Naomba kufahamishwa kuhusu gharama za maisha ndani ya Jiji la Tanga

Masokotz

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2018
Posts
3,713
Reaction score
6,121
Habari za wakati huu,

Ningependa kufahamu kuhusu mji wa Tanga na gharama za maisha. Baadhi ya mambo ningependa kufahamu ni pamoja na maeneo mazuri ya kuishi kwa watu wa kipato cha chini au cha kati, Gharama za kupangisha nyumba, chumba. Gharama za chakula na malazi katika lodges na guest houses, gharama za usafiri wa mjini. Shughuli za kiuchumi za wakazi wa Tanga.

Taarifa zozote zile ambazo zinaweza kumsaidia mtu anayetaka kuhamia Tanga kitalii

Asanteni
 
Jiji la maraha

Wanakwambia waja leo waondoka leo
 
Mzee kama unaenda Tanga kutafuta maisha basi pole sana, sie wenye mji tumekimbia tupo Mbeya ila nikwambie tu Tanga pazuri sana ukienda Tanga mjini kuanzia kule chumba elfu 10 mpaka elfu 20 kina umeme ila cha kawaida ukiitaji chenye rangi singboard ni kuanzia 20 mpaka 30. Tanga hakuna tofauti sana na Dar, kule watu wavivu mzee siyo wachapakazi sana. Maisha yakule magumu kama upo Dar hakuna tofauti saana labda ukaishi vijijin mfano Mkata kwa msisi lakini Tanga mjini, Handeni mjini, Lushoto mjini maisha ni yaleyale kama Dar es saalam, kila lakher.
 
Mji wa Tanga mjini gharama za kuishi ni flat rate yaani gharama za vyumba ni chini sanaa mitaa ya kuishi ni ww uamuzi wako, swala usafiri usihofu baiskeli tu itakutosha.

Mitaa kama ya Chumbageni, Sahare, Nguvumali, binafsi nahisi ni Poa sana
 
😆😆😆 Yaan unasema tng hakuna tofauti na dsm ? Ndugu aacha kumpotosha huyu ndugu, yaan dar na tng ni mbingu na ardhi mzee, dar kumechangamka sana mishe mishe kibao tng hamna kitu mji upo doro, ukitika saa sita mchana kuelekea saa saba maduka yana fungwa kwenda kuswali au muhindi anaenda kupumzika mpaka saa 8 Dar upuuzi huo hakuna.
Tng saa 3 usiku mji kimyaaaa wakati dar iyo saa 3 ndio kuna anza kukucha ....
 
Mkuu Asante. Sehemu salama ya kuishi ni wapi?
 
[emoji1][emoji1][emoji1][emoji119][emoji119][emoji119]

Mimi na majamaa ambao tumekua rika moa wote tumehama tanga.

Nyumbani Kwanjeka kule. Naenda kusalimia tu.
 
Bro maisha popote wasikutishe. Tupo Tanga na mambo yanaenda. Wa Dar wanaanza kurudi mdogo mdogo.
Sehemu salama kwa makazi ni Sahare, Chumbageni, Nguvumali, Kange uzunguni. Ole wako na Magomeni, Kwanjeka au Majengo.
Kula ya kawaida b/f 1000 lunch 1500 dinner 1500.
Usafiri ni daladala 400 boda ya ppl au baiskeli.
Uchumi ni biashara ya chakula (nafaka), matunda, samaki.
Lakini tu ukiingia HUTOKI
 
Hapo mwishoni hapo, hebu mfafanulie vizuri mtoa mada. Kwa nini akiingia tu Jijini Tanga, basi asitarajie tena KUTOKA? Anaweza kuogopa kuja Tanga.
 
Singboard ndio nini tena???

Mwenye ufahamu tueleweshane hebu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…