Nani mwenye hali ya kiuchumi kama yangu muda huu? Toa mawazo jinsi ya kujikwamua

Nani mwenye hali ya kiuchumi kama yangu muda huu? Toa mawazo jinsi ya kujikwamua

apollo jr

Member
Joined
Sep 3, 2015
Posts
48
Reaction score
36
Habari wana JF,

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 26, ni mhitimu wa Shahada ya Electrical & Electronics Engineering. Katika moja ya Chuo Kikuu hapa mjini Dar es Salaam kama ilivyo kawaida ya vijana wengi tukiwa vyuoni hujisahau kuwa kuna kumaliza masomo na kushindwa ku tafakari kukabiliana na maisha baada ya kumaliza chuo madhara yake ndio nayaona sasa.

Akili ilianza kuniijia nilipofika mwaka wa nne wa masomo yangu, nikawa ni mtu wakujiuliza sana inakuwaje nitaendesha maisha baada yakumaliza chuo na ukizingatia uchache wa ajira mtaani, nikawa mtu wa kujifariji muda wote nakusema nitafanya hata kazi ndogo ndogo za wiring installation maisha yataenda. Ilipofika August 2019 nilifanikisha kumaliza masomo yangu sasa hapo ndio ugumu wa maisha nikaanza kuuskilizia haswa haswa , nikiwa ghetto chakula kikaanza kuwa shida, madili yenyewe ya wiring installation yakawa machache kiasi kwamba kutegemea kunihudumia ikawa ngumu,

Nikawa ni mtu wa kuzunguka na barua za internship japo nipate hata hela ya kula tu, napo sikupata siku zikasogea mwenye nyumba nae anataka pesa yake hapo nakumbuka nimezidisha kama miezi mitatu , nilihisi kudata huku na kule nikakutana na mshkaji nikiwa nimesoma nae chuo course moja, akaanza kunipanga kuhusu forex kwa alivyonielezea tu nikajilaumu sana kuchelewa kuijua hii biashara nikauza vitu vyote ghetto kwa hasara nikapata kama 360tsh mwenye nyumba tukagawana nusu hasara nikampa 90tsh.

Mimi ni kati ya watu ambae nilikuwa na diss sana kukaa kwa ndugu ila nikasema siyo kesi kwakuwa nimeijua forex mwezi mmoja tu utanitosha kukusanya mkwanja wakupanga eneo zuri zaidi.

Bhasi kuanzia December nikaanza kukaa kwa ndugu na by January 2020 nikawa nimeingia rasmi kwenye ulimwengu wa FOREX kwa kile kiasi kilichobaki kutoka kwenye mauzo ya vitu vya ghetto ndio nikaanza nao kama mtaji na kujifunza kwa miezi nane mfululizo ni mimi na forex tu nikijipa matumaini nikiona baadhi ya wanufaikaji lakini kila nikijitahidi naishia kuchoma acc nakuanza upya tena kutafuta mtaji

Nimekuja kujitasmini toka January mpaka sasa August hakuna kitu nimefanya hata mia mbovu sina zaidi ya matumaini, Roho inauma sana sana nimefika point najihisi mfadhaiko moyoni, nanikifikiri nipo kwa ndugu umri unakimbia ndio nachanganyikiwa kabisa.

Naombeni mawazo yenu wandugu nianzie wapi ilihali sina mtaji.

Nakaribisha mawazo, maoni ,ushuhuda pia itapendeza Asante.
 
Don't depends single income...... Brother mfano ukijifunza mamb ya website na application kwa knowledge hiyo usingeweza kuingia forex kichwa kichwa...kwa sababu ungejua how things works behinds.... Account ulichoma c kwa sababu hujui kucheza....kwa sababu mfumo upo huo Ili upoteze
...you was trade with AI machine(Computer).... Labda kama una trade account kubwa kama eToro sasa unaanzia na laki 4 au 5 HV...na unapay by master/visa/paya card...hawa brokers wa M-PESA most them are not verified
Mfumo hauko ili wewe upoteze

Ukiona unampoteza Basi juu unatrade against big market movers

Unapaswa utrade kama market movers wanavyofanya ili upate faida consistently

Swali kujiuliza je una ujuzi sahihi wa kufanya hivyo

Kuchora TL ,sijui S&R hakutokupa pesa kamwe

Uzuri wa hii kitu inawachuja wateule from the beginning kabla haijaanza kukupa mafanikio konki .

Yaani hakuna pesa ya bure bure

Halafu kila kitu kwenye internet tatizo kung'amua kipi ndio kipi Ni shida hapo[emoji2]

4 years no the games and still on it [emoji123]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ingia mtaani mkuu, fanya chochote,
Mimi Nina elimu ya sheria lakini nauza Bar,
Halafu sioni Noma wala nini, hata wateja wangu wanalijua hilo.
Hata leo nikipata kazi mahakamani naacha hii kazi naingia mahakamani fresh kabisa.
Aisee nikupe pongezi sana hapa wengi ndipo hushindwa, na wote wenye moyo kama wako na ujasiri walifanikiwa. Mimi nilisoma Uchumi lakini sijawahi kupractise kazi yoyote related na hayo mambo.
 
