Nani anaongoza Kanisa Katoliki Tanzania kwa sasa?

Nani anaongoza Kanisa Katoliki Tanzania kwa sasa?

Nilidhani baada ya aliyekuwa Kadinali wa Kanisa la Katoliki Tanzania ambaye pia ni Askofu Jimbo la Daresalaam, Muadhama Askofu Pengo kustaafu na kurithiwa na Askofu Yuda, kwamba mrithi wake angerithi vyeo vyote viwili.

Lakini nimeona sivyo kwani Baba Askoft Yuda anatambuliwa na kuitwa Askofu wa Jimbo kuu Katoliki Daresalaam.

Je, Cheo cha Kadinali hakipo kwa sasa?
Au muundo wa kanisa unasemaje?

Kwa kukujibu shortly ni kwamba kanisa katoliki kiutawala halina kiongozi wa nchi. Ukitoka papa kimamlaka ya duna nzima anayefuata ni Askofu mkuu, Askofu maparoko etc!

Maaskofu wote wanaripoti kwa mkuu wao ambae ni papa.

Hivyo Askofu Niwemugizi ndiye mwisho na mwanzo katika jimbo lake.
 
Massinyori-mwakilishi wa papa anawazidi wote
Mwadhama kadrinali mjumbe katika conclave kikao mhimu cha kumchagua papa
Anahudhuria kikao cha kuchagua papa (conclave) akiwa na yeye ni candidate iwapo tu hajafikisha miaka 75
Kadrinali yoyote akiisha vuka miaka 75 ni mjumbe tu katika uchaguzi wa papa ila yeye siyo candidate(hawezi kuchaguliwa)
Tanzania kwa sasa kwa mjibu wa kanisa katoliki la Roma- mkubwa ni massinyori
Duh, leo tutalishwa matangopori mpaka tukome! Unajua maana ya Monsignor? Kusema kwamba ni mkubwa wa kanisa Katoliki utakuwa hauko sawa. Monsignor ni utambulisho tu wala siyo cheo kwenye mlolongo wa utawala wa kanisa Katoliki.
 
Raisi wa Baraza la Maaskofu Tanzania
Raisi wa Baraza la Maaskofu Tanzania siyo mkuu wa Kanisa Katoliki Kitaifa(hicho cheo hakipo),yeye analo jimbo lake analoliongoza yeye ni kiongozi wa taasisi kama taasisi nje ya taasisi hawezi kuwa na mamlaka yoyote kwenye jimbo lingine lolote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali ya tanzania ndio inayoongozz a roman katolik kuwapa kila kitu
 
Nilidhani baada ya aliyekuwa Kadinali wa Kanisa la Katoliki Tanzania ambaye pia ni Askofu Jimbo la Dar es Salaam, Muadhama Askofu Pengo kustaafu na kurithiwa na Askofu Yuda, kwamba mrithi wake angerithi vyeo vyote viwili.

Lakini nimeona sivyo kwani Baba Askofu Yuda anatambuliwa na kuitwa Askofu wa Jimbo kuu Katoliki Dar es Salaam.

Je, Cheo cha Kadinali hakipo kwa sasa?

Au muundo wa kanisa unasemaje?
Pengo alikuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam na siyo nchi nzima.

Kwa wakatoliki, kila Askofu anaripoti moja kwa moja kwa Papana ana madaraka yake fully ndaniya Jimbo lake na hakuna kuingiliana.
 
Kuhusu kuchagua sehemu yoyote upo sahihi ila kwasasa pengo bado ni Kardinali
Kama kardinali ni cheo basi atakuwa amestaafu pia maana nnavyoelewa Papa anaweza kumchagua kardinali kutoka nchi yoyote sio lazima iwe Tanzania.
 
Hakuna Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Tanzania nzima . Utawala wa KK umegawanyika kimajimbo na unafikia kikomo katika Jimbo husika kama walivyo Wakuu wa Wilaya ( Kikatiba ya Nchi).
 
