Elections 2010 Nani kuukwaa uwaziri mkuu?

Elections 2010 Nani kuukwaa uwaziri mkuu?

Status
Not open for further replies.
Waungwana waziri mkuu jina halijabadilika Mizengo Peter Kayanza Pinda ndiye waziri mkuu kwa miaka mingine mitano, source ni za kuaminika
 
A serious gvt will do a serious analysis for the quality output, i.e. best PM for the good of Tanzanians. The opposite is also true.
 
Wadau;

Kuna tetesi kwamba Ikulu imesita kupeleka jina la PM mteule (ilikuwa liende Dodoma asubuhi hii), badala yake litapelekwa alasiri kwa Spika wa Bunge ambaye ataliwakilisha kwa Wabunge wamuidhinishe kuwa PM!

Kuna habari kwamba Mwandosya, Magufuli, Tibaijuka na Pinda ni majina yaliyokuwa katika meza ya Mheshimiwa Rais. Kulikuwa na tetesi pia kwamba Edward Lowassa na Dr. Harrison Mwakyembe walipigiwa chapuo na makundi mawili tofauti yenye ushawishi katika siasa za Tanzania.

Mwakyembe:
Alionekana ana uwezo, msomi aliyebobea na ambaye CCM wapiga debe wake (kundi linalomtetea) wamekuwa wakishinikiza apewe nyundo kumaliza ufisadi maana wananchi walivutiwa sana na jinsi kamati yake ilivyokuwa mstari wa mbele kushughulikia issue ya UFISADI. Kwa bahati mbaya ameondolewa kwa kuhofia upinzani atakaoupata kutoka kwa wababe wa siasa za bongo wakiongozwa na EL, RA na wafanyabiashara wanaoisaidia CCM

Lowassa:
Anajulikana kwa makeke yake; haiba na mvuto kwa jamii. Ni swahiba wa JK na ana ushawishi mkubwa sana ndani ya CCM. Kinachomkwaza JK kumchukua, japo anatamani sana kumrejesha tena ni ile kashfa ya Richmond! Inasemekana JK anataka kutumia kigezo cha idadi nyingi za kura alizopata jimboni kwake kuonyesha kwa watanzania kuwa bado EL anakubalika. Kuna kundi linaloongozwa na viongozi wastaafau wanaopinga hili kutokea....JK anahofia kwamba akimchukua CCM itamomonyoka!

Pinda:
Ndiye PM kwa sasa, kulingana na hali ya kisiasa ilivyop, jinsi CCM ilivyoaibishwa kwenye uchaguzi JK anaona Pinda si mtu wa aina anayoitaka pale. Anadhani Pinda ni muoga na mkimya sana, anataka mchapakazi, anayeogopewa na mwenye ushawishi katika siasa za Bongo! Kitendo cha PM kulia bungeni, kudeclare kwamba anawaogopa mafisadi nk vinamfanya JK akose imani na Pinda. Inasemekana pia kwamba wakati wa kampeni za urais Pinda yeye hakujishughulisha kukisaidia chama, aliamua kukaa pembeni kutokujihusisha na uchakachuaji, kitu ambacho JK anakiona kama ni usaliti! Kinachomfanya aendelee kumfikiria ni kwamba kama atamtosa sasa ina maana ataongeza ma-ex PM, itakuwa ni kama kuongeza mzigo wa bajetio ya serikali, ameshauriwa aendelee naye hadi 2015 ambapo Pinda mwenyewe atastaafu kwa hiari!

Mwandosya:
Vyanzo vyetu vinadai kwamba Mark Mwandonsya hana ushawishi kwa baadhi ya vigogo wa chama chake, na kwa wananchi. Washauri wa JK wameona kumpa nyundo huyo kutadhoofisha makali ya Serikali na kumuongezea mzigo JK....kitu ambacho kitaexpose weaknesses za president....

