Nani anayetajwa na Mwenyekiti wa CCM Mwanza, Dkt. Diallo kwamba ana faili Hospitali ya Akili Milembe?

Iwe ndani au nje ya CCM hamna mfanyabiashara aliyezipenda sera za uchumi za mwendazake, alikuwa ni mwehu kabisa
 

Hao ndio aina ya wagonjwa tunaowahitaji. The self-proclaimed healthy ones who have nothing to show for it are practically dead. They’re just a burden to an already impoverished nation!

Watanzania masikini wangapi wamepoteza maisha kutokana na selfish behavior ya mafisadi? Kibao kikigeuka baadhi yao mafisadi wakafa kwa blood pressure inauma zaidi eh?
 
CHOKOCHOKO ZA MWENYEKITI WA CCM MKOA WA MWANZA NA CHOKOCHOKO ZA MWENYEKITI WA CHADEMA MKOA WA NJOMBE KUHUSU KATIBA MPYA!

Mheshimiwa Anthony Diallo ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza. Alikuwa Mbunge wa Ilemela kupitia CCM na aliwahi pia kuwa Waziri katika Wizara kadhaa! Lakini sasa amekataa 'kunyamala'. Ameamua kuiasi kauli ya Mkuu mmoja wa Mkoa aliyesema kuwa wastaafu wakae kimya kwa kuwa muda wao ulikuwa umekwisha, la sivyo wakisema, watatwangwa! Tarehe 9 Julai 2021, Diallo amenukuliwa na vyombo vya habari akilonga maneno mazito! Anasema kuwa huko nyuma waliwahi kumpa nafasi ya kuongoza nchi mtu aliyewahi kuwa na historia ya kutibiwa Milembe.

Kwa nafasi alizowahi kushika, Diallo alishiriki maamuzi makubwa katika nchi kupitia Ubunge, Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Ujumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM na Ujumbe wa Baraza la Mawaziri. Kwa sababu hiyo kauli zake sio za kupuuzia hata kidogo! Hata hivyo, Diallo hajatuambia ni lini walipitisha uamuzi huo wa kumpa mtu nchi aliyewahi kutibiwa Milembe na wala hajatuambia ni nani mtu huyo aliyepitishwa! Hizi ndizo 'chokochoko' zenye tija kwa Taifa. Lakini inaonekana wakubwa hawapendi kusikia 'maneno yenye kuleta chokochoko'. Je, Diallo atahojiwa kwa kuleta 'chokochoko' hizi kama alivyohojiwa Rose Mayemba yule Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Njombe? Je, Askofu Mwamakula atalazimika kumpazia sauti Diallo kama alivyompazia Mayemba?

Diallo ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza na Mayemba ni Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Njombe. Mmoja anaongoza Chama Tawala ngazi ya Mkoa na mwingine anaongoza Chama cha Upinzani ngazi ya Mkoa. Wote wanafanana kwa kuwa wote wametoa 'kauli zenye kulileta chokochoko' katika Taifa. Tofauti ni kuwa mmoja katumia mitandao ya kijamii na mwingine katumia televisheni. Mmoja aliwekwa chini ya ulinzi na kuhojiwa na Jeshi la Polisi na mwingine ndio kwanza Taifa linatafakari na kuchakata 'chokochoko' zake. Wote wawili wametoa 'chokochoko' zao katika muktadha wa mjadala kuhusu Katiba Mpya.

Pamoja na 'chokochoko' zake, Diallo anakoleza mjadala wa Katiba Mpya! Mjadala huo ndio 'chokochoko' kubwa zaidi. 'Chokochoko' hujadiliwa na hazikimbiwi. Kwa sababu hiyo, sisi Askofu Mwamakula hatutarajii kusikia Diallo anaitwa kuhojiwa kwa sababu ya 'chokochoko' hizo. Kama Chama cha Siasa kinaweza kupitisha jina la mtu mwenye 'rekodi ya kutibiwa Milembe' ili aongoze nchi na vyombo vya usalama vikaridhia au vikashindwa kubaini hilo, basi hiyo ndiyo 'chokochoko' kubwa zaidi inayofaa kujadiliwa sambamba na 'chokochoko' inayohusu Katiba Mpya!

Mwanakondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
 
Bado najiuliza huyo mwanasiasa aliyetajwa na Dr Anthony Diallo kwamba alikuwa na jarada hospitali ya Mirembe ni nani?

