Naomba Kikosi kijacho cha Taifa Stars kiteuliwe kwa Kuangalia Uzalendo, Uchungu na Upambaji wa Beki Ibrahim Baka

Naomba Kikosi kijacho cha Taifa Stars kiteuliwe kwa Kuangalia Uzalendo, Uchungu na Upambaji wa Beki Ibrahim Baka

Laiti Wachezaji wote wa Taifa Stars iliyoyaaga Usiku huu Mashindano ya AFCON huko nchini Ivory Coast wangekuwa na Spirit ya Beki Ibrahim Bska nina uhakika Tanzania tusingetolewa mapema hivi.

Kwangu Mimi huyu Beki Ibrahim Baka ndiyo ambaye Watanzania tunatakiwa tumpokee kwa Heshima zote wakirejea kwani ndiyo ameonyesha kweli kuwa amekamilika Kiuzalendo na alienda kweli kuipambania Bendera ya Taifa huko Mashindanoni.

Yanga SC najua nyie ni Watani zangu nikiwa kama mwana Simba SC tukuka Ila hongereni kwa kumuoa huyu Mchezaji tokea akiwa Kwao Kisiwani Zanzibar, Kumlea na Kumtengeneza kupitia Makocha wenu mahiri na hakika Beki Ibrahim Bska ataendelea kuwa Alama bora ya Uzalendo na Upambaji wa Taifa katika Timu ya Taifa ( Taifa Stars ) na GENTAMYCINE mapendekezo kama si sasa basi baadae apewe rasmi Usinga / Unahodha wa Kikosi cha Taifa Stara na Kitamfaa sana na atakitendea Haki kuliko Mafaza na Mabrazameni wengi walioko Kukosini Taifa Stars.

Hongera beki mahiri Ibrahim Baka.
Upo sahihi kabisa maendeleo hayana timu .
 
Acha usinikumbushe Cannavaro, binafsi yule ndio mchezaji wangu bora wa muda wote Yanga.
Sijawahi kumuona mchezaji aliyeipenda Yanga kama yeye! Akifuatiwa na Nsajigwa.
Daah Shadrack Nsajigwa Fuso sijui yuko wapi saivi. Mara ya mwisho nilimuona bench la timu ya Taifa Stars pamoja na Nadir Haroub mwenyewe. Sijui wako wapi hawa jamaa
 
Jamaa angekua na mwili nyumba maskauti wa timu za ulaya ambao wapo afcon kusaka vipaji lazima wangeondoka na jina lake.
Lisandro Martinez (Manchester United), Julien Timber (Arsenal), Jules Kounde (Barcelona) na Nathan Ake (Manchester City) hawa wote ni beki wa kati wanaocheza ktk ligi ngumu kwa level ya juu sana na wana vimo vifupi sana chini ya mita 1.8 yaani 5' 11''.

Nafikiri tatizo la wachezaji wetu hawana football agencies nzuri ambazo zipo well connected na vilabu vya ulaya, kwa uwezo wa baadhi ya wachezaji ukiondoa kasoro pekee ya kutopitia ktk mfumo mzuri wa shule za mpira ila hawakupaswa kuwepo hapa Afrika. Kuna wachezaji wazuri sana ligi za Africa kuliko hata wachezaji walioko ligi za Ulaya kutoka Afrika.
 
Tatizo umri Vincent Abubakar vilabu kibao ulaya vilikuwa vinamtaka ila umri umeenda watu wanakupima kwenye scanner hutoboi umri wa kwenye vyeti washaona wachezaji wanadanganya.
Bacca yupo kwenye umri mzuri tu na ulaya sio lazima aende epl, laliga au bundersliga kuna ligi kama belgium, turkey anaweza akacheza.
 
Lisandro Martinez (Manchester United), Julien Timber (Arsenal), Jules Kounde (Barcelona) na Nathan Ake (Manchester City) hawa wote ni beki wa kati wanaocheza ktk ligi ngumu kwa level ya juu sana na wana vimo vifupi sana chini ya mita 1.8 yaani 5' 11''.

Nafikiri tatizo la wachezaji wetu hawana football agencies nzuri ambazo zipo well connected na vilabu vya ulaya, kwa uwezo wa baadhi ya wachezaji ukiondoa kasoro pekee ya kutopitia ktk mfumo mzuri wa shule za mpira ila hawakupaswa kuwepo hapa Afrika. Kuna wachezaji wazuri sana ligi za Africa kuliko hata wachezaji walioko ligi za Ulaya kutoka Afrika.
Sifa za beki wa kati ya kwanza kabisa uwe mrefu. Ivyo vimo vya wakina canavaro yule wa itary, bucha wa man u n.k aisee technicaly uwe bora sana. Futi 5 kulikaba jitu kama zlatan ibrahimovic sio mchezo.
 
