtu tofauti na wanaotajwa tajwa.

Jina la katibu mkuu wa CCM Ndg.Chongolo halikuwahi kufikiriwa hata kidogo lakini ndio akawa hivyo tusishangae hata sasa ikawa hivyo.
Ni kweli kabisa mkuu. Hata Ndugai mwenyewe aliwahi kuwaasa mawaziri punde baada ya kula viapo vyao, alisema, "mama huwa hatabiriki."
 
Binafsi namkubali sana Zungu kwani;
Amejaa hekima na busara
Yuko fair kwa wote
Kichwani yupo smart
Si dhaifu kama aliyeondoka
 
Back
Top Bottom