Nani hajui watuhumiwa hupata kibano rumande kusema kweli leo mnamgeuzia kibao Sabaya kwa kua Magufuli kafa?

Nani hajui watuhumiwa hupata kibano rumande kusema kweli leo mnamgeuzia kibao Sabaya kwa kua Magufuli kafa?

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,892
Reaction score
7,780
Nimeona clip za video za baadhi ya watu wanaodai kuteswa na Sabaya. Zaidi ya madai yao hawaelezi wameteswa wapi na kwa sababu gani. Sabaya alikua Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya. Kwenye kamati hiyo wako wakuu wa vyombo vya ulinzi. Clip za Sabaya akienda kukamata au kupeleleza zinaonyesha wakikuta muhalifu anawakabidhi wahusika kisheria kushughulikia.

Usalama kwenye upelelezi hakuna asiejua wanatumia pia mbinu ya kumpiga au kumtesa mshukiwa kupata ushahidi. Kwenye jimbo la Hai Sabaya amepambana na uhalifu mkubwa wa aina mbalimbali na ukwepaji kodi mkubwa. Hili ni jimbo Mbowe kiongozi wa upinzani alitaka kuonekana kama ni mfalme.

Kwa maoni yangu wengi waliyotiwa kibano kwa kushukiwa na uhalifu au fujo za kisiasa wanamuona sabaya ndio adui na mtesi wao wakati wamehusishwa na uvunjaji wa sheria.

Serikali hii ya samia imeliendea kwa papara swala la sabaya kwa kufuata fitna za chuki. Kuna wapinzani wanaamini yeye ni mtu wao aliyekua chini ya magufuli hivyo wamemletea fitna za uongo.
 
SABAYA akiwa kwenye Escalade new model

202721885_4122239771201017_5510743221165187197_n.jpg
 
Kumshangilia huyu Masai mshamba Ni kukosa uzalendo wa Hali ya juu Sana kwa taifa letu...maovu alivyofanya sabaya alipaswa kunyon
Maovu yenyewe kuwazuia kuzalisha na kusambaza gongo kwa industrial scale, kuwazuia kutengeneza na kusambaza fedha bandia etc etc. Yaani chuki zote ni kuzuia ujanja wa kihalifu wa wamangi kufanya kazi.
 
Maovu yenyewe kuwazuia kuzalisha na kusambaza gongo kwa industrial scale, kuwazuia kutengeneza na kusambaza fedha bandia etc etc. Yaani chuki zote ni kuzuia ujanja wa kiahalifu wa wamangi kufanya kazi.
I agree with you. Wazalendo kamwe hawajawahi kubaki salama katikati ya kundi la wabadhirifu na mafisadi. Kitendo cha Ole Sabaya kurejesha nidhamu na ulipaji makini wa kodi Hai na kuwaumbua wafanyabiashara wahujumu-uchumi ndicho kiini cha haya yote anayotendewa ili kumlipiza kisasi.
 
Kumpiga mtuhumiwa ili akiri kosa au ili upate ushahidi ni kinyume na International laws ambazo Tz ni mwanachama wake.

Hivyo kupiga watuhumiwa ni open secret. Yaani inafanyika na watu wanajua inafanyika ila hakuna anayejigamba kwamba anafanya kwakua ni kesi nzuri tu ya kukupa mpaka miaka 30.

So jifunze. Knowledge is out there.
 
Nimeona clip za video za baadhi ya watu wanaodai kuteswa na Sabaya. Zaidi ya madai yao hawaelezi wameteswa wapi na kwa sababu gani. Sabaya alikua Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya. Kwenye kamati hiyo wako wakuu wa vyombo vya ulinzi. Clip za Sabaya akienda kukamata au kupeleleza zinaonyesha wakikuta muhalifu anawakabidhi wahusika kisheria kushughulikia.

Usalama kwenye upelelezi hakuna asiejua wanatumia pia mbinu ya kumpiga au kumtesa mshukiwa kupata ushahidi. Kwenye jimbo la Hai Sabaya amepambana na uhalifu mkubwa wa aina mbalimbali na ukwepaji kodi mkubwa. Hili ni jimbo Mbowe kiongozi wa upinzani alitaka kuonekana kama ni mfalme.

Kwa maoni yangu wengi waliyotiwa kibano kwa kushukiwa na uhalifu au fujo za kisiasa wanamuona sabaya ndio adui na mtesi wao wakati wamehusishwa na uvunjaji wa sheria.

Serikali hii ya samia imeliendea kwa papara swala la sabaya kwa kufuata fitna za chuki. Kuna wapinzani wanaamini yeye ni mtu wao aliyekua chini ya magufuli hivyo wamemletea fitna za uongo.
Duuh! Kweli duniani kuna watu na viatu! Na wewe unajiita eti mtetezi wa haki na sheria!
 
Back
Top Bottom