Massinyori-mwakilishi wa papa anawazidi wote

Mwadhama kadrinali mjumbe katika conclave kikao mhimu cha kumchagua papa

Anahudhuria kikao cha kuchagua papa (conclave) akiwa na yeye ni candidate iwapo tu hajafikisha miaka 75

Kadrinali yoyote akiisha vuka miaka 75 ni mjumbe tu katika uchaguzi wa papa ila yeye siyo candidate(hawezi kuchaguliwa)

Tanzania kwa sasa kwa mjibu wa kanisa katoliki la Roma- mkubwa ni massinyori

Mkuu, unavyosema Monsinyori anawazidi wote sijui ni akina nani hao unaowalinganisha na Monsinyori na siyo Massinyori kama ulivyoandika labda kama unamaanisha jina jingine jipya!
But any way, hebu tuangalie baadhi ya matumizi ya maneno yanayotutatiza wengi, tunapoyasikia na hatujui yanatumikaje;
1.mwandamizi,
2.mwadhama,
3.mhashamu,
4.monsinyori


1.Mwandamizi
Maana yake ni mtu anayetarajiwa kurithi cheo au madaraka fulani. Hivi askofu mwandamizi ni yule atakayechukua cheo au madaraka moja kwa moja baada ya yule aliyepo sasa kutoka katika cheo hicho. Mfano kama ilivyokuwa kwa Askofu YudaThaddeus Ruwa'ichi kabla ya kumrithi Askofu Pengo.

2. Mwadhama
Maana yake "mheshimiwa sana" . Mwadhama hutumika kwa makardinali. Mfano Mwadhama Kardinali Pengo.

3. Mhashamu
Mhashamu maana yake "mheshimiwa".
Hutumika kwa maaskofu wakuu na maaskofu wa kawaida. Mfano Mhashamu Askofu Yuda Thaddeus Ruwa'ichi, n.k

4. Monsinyori
Maana yake ni "kasisi wa kipapa".
Ni cheo ambacho kwa sasa kinatolewa kwa mapadri wenye umri kuanzia miaka 65,(hii ni baada ya mabadiliko yaliyofanywa na Papa Francis, awali kilikuwa kinatolewa kabla ya huo umri) baada ya kufanya kazi ya kutukuka Jimboni mwake au katika baadhi ya ofisi muhimu za Kanisa, - ambapo matumizi ya jina Monsinyori limekuwa ni mila na desturi , kwa mfano katika ofisi ya Askofu, au Mwakilishi Mkuu wa Jimbo au Vika wa jimbo.

Vile vile"monsinyori" hupewa manaibu maaskofu kwa heshima ya nafasi hiyo.
Mfano kuna Monsinyori Deogratias Mbiku wa Jimbo kuu Dar es salaam ambaye ni msaidizi wa Askofu mkuu jimbo kuu Dar es salaam.


N.B: Kwa upande wa mapadre wa kawaida, tunawaita waheshimiwa tu.
 
Yaani
Kwasasa bado ni kardinali na alichokistaafu yeye ni cheo cha uskofu mkuu,hana jimbo ambalo analiongoza. Hivyo anaruhusiwa hadi atakapoteuliwa kardinali mwingine.uko sahihi

Ni km yule kardinal rugambwa km sikosei aliendelea kuwa cardinal hadi umauti hapo pengo alishika uaskofu km ruaichi alivo sasa ila baada ya kufa rugambwa ndio pengo akapewa ukardinal.
 
Upo sahihi kiongozi ! Na ukisoma canon law(sheria za kanisa) kardinali ni mjumbe na mwakilishi ktk baraza lile ambalo huhusika kumchagua Papa huko Roma na pia ni baraza la ushauri kwa papa.Ukipewa Ukardinali automatically unakuwa pia raia wa VATICAN,unapewa hadhi hiyo ya uraia kutokana na nature ya kazi ya Ukardinali.Ukija hapa Tz wengi hudhan Kardinali ndo kiongozi wa kanisa katoliki Tanzania,hapana! Msemaji mkuu wa kanisa katoliki Tz ni raisi aliyechaguliwa na baraza la Maaskofu,mambo mengine yanayofanyika kwa Kardinali hapa Tz ni kumpa tu heshima lakini hana canonical jurisdiction yoyote ile in the eye of the law.
Yaani


Ni km yule kardinal rugambwa km sikosei aliendelea kuwa cardinal hadi umauti hapo pengo alishika uaskofu km ruaichi alivo sasa ila baada ya kufa rugambwa ndio pengo akapewa ukardinal.
 
