Naomba kueleweshwa hii takwimu iliyotolewa na bodi ya ligi kupitia admin wao wa mtandao wa X

Mbona kiswahili chepesi sana hicho na kimenyooka. Nitakufafanulia usjali mjomba.
1. Simba sc = Timu ya mpira ya kariakoo mtaa wa msimbazi Dar.
2. Pekee = Hakuna ingine ya kufananisha nayo
3. Bao = goli
4. Kila mchezo = Michezo yote iliyoshiriki
5. Msimu = sio lisimu la mkononi likuubwa hapana, manaake ni kipindi kilichopangwa kukamilisha michezo kwa mwaka husika.
Nadhani umeelewa sasa
 
Yaani timu iliyo na magoli 59 ndio iwe ndio timu pekee iliyokuwa na wastani wa kufunga goli kila mchezo. Vipi kwa timu iliyokuwa na magoli 63 na 71?
 
Wabongo ndiyo watu wasioelewa pengine dunia nzima..

Hata lugha yao hawaielewi.

Haya kwa Kiingereza wamewatafsiria.

Mmechagua kutowaelewa Bodi ya Ligi. Leteni takwimu zenu zinazoonyesha kuna timu nyingine ilifunga katika kila mchezo.
 
Wabongo ndiyo watu wasioelewa pengine dunia nzima..

Hata lugha yao hawaielewi.
Kwahiyo timu yenye magoli 59 ndio timu pekee iliyokuwa na wastani wa kupata goli kila mechi, vipi timu iliyo na magoli 30? Vipi timu iliyokuwa na magoli 71? Vipi timu iliyokuwa na magoli 63?
 
Yaani timu iliyo na magoli 59 ndio iwe ndio timu pekee iliyokuwa na wastani wa kufunga goli kila mchezo. Vipi kwa timu iliyokuwa na magoli 63 na 71?
Sio wastaani. Tofautisha maana ya wastani na actual performance. Hii ina maana hakuna mchezo wa ligi ambao simba imecheza ikakosa bao. Hata ikitoa droo ni kuanzia 1 -1. Ikifungwa maana itapoteza kwa kupata goli kuanzia moja
 
Kwahiyo timu yenye magoli 59 ndio timu pekee iliyokuwa na wastani wa kupata goli kila mechi, vipi timu iliyo na magoli 30? Vipi timu iliyokuwa na magoli 71? Vipi timu iliyokuwa na magoli 63?
Wewe ni kichwa ngumu. Mwalimu wako alipata kazi ngumu, nashauri aongezewe pensheni.

Hajasema wastani, hiyo umeleta wewe..

Tafsiri nyepesi, katika kila mechi Simba kafunga goli moja. Simba hajatoka suluhu ya 0-0 katika season iliyopita. Wala haijapokea kichapo bila ya kufunga goli.

Unaweza kufunga magoli 71, ila kuna mechi ukatoka tasa. Ama ukafungwa bila ya wewe kupata goli.

Kiswahili ni kigumu namna hiyo?
 
Yaani timu iliyo na magoli 59 ndio iwe ndio timu pekee iliyokuwa na wastani wa kufunga goli kila mchezo. Vipi kwa timu iliyokuwa na magoli 63 na 71?
Kwahiyo timu yenye magoli 59 ndio timu pekee iliyokuwa na wastani wa kupata goli kila mechi, vipi timu iliyo na magoli 30? Vipi timu iliyokuwa na magoli 71? Vipi timu iliyokuwa na magoli 63?
Sio wastani. Imefunga kila mechi. ligi ina mechi 30+ hivyo wao wamefunga kila mechi angalau goli moja. Hata akifungwa anapata goli(1-2 au 1-3). Hawana matokeo ya 0-0. Huyo mwenye 63 au 71 kuna mechi katoka suluhu(0-0) au akifungwa hapati goli(0-1 au 0-2).
 
Kwahiyo timu yenye magoli 59 ndio timu pekee iliyokuwa na wastani wa kupata goli kila mechi, vipi timu iliyo na magoli 30? Vipi timu iliyokuwa na magoli 71? Vipi timu iliyokuwa na magoli 63?
Mkuu ligi ana mechi 30, unaweza kua na magoli 200 lakini ikatokea Kuna Mechi hukufunga goli, na Kuna timu ikawa na goli 30 lakini ikawa umefunga goli Moja Kila mechi, mbona kiswahili chepesi tu
 
Wenye akili kule ni wawili tuu usitegemee aelewe
Kwanzia mwanzo wa post hadi hapa ni wewe na dr. Restart ndio mlioleta kejeli wakati mtu kaomba kueleweshwa. Hakuna binadamu anayeweza kufahamu au kuelewa kila kitu duniani. Ndio maana kuna kitu kinaitwa ufafanuzi. Ila kwavile umesema wenye akili ni wawili naomba nikubaliane na takwimu yako kuwa ni heri wapo wawili kuliko upande wa pili wote ni mbumbumbu
 
Aahaaaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…