Nani yuko nyuma ya Mkataba wa TFF na GSM, kwanini TFF wanazuia usijadiliwe wala kuhojiwa?

Ni wazi kuna jambo la siri linalofichwa lililopo kwenye huo mkataba kati ya TFF na GSM.

Ni wapumbavu pekee watakaolinganisha uwepo wa huo mkataba kati ya TFF na GSM, waone uko sawa na ile mingine ambayo imewahi kuingiwa na vilabu vya mpira kama Azam na TFF.

TFF lazima ituambie ni zipi contents za huo mkataba, sio kuishia kutaja kiasi cha pesa tu bilioni 2, vilabu vya mpira vikiwa kama shareholders wa mpira wetu wana haki ya kujua kilichopo kwenye huo mkataba.

Huwezi kuingia mkataba na TFF kuhusu mpira wa miguu halafu useme ni wa siri ikiwa kuna vilabu vingine vinavyoshiriki ligi yetu, kitendo cha kuzuia wengine wasihoji juu ya kilichomo kwenye huo mkataba ni ujinga wa hali ya juu, udikteta, na upuuzi mkubwa kabisa.

TFF na GSM watambue hili sio taifa la mazuzu wasiojua kuhoji kama wao, na kuwatisha kuwachukulia hatua za kisheria wale watakaohoji, wakati Katiba yetu 1977 imetoa haki ya uhuru wa kutoa maoni kwenye jambo lolote, huo mkataba kati ya TFF na GSM hauwezi kuwa juu ya Katiba yetu Tanzania.
 
Walishajitoa kwenye kudhamini ligi yenu..
Kaangalia Ulaya Betway, Fly Emirates, Sportpesa wanazamini timu zaidi y mbili katika ligi moja na hakuna kelele km hizi..
Uwanjani quality inaonekana hata hvyo Mo hajazuiwa kudhamini timu nyingine
Hiyo mikataba ya hao wote uliowataja sio ya siri, kwanini huu wa TFF na GSM uwe wa siri?
 
Hivi wewe umesoma hiyo taarifa ni ya mwaka gani?
 
Watu wanachanganya iwnership na sponsorship. Kwa mfano kwenye UEFA kampuni hawaruhisiwi kumiliki zaidi ya timu moja kwenye mashindanyai lakini wanaweza kudhamini zaidi ya timu moja.
Kwa mfano kutoka 2006 mpaka sasa Emirates Airlines imekuwa mdgamini wa Arsenal, AC Milan, Benfica. etc bila matatizo yeyote yale. Nashangaa hixi kelele zinatoka wapi msimu huu mbona huko nyuma hazikuwepo?
 
Ni mimi ndio sielewi au? Gsm wanazipa hizo timu pesa kutangaza biashara yao na sio kununua timu. So mkataba sio baina ya TFF na GSM bali ni GSM na hizo timu. ni sawa na kuwauliza TFF mkataba wa Simba na Mbet, utakua ujuha.

Udhamini uliokataliwa ni ule wa timu zote za ligi kuu kuweka nembo ya GSM kwenye jezi ambao TFF walihusika.

Sportpesa ipo kifuani mwa timu 3 ligi kuu lakini hakuna anaehoji, why GSM?. GSM hahusiki na uongozi wowote wa hizo timu, wao ni kutoa pesa kw ajili ya kutangaza bidhaa zao.
 
Wakati ule team hazina wadhamini mlilalamika sana kutafuta wadhamini

Leo shirikisho linawaletea wadhamini bado tena mnapinga
 
Lakini bado huyu Dr hawezi kukuelewa sijui anataka nini?
 
simba waulize kuuzwa kwa simba
 
Hawa wajinga akili kama mapopo tu , tutasema na hawatafanya kitu
 
SA wana Dstv ambayo ni wadhamini huko na pia wana Timu Super sport ila hawawezi kudhamini Timu nyingi kama Bongo ni uongo huo....
 
mambo ya 2021 unajadili leo?
mkuu kulikoni?
 
GSM wako kwajili ya kufurahisha Samia. Ilimradi Samia anafurahia Kila kitu basi hakuna swali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…