Na kwanini mifumo ilimruhusu kugombea?

Je, ni TAL wa Chadema?

Nawasalimu kwa jina la JMT!
Pasueni kichwa ni yupi lkn yupo ndani yenu.

CCM yoweeeee
Itikia yoweeeee
 
Kwani kuwa na file mirembe ni kosa....

Unajua chochote kuhusu mental health?


Ukiwa na jalada Mirembe hospital wewe simply ni Mwendawazimu, wa kiwango gani ?!, hiyo ni issue nyingine.
 
Reactions: BAK
Hilo nalo ni swali?
Hata mwenyewe maruhumu aliwahi kukiri kuwa sometimes mastress na maukichaa yake yanamjia
 
He died for a good reason inatosha, hao unaotaka wanyongwe na mwendazake hiyo kazi tumemuachia aifanye huko alipo.
 
Nimecheka sana wallah! Tundu atabaki kuwa Tundu tuu

Rest well our hero President John Pombe Magufuli


Nimecheka sana wallah! Pombe itabaki kuwa Pombe tuu.

Rest in hell Jpm for the wrongs you did to Tz.
 
Eti aliywahi kuwa mkuu wa nchi labda Yule gavana wa mwisho
 
Kura ambazo zili duplicatiwa , Rais alishasema watu wamkosowe sasa nyie hamtaki mungu wenu ambaye hayupo kwa sasa as asikosolewe.
 
mpumbavu kama wapumbavu wengine...PUMBAVU..... nchi ilimhitaji sana JPM....Mungu anajua kwanini amempa pumziko...
Sema familia yako nchi unaisingizia tu, nani alihitaji kuwa na kiongozi ambaye ukitaka kuongea jambo linalohusu nchi yako ulipaswa kuangalia kwanza watu waliokuzunguka.
 
Pathetic fool, kweli ng'ombe ni ng'ombe tu habadiliki, mlishaanza kuzoea kuongozwa kwa mijeredi.
 
Katika hali ya halisi ukiambiwa umechafua hali ya hewa ina maana umejamba. Kisiasa itakua umeongea jambo la kuwaudhi watu wengi kwenye siasa.

Wenye kumbukumbu watakumbuka enzi ya awamu ya nne iliyokuwa na kashfa nyingi za ufisadi hadi rushwa kuonekana kama ndio njia sahihi kufanikisha kila jambo Anton Dialo alistaajabisha watu kwa tukio moja. Enzi za awamu ya nne ilisemekana alimshitaki waziri wa maliasili enzi hizo kwa JK kwa kutoweza kumpa kitalu cha uwindaji baada ya kumpa dola za kimarekani kiasi fulani. Kuonesha jinsi rushwa ilikua kitu cha kawaida kwa wakubwa kufuatana na Dialo JK alimuamuru waziri huyo kumrudishia Dialo hela zake. Hakuna ushahidi kama JK aliwachukulia hatua yoyote vigogo hao.

Huyo Dialo enzi hiyo ya awamu ya nne alijilimbikizia vyeti feki hadi vya Phd huku kuna shaka ya yeye kufika japo kidato cha nne. Kuna mwandishi mmoja aliandika kitabu kuwaorodhesha watu mashuhuri wenye vyeti feki ambapo Anton Dialo ni mmoja wapo.

Kutokana na hila na kujilimbikizia sifa za uongo Anton Dialo ambaye pia ni mfanya biashara mkubwa akaweza kufikia kua naibu waziri.
Kwa ukweli kauli zake za kinafiki dhidi ya magufuli zimewaudhi wengi. Huyu ni mmojawapo ya watu wamekua wanasitiriwa ndani ya ccm kwa sababu ni mmoja ya wale waliyoigeuza ccm kama kampuni yao binafsi enzi za awamu wa nne.
 
CCM na rushwa ni sawa na moyo na Damu! Yaani ukiondoa damu tu moyo unasimama.

Kwa ujasiri kabisa Diallo anasema vyombo vyake vilishiriki kikamilifu kumfanyia kampeni mgombea wa CCM kwa miadi ya kuja kupewa ahueni "kukumbukwa" sijui kwenye nini huko! Hii ni Rushwa ya wazi kabisa
 
Kwani kaongea jambo gani la maudhi huyo Diallo? funguka mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…