Nani yuko nyuma ya Lissu kwenye hizi chuki wanaoneza kuhusu Uzanzibari na Utanganyika?

Kitu cha msingi cha kujiuliza ni je anayoyasema ni ya kutunga au yapo wazi mtu kujionea kwa macho mchana kweupe?

Kama anaongea kinachoonekana ubaya wake upo wapi?

Na kama anatunga anachosema then wewe ukiwa miongoni mwa watu wachache sana wenye maono ya kuona ubaya wake hebu tuambie basi ubaya wake upo wapi?
 
Wazanzibari hawautaki Muungano.
Watanganyika hawautaki Muungano.
Je, nani hasa mnufaika wa Muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar??????
 
Umeandika ujinga
 

Attachments

  • IMG-20240502-WA0009.jpg
    117 KB · Views: 5
Wewe umelipwa na nani kueneza hii elimu ya ujinga?

Kuwa chama pinzani kwa mujibu wa Katiba pamoja na kuwafungua macho raia kwa kuikosoa Serikali na kuonesha madhambi ya kihalifu yafanywayo na viongozi watawala pamoja na mapungufu yaliyopo kwenye muungano ulofumbiwa macho miaka nenda rudi kwa manufaa ya wachache ndiyo sababu inayoweza kuleta machafuko?

Sasa chimbuko la machafuko hayo itakuwa ni viongozi wa kiserilkali kufanya madhambi au ni yule mtoa taarifa juu ya uhalifu?

Mlishawaona Taifa la waTz ni la wapumbaf sana kiasi cha mtu kushiba kande na kuwabeulia taka taka zako na usione mtu wa kureply ujinga wako.

Tundu Lisu katenda kosa gani la kimsingi lililo kinyume cha sheria za vyama vya upinzani ama jinai?

Mna misemo ya kwamba vyama vya upinzani vikishika dola yatatokea machafuko, sasa watakaoleta machafuko watakaotawala au watakaokosa urua?

Jiandaeni kisaikolojia na kampeni zenu hizi chafu za kipumbaf.
 
Wewe ndio wa kupuuzwa!
 
Msiwe wajinga nyinyi, jibuni hoja zake, walio nyuma ya Lissu ni Watanganyika, kwanini mnataka kumeza Tanganyika kibwege hivyo ?
 

Umeandika upuuzi. Unawatusi watu wenye akili. Ungekuwa na weledi ungeiona hoja ya Lisu kwa weledi kama wote wenye akili timamu walivyoiona.

Hoja ya Lisu imekuwepo tangu enzi za Bunge la chama kimoja. Wakati ule wa azimio la Bunge lililoridhiwa kwa kauli moja kuwa kuwepo na serikali 3, azimio lililotokana na hoja ya wabunge 55, ulikuwa hujazaliwa bado?

Watu wenye mawazo duni kama wewe ndio wanaotufanya tuwe hapa tulipo. Wazanzibari wanalalamika na Watanganyika wanalalamika.

Options zilizobakia za kuufanya Muungano huu uwe na tija au ni kuwa na Serikali moja (nina hakika Wazanzibari hawatakubali) au kuwa na Serikali 3 (Wazanzibari watakubali na Watanganyika watakubali). Muungano wenye Serikali mbili ni upuuzi. Na wafanya maamuzi wasipoamua kutumia akili, wakabakia kwenye unafiki, Muungano huu kuna siku utakufa, na kutatokea uhasama kati ya Tanganyika na Zanzibar. Marekebisho yakifanyika sasa, yatafanyika kwa njia ya maelewano na upendo.
 
Katiba ya Zanzibar hiyooo ndo inamchochea Lissu so shughulikeni nayo.
 
Huyo ni kibaraka wa mabeberu ambaye anatumika kutaka kuvunja muungano wetu adhimu pamoja na kuchochea machafuko hapa nchini, ili hatimaye kuharibu uchumi wetu huu ambao kwa sasa unakua kwa kasi.
 
Yeye kanukuu katiba, kosa lake ni kuelezea uzuri wa katiba ya zanzibari kwa watanganyika wasiojiita watanganyika?
 
Huyo ni kibaraka wa mabeberu ambaye anatumika kutaka kuvunja muungano wetu adhimu pamoja na kuchochea machafuko hapa nchini, ili hatimaye kuharibu uchumi wetu huu ambao kwa sasa unakua kwa kasi.
Hahahaa uchumi gani huo unaokuwa kwa kasi? Huu huu wa serikali kukosa hata pesa ya kuwalipa wastaafu kwa wakati mpaka wanalazimisha kikokotoo?
 
Kosa la Lissu ni nini??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…