Kumbuka pia siyo kila kitu ni kwa ajili ya kila mtu namaanisha jipimevizuri huenda Forex is not for you. Watu wengi uwa wanahisi kwakuwa flani kafanikiwa kwa njia hii na mimi nitafanikiwa kwa njia hiyo hiyo, that is not true kuna mambo mengine utashuhudia mwenzako anafanikiwa ila wewe ukjaribu hutofanikiwa kamwe bali utaishia kupoteza muda.

Kwanza tafuta sehemu upate uhakika wa kula then uje utrade ukiwa umetuliza akili, ukitrade huku uko desperate lazima utachoma kila day.
 
Pole sana ila bado una nafasi Mkuu usione aibu omba hata vibarua/saidia fundi huku ukiwa unaGenerate mtaji mdgmdg na kujifunza zaid na zaidi sio forex tu hata biashara nyingine nyingi hutabaki mtu.
Usiache kusali na kumuomba MUNGU.
Asante kwa ushauri mzuri... Mungu nikila kitu kwangu naamini tafanikiwa kujikwamua kutoka hapa nilipo
 
Jifunze skills moja wapo tofauti na hiyo: mfano computer-> website design and development au blogging ..... Billionaire Warren Buffets anasema don't put all eggs in one basket...... Dunia inashift from physical activities to online activities rapidly... Wish you success
Niukwelii mtupu unayosema mkuu, hata mimi naamini hivyo dunia ina shift na hata ninao kaanao mala nyingi wana appriciate what i think. shida nimeshapoteza time nyingi na sina pesa , sasa naanza kuonekana muongeaji tu mkuu
 
Don't depends single income...... Brother mfano ukijifunza mamb ya website na application kwa knowledge hiyo usingeweza kuingia forex kichwa kichwa...kwa sababu ungejua how things works behinds.... Account ulichoma c kwa sababu hujui kucheza....kwa sababu mfumo upo huo Ili upoteze
...you was trade with AI machine(Computer).... Labda kama una trade account kubwa kama eToro sasa unaanzia na laki 4 au 5 HV...na unapay by master/visa/paya card...hawa brokers wa M-PESA most them are not verified
Absolutely true.. mkuu kwa muda wote huo nimejifunza mengi sana ktk industry ya forex, dealers wanatuona retair traders kama soko kweli kwa mtaji mdogo na bad pyschology ni ngumu ku win
 
Mfumo hauko ili wewe upoteze

Ukiona unampoteza Basi juu unatrade against big market movers

Unapaswa utrade kama market movers wanavyofanya ili upate faida consistently

Swali kujiuliza je una ujuzi sahihi wa kufanya hivyo

Kuchora TL ,sijui S&R hakutokupa pesa kamwe

Uzuri wa hii kitu inawachuja wateule from the beginning kabla haijaanza kukupa mafanikio konki .

Yaani hakuna pesa ya bure bure

Halafu kila kitu kwenye internet tatizo kung'amua kipi ndio kipi Ni shida hapo[emoji2]

4 years no the games and still on it [emoji123]

Sent using Jamii Forums mobile app
well say brother, hata mimi sipingi sana kuhusu forex kwa sababu nimeona walio fanikiwa shida kwangu ni mazingira niliyopo hayawezi nivumilia kutokuwa na pesa kwa muda mrefu.... majungu na vimaneno vinafanya hadi naingia na pressure kubwa sokoni, nakama unavoelewa forex haihitaji papara kabisa
 
Ingia mtaani mkuu, fanya chochote,
Mimi Nina elimu ya sheria lakini nauza Bar,
Halafu sioni Noma wala nini, hata wateja wangu wanalijua hilo.
Hata leo nikipata kazi mahakamani naacha hii kazi naingia mahakamani fresh kabisa.
Shujaaa
 
Nothing is mfumo bro ila ni Big market movers hao.

Wanajua Ku switch sanaa market kwasababu wana high financial knowledge.

#YNWA
also they have mandate... to see where retairs place their order so its much easier to move against
 
Kumbuka pia siyo kila kitu ni kwa ajili ya kila mtu namaanisha jipimevizuri huenda Forex is not for you. Watu wengi uwa wanahisi kwakuwa flani kafanikiwa kwa njia hii na mimi nitafanikiwa kwa njia hiyo hiyo, that is not true kuna mambo mengine utashuhudia mwenzako anafanikiwa ila wewe ukjaribu hutofanikiwa kamwe bali utaishia kupoteza muda.

Kwanza tafuta sehemu upate uhakika wa kula then uje utrade ukiwa umetuliza akili, ukitrade huku uko desperate lazima utachoma kila day.
Asante sana mkuu kwa maoni mazuri.
 
Back
Top Bottom