Nilidhani baada ya aliyekuwa Kadinali wa Kanisa la Katoliki Tanzania ambaye pia ni Askofu Jimbo la Dar es Salaam, Muadhama Askofu Pengo kustaafu na kurithiwa na Askofu Yuda, kwamba mrithi wake angerithi vyeo vyote viwili.

Lakini nimeona sivyo kwani Baba Askofu Yuda anatambuliwa na kuitwa Askofu wa Jimbo kuu Katoliki Dar es Salaam.

Je, Cheo cha Kadinali hakipo kwa sasa?

Au muundo wa kanisa unasemaje?


Hakuna kiongozi wa kanisa katoliki Tanzania, tofauti na wenzetu wa KKKT. Maaskofu wote wa kanisa katoliki wana mamlaka kamili katika majimbo yao na huripoti Roma moja kwa moja kwa Papa ambaye huwateua na ndiye mwenye mamlaka juu yao.
Kiutawala wa kidunia mfano hapa Tanzania unaweza fananisha sema na wakuu wa mikoa. Hakuna mkuu wa wakuu wa mikoa Tanzania, bali wote huripoti kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano. Mkuu wa mkoa mfano DSM hawezi ingilia maamuzi ya mkuu wa mkoa sema Tabora. Anayeweza ni anayemteua ambaye ni Rais.
Ndivyo kwa maaskofu wa kanisa katoliki Tanzania na nchi yoyote ile iwayo
 
Kila askofu ni mtawala mkuu wa jimbo lake bila kujali ni askofu au askofu mkuu...
Anaitwa askofu mkuu kwa kwa kuwa yupo ktk jimbo kuu flani ambalo linaundwa na majimbo kadhaa.... But hii haimaanishi majimbo hayo yapo chini yake la haha. Mfano Songea ni jimbo kuu but haimaanishi askofu mkuu wa Songea anatawala Mpka majimbo ya njombe iringa nk... La haha... Hiki ni cheo ktk utendani but sio utawala.
Na pia haimaanishi askofu wa njombe anawajibika kwa askofu wa Songea...

Kila askofu anawajibika kwa papa bila kujali ni askofu mkuu au ni askofu.
Askofu mkuu wa Dar akienda morogoro Ile fimbo ataigeuzia kwake kwa kuwa wale waumini sio kondooo wake japo jimbo la Moro ni sehemu ya jimbo kuu la dar.
 
Nilidhani baada ya aliyekuwa Kadinali wa Kanisa la Katoliki Tanzania ambaye pia ni Askofu Jimbo la Dar es Salaam, Muadhama Askofu Pengo kustaafu na kurithiwa na Askofu Yuda, kwamba mrithi wake angerithi vyeo vyote viwili.

Lakini nimeona sivyo kwani Baba Askofu Yuda anatambuliwa na kuitwa Askofu wa Jimbo kuu Katoliki Dar es Salaam.

Je, Cheo cha Kadinali hakipo kwa sasa?

Au muundo wa kanisa unasemaje?
Hapa ndipo wakatoliki wengi hukwama,kuwa kadnali haina maana kwamba wewe Ni kiongozi wa kanisa katika nchi,kuwa kadnali unapewa hadhi ya kuwa raia wa Vatican na unapata haki ya kushiriki kumchagua Papa na kushiriki matukio mbali mbali ya kanisa huko Vatican city.Kuna nchi zina makadnali zaidi ya mmoja na wote wana hadhi sawa.Kadnali Pengo hakuwahi kuwa kiongozi mkuu wa kanisa Tanzania,hata hivyo mfumo wa kanisa Katoliki haujajengwa kutegemea mipaka ya nchi bali majimbo.Uongozi wa kimamlaka katika kanisa unaishia kwenye jimbo na ngazi ya juu zaidi ya hapo ni Vatican.Maaskofu wana baraza lao ambalo halina nguvu zaidi ya ushauri linaitwa Baraza la Maaskofu,Kama mkuu wa baraza hili tukamuita ndo kiongozi wa kanisa katika nchi ,basi Kadnali Pengo hakuwahi kushika cheo hiki nakumbuka askofu Ngalerekumtwa ndo alikuwa na cheo hiki sijui kwa Sasa.
 
Back
Top Bottom