Naomba kuelimishwa kama ungekuwa na shamba Hekari 30, ungelima au ungelifanyia shughuli gani?

Naomba kuelimishwa kama ungekuwa na shamba Hekari 30, ungelima au ungelifanyia shughuli gani?

Prakatatumba abaabaabaa

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2022
Posts
1,842
Reaction score
6,087
Nimekuja kwenu kupata elimu kutoka kwa wazoefu,

Mimi ni mtumishi Mwalimu nipo kigoma, kwa mara ya kwanza nilipata shamba Hekari 6 kigoma, nikafikiri cha kufanya nikaona nilime migazi hekari zote sita, migazi ni mti unaotoa mafuta ya mawese, pamoja na mafuta ya mise, mafuta yanayotumika kutengenezea sabuni za gwanji. Miti ya kisasa aina ya tenera inaanza kutoa migazi baada ya miaka 4 mpaka 5.

Nimepata tena Hekari 30 za pamoja, nafikiria kupanda zao la muda mrefu, ulimaji kwa kigoma naona ni mgumu siwezi kulima mahindi au maharage kwa sababu asilimia kubwa wanatumia jembe la mkono, nilipo sijawahi kuona tractor zikifanya kazi, na nguvu kazi ni warundi na gharama ya kulima Hekari 30 naona ni kubwa, nina mawazo mawili, wazo la kwanza nilitaka nilime mkonge au katani Hekari zote 30, pia wazo la pili nilitaka nilime mikorosho.

Swali langu je naweza toa miche ya mikorosho uko kusini na ikakubali vizuri kwa ukanda huu wa kigoma? Au wazo gari unaloliona ni bora ili hii ardhi iwe productive?
 
Nimekuja kwenu kupata elimu kutoka kwa wazoefu,

Mimi ni mtumishi Mwalimu nipo kigoma, kwa mara ya kwanza nilipata shamba Hekari 6 kigoma, nikafikiri cha kufanya nikaona nilime migazi hekari zote sita, migazi ni mti unaotoa mafuta ya mawese, pamoja na mafuta ya mise, mafuta yanayotumika kutengenezea sabuni za gwanji. Miti ya kisasa aina ya tenera inaanza kutoa migazi baada ya miaka 4 mpaka 5.

Nimepata tena Hekari 30 za pamoja, nafikiria kupanda zao la muda mrefu, ulimaji kwa kigoma naona ni mgumu siwezi kulima mahindi au maharage kwa sababu asilimia kubwa wanatumia jembe la mkono, nilipo sijawahi kuona tractor zikifanya kazi, na nguvu kazi ni warundi na gharama ya kulima Hekari 30 naona ni kubwa, nina mawazo mawili, wazo la kwanza nilitaka nilime mkonge au katani Hekari zote 30, pia wazo la pili nilitaka nilime mikorosho.

Swali langu je naweza toa miche ya mikorosho uko kusini na ikakubali vizuri kwa ukanda huu wa kigoma? Au wazo gari unaloliona ni bora ili hii ardhi iwe productive?
Lima migazi mavuno itakuwa Kila mwaka
 
Ningelizungushia liwe ranchi baadhi ya maeneo maeneo mengine nalima.

So pale ambapo sina uwezo wa kulima nalishia mifugo
Una mawazo ambayo niliposoma tu huu uzi nikawaza hivyo
Mifugo ndio mahali Pake kwa hizo heka
Na baadhi atalima mashamba na pia manyasi kwa ajili ya chakula
Natafuta heka hata 50 kwa shughuli kama hii ila sehemu yenye maji
 
Ulinunuwa Shingapi Mkuu
Huko njombe vijijini kuna ekari 100 kwa mtu anayetaka kuwekeza:
1) Ranch ...mifugo anuai ..shamba la mimea ya mifugo, miundombinu supportive nk
2) Kilimo cha miparachichi ya kisasa
3) Kilimo cha Chai (ihudumie vema)
4) Kilimo fasta fasta cha viazi mviringo, njegele nk.
Ekari 600k, zinauzwa zote kwa pamoja.
 
Back
Top Bottom