Tibaijuka:
Hadi sasa anaongoza katika list, JK anataka kumpa nyundo mama huyu nguli amabaye ameonyesha ukomavu wa kisiasa na mwenye upeoo mkubwa sana katika anga za kimataifa! Kundi kubwa la vigogo wa Chama wanamtaka mama huyu amabaye anakubalika sana pia katika maeneo ya maziwa makuu. Inasemekana JK anatatizwa na kitu kimoja tu...tayari Dr. Asha Rose Migiiro ametajwa na ameshaombwa kuja kuomba urais kupitia CCM (2015) na tayari ameonyesha nia;sasa endapo PM akiwa Tibaijuka itakuwa vigumu kwa Rais na PM wake wote kuwa wanawake 2015!! Mbaya zaidi inasemekana pia Tibaijuka ana mpango wa kuomba kiti cha urais 2015!! Kwa taarifa tu ni kwamba uamauzi wa Dr Migiro ndiyo utaamua kama Tibaijuka apewe u-PM au la! Endapo atakuwa PM ina maana Dr. Migiro hatarejea kugombea 2015...ili kumpisha Tibaijuka abanjuke na upresidaa!!

Magufuli:
JK, washauri wake, CCM na wapinzani hawana hoja against huyu jamaa. Kila mmoja anajua kwamba ni mchapakazi, msomi na hana woga! Anakubalika sana na wananchi na upande wa wapinzani pia. JK anafahamu kwamba jamaa ni jembe na akimpa mpini basi chombo kitakaa mrama! TAtizo ni moja; JK anaogopa kufunikwa na Magufuli na inasemekana ana bifu naye binafsi.! Pia mafisadi wanahofia akipewa u-PM itakuwa mwisho wa wao kuichezea nchi hii, na mawaziri wanamuogopa, inasemekana kuna njama zinafanyika aondolewe hata kwenye baraza la mawaziri!! Tatizop wanajua wananchi watapiga kelele na itakuwa aibu kwao....Uwezekano wa yeye kupata u-PM ni endapo tu kama mama Migiro ataendeleza msimamo wake wa kuwania urais 2015.....

Tusubiri tuone

Mizengo Pinda ana nafasi kubwa ya kurudishiwa u-PM ingawa kitendo cha kuchelewesha jina la PM bungeni kinaacha maswali mengi zaidi.
 
MAGUFULI ni bomba zaidi.
Kwan inji hii ilipo sasa, mtu aina ya Magufuli ndio anatufaa kama choice ni kwa hao wawili. Mambo yakinyooka then unaweza kumpa mama Tibaijuka.Tunahitaji mtu anayesema spoon spoon na sio kuzuga, pia some kind of a dictator!
 
Nionavyo mimi, uongozi wa juu tanzania ni mzigo mkubwa sana kwa walipa kodi, especially baada ya mabwana wakubwa hao kujihalilishia maslahi makubwa wawapo madarakani, na mafao ya makubwa mno wanaopotoka madarakani, achilia mbali yale wanayoiba. Kibaya zaidi wote huwa wana sifa hizi:

1. Hawana uzalendo wa kweli
2. Hawana uthubutu wa kukemea,kushauri na hata kupingana na wakubwa na hata ikibidi wajiuzulu kwa kukataa kushinikizwa kufanya maamuzi yanayowaumiza walipa kodi.
3. Wamejaa unafiki na kazi zao ni kusoma tu hotuba walizoandaliwa.

Mfano; ni nani mwenye ubavu wa kumkosoa, kumpinga rais endapo atatenda au ataenda kinyume na taratibu?? Kazi hiyo inafanywa na walio nje tu,especially wapinzani.

Kwa mantiki hiyo sioni sababu ya kuumiza kichwa kutafuta waziri mkuu mwingine, cha msingi hapo ni kulipungizia taifa hili limzigo la kuendelea kulea vigogo lukuki ambao wamepata kulitumikia taifa hili, na ndio maana ningekuwa na uwezo wa kushauri, nimemshauri kikwete amrudishe huyu mizengo pinda kwenye nafasi aliyoishika kwa miaka hiyo mitatu.kinyume chake tutaongeza tu idadi ya mawaziri wakuu wastaafu bila sababu ya msingi.
 