Laiti Wachezaji wote wa Taifa Stars iliyoyaaga Usiku huu Mashindano ya AFCON huko nchini Ivory Coast wangekuwa na Spirit ya Beki Ibrahim Bska nina uhakika Tanzania tusingetolewa mapema hivi.

Kwangu Mimi huyu Beki Ibrahim Baka ndiyo ambaye Watanzania tunatakiwa tumpokee kwa Heshima zote wakirejea kwani ndiyo ameonyesha kweli kuwa amekamilika Kiuzalendo na alienda kweli kuipambania Bendera ya Taifa huko Mashindanoni.

Yanga SC najua nyie ni Watani zangu nikiwa kama mwana Simba SC tukuka Ila hongereni kwa kumuoa huyu Mchezaji tokea akiwa Kwao Kisiwani Zanzibar, Kumlea na Kumtengeneza kupitia Makocha wenu mahiri na hakika Beki Ibrahim Bska ataendelea kuwa Alama bora ya Uzalendo na Upambaji wa Taifa katika Timu ya Taifa ( Taifa Stars ) na GENTAMYCINE mapendekezo kama si sasa basi baadae apewe rasmi Usinga / Unahodha wa Kikosi cha Taifa Stara na Kitamfaa sana na atakitendea Haki kuliko Mafaza na Mabrazameni wengi walioko Kukosini Taifa Stars.

Hongera beki mahiri Ibrahim Baka.
Hakika huyu jamaa ni mpambanaji sana, niliwahi kusikia mwamba ni mjeda! kama kweli huyu jamaa ni mzalendo haswa!

Nmekumbuka nchi ya Korea kusini kama sikosei, wachezaji wote ni wajeda na hiyo ni sheria kwa kila raia lazima upitie hizo mambo! ukiangalia umbambanaji wa ile timu Asian cup ndiyo utaelewa kuuelezea uzalendo vizuri!
 
Fungulia mbwa
Ukimaanisha kuwa GENTAMYCINE niliyefungiwa Jukwaa la Michezo hapa JamiiForums ni Mbwa na kwamba nimefunguliwa.

Ubarikiwe kwa Wewe Binadamu ambaye umeona Mimi ni Mbwa na kama bado kuna Matusi mengine au Kashfa zingine unazo dhidi yangu tafadhali nakuomba uzitioe na Ukisharidhika utaniambia sawa?

Na wala sijakusahau kuwa hata nawe pia kama ilivyokuwa kwa Dr Matola PhD mara kwa mara mlikuwa mkiwaomba Moderators na mpaka JamiiForums Founder Maxence Melo kuwa NISIFUNGULIWE kamwe hili Jukwaa la Michezo kutokana na CHUKI zenu zisizo na Miguu wala Kichwa dhidi yangu.

Nakuacha na maneno Kuntu na Takatifu yaliyoko katika Kitabu cha Yeremia ( Jeremia ) 1:19.

Asante.

Cc: Moderators Cookie, YinYang, Active, Wand and Paw
 
Acha usinikumbushe Cannavaro, binafsi yule ndio mchezaji wangu bora wa muda wote Yanga.
Sijawahi kumuona mchezaji aliyeipenda Yanga kama yeye! Akifuatiwa na Nsajigwa.
Pamoja na pongezi zako zote Kwake ila nasikitika tu kuwa hujafahamu / hujui kuwa Nadir Haroub Cannavaro ni mwana Simba SC lia lia wa Moyoni, kama ambavyo Watu wengi pia hawajui kuwa aliyewahi kuwa Nahodha mwenye Mafanikio na Simba SC Suleiman Matola ( sasa ni Kocha ) ni mwana Yanga SC kindakindaki sema tu Wote hawa Fedha za Yanga na Simba ziliwafanya wawe Wanafiki wa Kiushabiki kwa muda.

Na bahati nzuri wote hawa ni Marafiki zangu wakubwa tokea wakiwa Wachezaji na hata sasa tunakutana maeneo mbalimbali.
 
Pamoja na pongezi zako zote Kwake ila nasikitika tu kuwa hujafahamu / hujui kuwa Nadir Haroub Cannavaro ni mwana Simba SC lia lia wa Moyoni, kama ambavyo Watu wengi pia hawajui kuwa aliyewahi kuwa Nahodha mwenye Mafanikio na Simba SC Suleiman Matola ( sasa ni Kocha ) ni mwana Yanga SC kindakindaki sema tu Wote hawa Fedha za Yanga na Simba ziliwafanya wawe Wanafiki wa Kiushabiki kwa muda.

Na bahati nzuri wote hawa ni Marafiki zangu wakubwa tokea wakiwa Wachezaji na hata sasa tunakutana maeneo mbalimbali.
Regardless!
Mimi najali zaidi kile nilichokiona akikifanya uwanjani kwa mapenzi na uhodari.
 
Back
Top Bottom