Nani zaidi? Simba vs Yanga thread

Nimejaribu kupiga kura kwa Yanga zinagoma. Inawezekana kuna namna nyau wameingilia mtandao!
 
Tushabikie simba kipato kiongezeke,yanga ni ina laana ya imasikini
 
Hapo unaweza kuta waliopiga kula kwa pande zote hawafiki hata hata 25000 ila kuna vigogo wametia mpunga wa kutosha
Mfano mtu mmoja akitoa million tano maanake apo ni idadi ya watu 5000.
Je kwenye timu moja wakitoa watu 20. Tayari gape linakuwa kubwa.
 
Sasa nyie mnataka tuchukue makombe yote? Hili ndilo kombe lenu mlilobakiza msimu huu!
Muwalaumu Azam Media kwa kuileta hii, ukiiangalia kwa undani utagundua inaexpose mambo mengi, sio hela tu. Ndio maana Yanga waliamua kuitisha press juzi wakiwa wakali wamekasirika, ni kwa vile tu wanapokea fedha za udhamini kutoka kwa Azam Media, vinginevyo kwa uelekeo wa mazungumzo yale, wangeweza hata kuwatukana Azam Media, maana jamaa alitokwa povu hadi akawa anagonga meza
 
Ingekuwa hivyo kusingekuwapo uwiano wa kura na fedha. Hao hapo ni wapiga kura
 
Utafiti wangu niliofanya mashabiki wengi wa Yanga ni wanawake,bilashaka kila mtu anajua wanawake ni watu wakupewa siyo watu wakutoa.
 
Nimecheka sana comments za watu humu. Lol.
Tuipigie kura chama letu la wananchi, haiwezekani ndani ya miezi 6 tupate sh. 1.07B kupitia kadi za wananchi, halafu hapa tuburuzwe kirahisi. Lazima kuna hujuma. Yaani hapa naongea huku nagonga meza na mate yanaruka
 
Sio rahisi hivyo,tena vigogo wanatamani watu wasichange ili tuamini bila wao soka haliendi
 
Tuipigie kura chama letu la wananchi, haiwezekani ndani ya miezi 6 tupate sh. 1.07B kupitia kadi za wananchi, halafu hapa tuburuzwe kirahisi. Lazima kuna hujuma. Yaani hapa naongea huku nagonga meza na mate yanaruka
Hahahaaa. Tulipigie tu aisee.

Japo wananchi wana huruma sana aisee yaani wameamua kutuachia hii na bila shaka hili ndo litakuwa kombe letu pekee litakalotufanya tutembee kifua mbele na kufunika makombe yote pale kwa Timu ya Wananchi. Teh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…