Naomba kuelimishwa kama ungekuwa na shamba Hekari 30, ungelima au ungelifanyia shughuli gani?

Naomba kuelimishwa kama ungekuwa na shamba Hekari 30, ungelima au ungelifanyia shughuli gani?

Nimekuja kwenu kupata elimu kutoka kwa wazoefu,

Mimi ni mtumishi Mwalimu nipo kigoma, kwa mara ya kwanza nilipata shamba Hekari 6 kigoma, nikafikiri cha kufanya nikaona nilime migazi hekari zote sita, migazi ni mti unaotoa mafuta ya mawese, pamoja na mafuta ya mise, mafuta yanayotumika kutengenezea sabuni za gwanji. Miti ya kisasa aina ya tenera inaanza kutoa migazi baada ya miaka 4 mpaka 5.

Nimepata tena Hekari 30 za pamoja, nafikiria kupanda zao la muda mrefu, ulimaji kwa kigoma naona ni mgumu siwezi kulima mahindi au maharage kwa sababu asilimia kubwa wanatumia jembe la mkono, nilipo sijawahi kuona tractor zikifanya kazi, na nguvu kazi ni warundi na gharama ya kulima Hekari 30 naona ni kubwa, nina mawazo mawili, wazo la kwanza nilitaka nilime mkonge au katani Hekari zote 30, pia wazo la pili nilitaka nilime mikorosho.

Swali langu je naweza toa miche ya mikorosho uko kusini na ikakubali vizuri kwa ukanda huu wa kigoma? Au wazo gari unaloliona ni bora ili hii ardhi iwe productive?
Nafkir wakt unawaza upande nn pia waza hzo changamoto unazkabili vp,,mfano kama hamna tractor na hujawah kuona huon kama ukipambna siku moja hzo nyenzo zkapatkana utakua umefankiwa??
 
Lima citrus, hili wazo sijawahi skia mtu akilishobokea ni kilimo kilichojificha.

Kama Kuna access ya maji kwa urahisi, miti kama limao na ndimu ndio mahala pake.

Tafuta mbegu ya muda mfupi sana na mbolea ya kukuzia, kukubwa maji yawepo.
Haya mazao kukiwa na maji hayana msimu ukichuma maua yanachanua.
 
Endelea na kilimo cha migazi, labda unaweza kuweka na miti ya mbao mfano mikaratusi au cedrella....mifugo inahitaji usimamizi wa karibu, ukicheza tu unapoteza hela.

Unapokuwa kwenye ajira na ikiwa hiyo ajira ndiyo inaendesha maisha yako, hakikisha uwekezaji unaofanya nje ya ajira usiwe ni ule wa kukulazimu kutumia muda mwingi kusimamia kwa kuwa muda huo hutopata unless uwe ni mtoro kazini jambo ambalo siyo zuri....miti ya mbao au migazi inaweza kujiendesha yenyewe wewe ukiwa mbali.
 
Lima citrus, hili wazo sijawahi skia mtu akilishobokea ni kilimo kilichojificha.

Kama Kuna access ya maji kwa urahisi, miti kama limao na ndimu ndio mahala pake.

Tafuta mbegu ya muda mfupi sana na mbolea ya kukuzia, kukubwa maji yawepo.
Haya mazao kukiwa na maji hayana msimu ukichuma maua yanachanua.
Soko la limao lipo?, nafikiri ekari 5-10 nipande coconut.
 
Nimekuja kwenu kupata elimu kutoka kwa wazoefu,

Mimi ni mtumishi Mwalimu nipo kigoma, kwa mara ya kwanza nilipata shamba Hekari 6 kigoma, nikafikiri cha kufanya nikaona nilime migazi hekari zote sita, migazi ni mti unaotoa mafuta ya mawese, pamoja na mafuta ya mise, mafuta yanayotumika kutengenezea sabuni za gwanji. Miti ya kisasa aina ya tenera inaanza kutoa migazi baada ya miaka 4 mpaka 5.

Nimepata tena Hekari 30 za pamoja, nafikiria kupanda zao la muda mrefu, ulimaji kwa kigoma naona ni mgumu siwezi kulima mahindi au maharage kwa sababu asilimia kubwa wanatumia jembe la mkono, nilipo sijawahi kuona tractor zikifanya kazi, na nguvu kazi ni warundi na gharama ya kulima Hekari 30 naona ni kubwa, nina mawazo mawili, wazo la kwanza nilitaka nilime mkonge au katani Hekari zote 30, pia wazo la pili nilitaka nilime mikorosho.

Swali langu je naweza toa miche ya mikorosho uko kusini na ikakubali vizuri kwa ukanda huu wa kigoma? Au wazo gari unaloliona ni bora ili hii ardhi iwe productive?
Kwanini usilime avocado zile maarufu kutoka Burundi maana msimu wake uwa parachichi kwa tz ni chache hivyo kuwa na bei nzuri
 
Back
Top Bottom