Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wadau;
Kuna tetesi kwamba Ikulu imesita kupeleka jina la PM mteule (ilikuwa liende Dodoma asubuhi hii), badala yake litapelekwa alasiri kwa Spika wa Bunge ambaye ataliwakilisha kwa Wabunge wamuidhinishe kuwa PM!
Kuna habari kwamba Mwandosya, Magufuli, Tibaijuka na Pinda ni majina yaliyokuwa katika meza ya Mheshimiwa Rais. Kulikuwa na tetesi pia kwamba Edward Lowassa na Dr. Harrison Mwakyembe walipigiwa chapuo na makundi mawili tofauti yenye ushawishi katika siasa za Tanzania.
Mwakyembe:
Alionekana ana uwezo, msomi aliyebobea na ambaye CCM wapiga debe wake (kundi linalomtetea) wamekuwa wakishinikiza apewe nyundo kumaliza ufisadi maana wananchi walivutiwa sana na jinsi kamati yake ilivyokuwa mstari wa mbele kushughulikia issue ya UFISADI. Kwa bahati mbaya ameondolewa kwa kuhofia upinzani atakaoupata kutoka kwa wababe wa siasa za bongo wakiongozwa na EL, RA na wafanyabiashara wanaoisaidia CCM
Lowassa:
Anajulikana kwa makeke yake; haiba na mvuto kwa jamii. Ni swahiba wa JK na ana ushawishi mkubwa sana ndani ya CCM. Kinachomkwaza JK kumchukua, japo anatamani sana kumrejesha tena ni ile kashfa ya Richmond! Inasemekana JK anataka kutumia kigezo cha idadi nyingi za kura alizopata jimboni kwake kuonyesha kwa watanzania kuwa bado EL anakubalika. Kuna kundi linaloongozwa na viongozi wastaafau wanaopinga hili kutokea....JK anahofia kwamba akimchukua CCM itamomonyoka!
Pinda:
Ndiye PM kwa sasa, kulingana na hali ya kisiasa ilivyop, jinsi CCM ilivyoaibishwa kwenye uchaguzi JK anaona Pinda si mtu wa aina anayoitaka pale. Anadhani Pinda ni muoga na mkimya sana, anataka mchapakazi, anayeogopewa na mwenye ushawishi katika siasa za Bongo! Kitendo cha PM kulia bungeni, kudeclare kwamba anawaogopa mafisadi nk vinamfanya JK akose imani na Pinda. Inasemekana pia kwamba wakati wa kampeni za urais Pinda yeye hakujishughulisha kukisaidia chama, aliamua kukaa pembeni kutokujihusisha na uchakachuaji, kitu ambacho JK anakiona kama ni usaliti! Kinachomfanya aendelee kumfikiria ni kwamba kama atamtosa sasa ina maana ataongeza ma-ex PM, itakuwa ni kama kuongeza mzigo wa bajetio ya serikali, ameshauriwa aendelee naye hadi 2015 ambapo Pinda mwenyewe atastaafu kwa hiari!
Mwandosya:
Vyanzo vyetu vinadai kwamba Mark Mwandonsya hana ushawishi kwa baadhi ya vigogo wa chama chake, na kwa wananchi. Washauri wa JK wameona kumpa nyundo huyo kutadhoofisha makali ya Serikali na kumuongezea mzigo JK....kitu ambacho kitaexpose weaknesses za president....
Tibaijuka:
Hadi sasa anaongoza katika list, JK anataka kumpa nyundo mama huyu nguli amabaye ameonyesha ukomavu wa kisiasa na mwenye upeoo mkubwa sana katika anga za kimataifa! Kundi kubwa la vigogo wa Chama wanamtaka mama huyu amabaye anakubalika sana pia katika maeneo ya maziwa makuu. Inasemekana JK anatatizwa na kitu kimoja tu...tayari Dr. Asha Rose Migiiro ametajwa na ameshaombwa kuja kuomba urais kupitia CCM (2015) na tayari ameonyesha nia;sasa endapo PM akiwa Tibaijuka itakuwa vigumu kwa Rais na PM wake wote kuwa wanawake 2015!! Mbaya zaidi inasemekana pia Tibaijuka ana mpango wa kuomba kiti cha urais 2015!! Kwa taarifa tu ni kwamba uamauzi wa Dr Migiro ndiyo utaamua kama Tibaijuka apewe u-PM au la! Endapo atakuwa PM ina maana Dr. Migiro hatarejea kugombea 2015...ili kumpisha Tibaijuka abanjuke na upresidaa!!
Magufuli:
JK, washauri wake, CCM na wapinzani hawana hoja against huyu jamaa. Kila mmoja anajua kwamba ni mchapakazi, msomi na hana woga! Anakubalika sana na wananchi na upande wa wapinzani pia. JK anafahamu kwamba jamaa ni jembe na akimpa mpini basi chombo kitakaa mrama! TAtizo ni moja; JK anaogopa kufunikwa na Magufuli na inasemekana ana bifu naye binafsi.! Pia mafisadi wanahofia akipewa u-PM itakuwa mwisho wa wao kuichezea nchi hii, na mawaziri wanamuogopa, inasemekana kuna njama zinafanyika aondolewe hata kwenye baraza la mawaziri!! Tatizop wanajua wananchi watapiga kelele na itakuwa aibu kwao....Uwezekano wa yeye kupata u-PM ni endapo tu kama mama Migiro ataendeleza msimamo wake wa kuwania urais 2015.....
Tusubiri tuone
Kwan inji hii ilipo sasa, mtu aina ya Magufuli ndio anatufaa kama choice ni kwa hao wawili. Mambo yakinyooka then unaweza kumpa mama Tibaijuka.Tunahitaji mtu anayesema spoon spoon na sio kuzuga, pia some kind of a dictator!MAGUFULI ni bomba zaidi.
Vuai kapewa uwaziri jana na Dr. Shein - jaribu tena jina lingine!
Hawa wasomi wetu wanaganga njaa tu. Huyu mama kwa level na exposure aliyonayo sikumtegemea kwamba angekuja kugombea ubunge ili angalau apate nafasi kwenye ufalme wa JK (apewe uwaziri). Hii yote inaelezea vacuum iliyopo kwa wanazuoni wetu. Si wabunifu na kazi pekee wanayoiona ya kuwaingizia kipato kirahisi ni ya kuingia kwenye siasa.
This is too low, angeweza kuanzisha taasisi ambayo ingewasaidia watanzania kuondokana na makazi duni na kuwapa elimu ya kujitegemea.
Mbaya zaidi ameingia kwenye chama kile kile cha 'business as usual' CCM!!
Binafsi namwona anafanana kwa kila kitu na kina Getrude Mongella, Mch. Lwakatare, Margareth Sitta, Batilda Buriani, Salma Kikwete, Vicky Kamata, Nakaaya Sumari, Sophia Simba, na waganga njaa wengine wengi. Sioni mwenye majibu sahihi na mbinu za kisayansi za kuwakomboa watanzania kutoka kwenye lindi la umasikini!!
Huyu alikuwa na bifu na JK hawezi pewa uwaziri mkuu..hapo akipewa magufuli ndo mawaziri watajua nini maana ya kuwa waziri...yaani huyo hana longolongo ni kunyosha mstari
Pinda amepita bila kupingwa hivyo ni mwakilishi wa Jimbo. Anna Tibaijuka naye si alipita bila kupingwa, tofauti iko wapi.
Habari kutoka Dodoma zinasema kuwa kati ya Tibaijuka na Magufuli mmojawapo atateuliwa kuwa Waziri Mkuu. Awali kulikuwa na candidates watatu mezani kwa Kikwete; akiwemo Mwandosya, ambaye sasa jina lake limeondolewa.
Akitambua bayana kuwa serikali yake haina haiba wala mvuto wa kutosha kuungwa mkono na wananchi, Kikwete amesema anataka waziri Mkuu "kukuru-kakara" atakayeweza kuburuza hybrid policy katika kilimo, viwanda (manufacturing) kwa ajili ya kuleta impact katika ajira. Huu ni mkakati wa ku-mobilize vijana amabo wanaonekana kuitupa mkono CCM, hasa kutokana na uzoefu wa CCm kutoungwa mkono na vijana wengi wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2010.
Nwasilisha. Tuendelee kutega masikio yetu.
wazee wala msihangaike kupiga ramli Pinda anaendelea kama kawa kutokana na kukwepa garama.
ni ngumu sana kumtoa pinda wakati hajafanya mistake yeyote pia itakua mzigo kwa serikali kuwahudumia mawaziri wakuu wastaafu walioko mtaani kwa sasa.
wakati kikwete anaingia madarakani magofuli na mwandosya walikua ndo pendekezo but kikwete akawakataa kutokana na urafiki wake na lowasa na kama mnakumbuka siku ile ya kupeleka jina bungeni magufuli alianguka na kuzimia gafla so hata sababu hazikuwekwa wazi.
Kwa hiyo magofuli mkwere hawezi kumweka kwa sasa itakua aibu.
Lipi bora, kumhudumia huyo Pinda kama waziri mkuu mstaafu au kuendelea kua na serikali iliyolala?? Tunahitaji kichwa kama cha Magufuli kikae pale juu kiamshe watu...Mawaziri wote watashika adabu, wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, akishika Magufuli wataomba kuacha kazi, wamezoea starehe, Ila Magufuli basi akikosa ni bora japo wamtupe Mambo ya Ndani, au wamrudishe kwenye wizara yake ya miundombinu kazi iishe!
kuna uwezekano akawa Pr Maji Marefu ccm si mnawajua vyema