Hawa wasomi wetu wanaganga njaa tu. Huyu mama kwa level na exposure aliyonayo sikumtegemea kwamba angekuja kugombea ubunge ili angalau apate nafasi kwenye ufalme wa JK (apewe uwaziri). Hii yote inaelezea vacuum iliyopo kwa wanazuoni wetu. Si wabunifu na kazi pekee wanayoiona ya kuwaingizia kipato kirahisi ni ya kuingia kwenye siasa.

This is too low, angeweza kuanzisha taasisi ambayo ingewasaidia watanzania kuondokana na makazi duni na kuwapa elimu ya kujitegemea.

Mbaya zaidi ameingia kwenye chama kile kile cha 'business as usual' CCM!!

Binafsi namwona anafanana kwa kila kitu na kina Getrude Mongella, Mch. Lwakatare, Margareth Sitta, Batilda Buriani, Salma Kikwete, Vicky Kamata, Nakaaya Sumari, Sophia Simba, na waganga njaa wengine wengi. Sioni mwenye majibu sahihi na mbinu za kisayansi za kuwakomboa watanzania kutoka kwenye lindi la umasikini!!

Pamoja na mapungufu ya wasomi wetu lakini jamani tukubali kuwa si wakati wote hao wasomi wanaganga njaa. Kwamfano kwenye project planning and mangement hasa kuna assumptions unazotakiwa kuziweka ili kurealize out put; one is political will. Sasa msomi yeyote yule anayetaka kuleta effective change lazima ahakikishe anakuwa na political influence kwenye constitutional level otherwise nguvu yake inaweza potea bure na kuonekana hafai zaidi. Tunawashangaa wasomi wenye hiyo opportunity na bado wakaonyesha kushindwa!

Mm huyu mama nakumbuka alikuwa anataka kufanya kitu kwa taifa hili lakini somehow somewhere akawa frustrated na hatimaye kujikuta akienda nje. Pengine wakati ule alijifunza kitu na this time akaamua kuja katika sura inayokubalika zaidi kisiasa ili atimize kile ambacho alikitamani kukifanya wakati huo; sina uhakika najaribu kumuelewa kwanini akagombee ubunge wakati status yake ni zaidi ya hiyo? Mimi will wait to see to prove my hypothesis kwasababu by then alini aspire sana na mambo ya BAWATA ambayo ili promote sana vijana wakike.

Like wise for Batilda Burian wengi wetu tumeona jinsi gani ameweza kuonyesha jinsi gani anauwezo wakufanya kitu kizuri if at all she would have been independent in mind. Tatizo naliona nikukosa confidence na kusimama kama yy na hivyo kuhusishwa na watu wengine ambao hawakubaliki kijamii (Maoni binafsi si lazima niwe sahihi).

As a gender activist ningependa kuwapongeza wamama wote waliothubutu na kusimama kwa miguu yao nakushinda bila kuhusishwa na huruma za watu wengine kuwabeba and for this case my sincere congrats to Halima James Mdee na wengine nisio wafahamu kama wapo; mazingira ya kugombea kwake yalikuwa magumu zaidi ya wanawake wengine wote walioshinda Ubunge kwani kuwa upinzani pekee ilitosha kumnyima confidence ya kusimama na kushinda vikwazo vyote vya gender issues na political monopoly iliyopo nchini mwetu.
 
Pinda amepita bila kupingwa hivyo ni mwakilishi wa Jimbo. Anna Tibaijuka naye si alipita bila kupingwa, tofauti iko wapi.

Achana naye huyu jamaa naona anajikanyaga!nafikiri ana ajenda ya siri na huyu mama!hivi huyu mama mbona mnampromoti sana?amelifanyia nini hili taifa?au kufanya kwake kazi umoja wa mataifa?au huo usomi wake?Kweli nimeamini watanzania tuna papala sana!!
 
