Naomba kufahamishwa kuhusu "kunde" aina ya ngwara

Naomba kufahamishwa kuhusu "kunde" aina ya ngwara

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
1. Kutahitajika kiasi gani kwa ajili ya kupanda eka 20?

2. Inapatikana wapi mkoani Mwanza au mikoa ya jirani?

๐Ÿ™๐Ÿ™๐Ÿ™
 
1. