Mkuu kwanza asante kwa kunikumbusha kwamba jamaa alikiwa akiishi Sweden,
Kiukweli nchi hii haithamini uasisi wa vitu mbalimbali. Hii ndiomaana mpaka leo Tanzania tunashindwa kutengeneza hata soksi. Hebu angalia wazo la Maralia lililoasisiwa na Sugu akitokea USA kipindi hicho likaporwa na kile kijamaa kishenzi cha Clouds fm na kikapata mnuso wa kutosha kwa mawazo ya Sugu. Mpaka leo hii mwenye wazo lile hajanufaika lolote iwe kwa kutambuliwa au kunufaika kipesa. Hivi mtu wa namna hii anaweza kupata moyo wa kuumiza kichwa kutoa mawazo mengine mazuri kwa nchi yake??? Nasikitika sanaq kunamijitu inamdharau Sugu hapa.. laiti wangeijua thamani ya kichwa hiki ndani ya hii nchi wangeziba mibakuri yao..!!
Nikija kwenye Mziki mkuu nadhani kunatofauti kati ya mziki wa Dola Soul, Sugu, Prof J (Hiphop) na mziki Inspector Haroun, Mandojo & Domokaya (Bongofleva) So kibongobongo nikisema Bongofleva nikiijumlisha na Hip-hop, nakua kama nakosea. Lakini nikienda nje ya nchi, Bongofleva inafahamika ni mziki wowote wa Tanzania ulioktk maudhui hayo (ukijumuisha na hiphop) Ni kama jina Bongo, kwazamani ukiwa hapa nchini ukalitamka hili, unamaanisha Dareslaam. Lakini ukiwa nje ya nchi unamaanisha Tanzania..!!!
So maana yangu ilikuwa hapo, kwani inafahamika wazi mziki wa kurap ulipoanza hapa nchini ilikuwa ni hiphop pekee. Baada ya mziki huo kukua ndipo zikaanza R&B na baadaye wakaanza hawa kina Inspector Haroun kuimbaimba. Kuimba kwa Inspector na kwa Sugu ni tofauti, So nilitaka kujua ni nani aliyeanzisha hii Style ya kina Inspector ambayo tunaona mpaka sasa ndiyo iliyoshika soko na kuwatoa kina Kiba Dimpoz, Diamond, kiasi kina Madee wakaimba Hiphop haiuzi..!!!
Wish nimeeleweka mkuu
Matola.
gwijimimi matumbo Deo carleone for more detail.!!
BACK TANGANYIKA