Habari kutoka Dodoma zinasema kuwa kati ya Tibaijuka na Magufuli mmojawapo atateuliwa kuwa Waziri Mkuu. Awali kulikuwa na candidates watatu mezani kwa Kikwete; akiwemo Mwandosya, ambaye sasa jina lake limeondolewa.
Akitambua bayana kuwa serikali yake haina haiba wala mvuto wa kutosha kuungwa mkono na wananchi, Kikwete amesema anataka waziri Mkuu "kukuru-kakara" atakayeweza kuburuza hybrid policy katika kilimo, viwanda (manufacturing) kwa ajili ya kuleta impact katika ajira. Huu ni mkakati wa ku-mobilize vijana amabo wanaonekana kuitupa mkono CCM, hasa kutokana na uzoefu wa CCm kutoungwa mkono na vijana wengi wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2010.
Nwasilisha. Tuendelee kutega masikio yetu.

... kwani the real presidaa (RA) anataka nani awe PM?
 
wazee wala msihangaike kupiga ramli Pinda anaendelea kama kawa kutokana na kukwepa garama.
ni ngumu sana kumtoa pinda wakati hajafanya mistake yeyote pia itakua mzigo kwa serikali kuwahudumia mawaziri wakuu wastaafu walioko mtaani kwa sasa.
wakati kikwete anaingia madarakani magofuli na mwandosya walikua ndo pendekezo but kikwete akawakataa kutokana na urafiki wake na lowasa na kama mnakumbuka siku ile ya kupeleka jina bungeni magufuli alianguka na kuzimia gafla so hata sababu hazikuwekwa wazi.
Kwa hiyo magofuli mkwere hawezi kumweka kwa sasa itakua aibu.

Lipi bora, kumhudumia huyo Pinda kama waziri mkuu mstaafu au kuendelea kua na serikali iliyolala?? Tunahitaji kichwa kama cha Magufuli kikae pale juu kiamshe watu...Mawaziri wote watashika adabu, wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, akishika Magufuli wataomba kuacha kazi, wamezoea starehe, Ila Magufuli basi akikosa ni bora japo wamtupe Mambo ya Ndani, au wamrudishe kwenye wizara yake ya miundombinu kazi iishe!
 
pinda hakumkampenia jk ndo maana jk ana mihasira

mtotot wa mkulima
 
Lipi bora, kumhudumia huyo Pinda kama waziri mkuu mstaafu au kuendelea kua na serikali iliyolala?? Tunahitaji kichwa kama cha Magufuli kikae pale juu kiamshe watu...Mawaziri wote watashika adabu, wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, akishika Magufuli wataomba kuacha kazi, wamezoea starehe, Ila Magufuli basi akikosa ni bora japo wamtupe Mambo ya Ndani, au wamrudishe kwenye wizara yake ya miundombinu kazi iishe!

Wewe usijidanganye CCM wote wamelala hakuna mtu ambaye ana nafuu, Ila Nyerere aliyetangulia mbele ya haki wengine wote ni mafisadi, Kwa sababu wewe kama siyo mwizi kwa nini uanze kumficha na kuwatetea wezi. Tena bora ya Mwakyembe kuliko huyu magufuli mnayemtaja.
 
Sioni umuhimu wa kuwa na Waziri Mkuu kwenye serikali yenye rais tayari. Nafikiri huu ni mfumo mbovu unaochangia wingi wa gharama kwa serikali pia, na ni dalili pia kwamba marais wetu hawajitumi kama inavyotarajiwa kwa kutegemea waziri mkuu ambaye ndio mtendaji mkuu wa serikali....kwanini rais mwenyewe asiwe mtendaji mkuu?! Kazi hasa ya rais ni nini ukitofautisha na wazir1 mkuu?! For me, in many ways rais wa Tanzania anakuwa kama ceremonial leader tu ambaye hana active function in a daily life of Tanzanians....labda ndio maana JK anatumia nafasi kutalii muda wote.
 
waziri mkuu is another big surprise...

Makufuli maneno mengi kazi kidogo, tunataka watu chapa kazi kama kina Prof Mbilinyi (sijui aligombania ubunge maskini)
 
Ni gharama kuwatunza mawaziri wakuu. Hivyo mp is likely. Binafsi ningepdelea w/m awe self oriented. Driver.
 
Waziri Mkuu ni Pinda jamani jina halijabadilika
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom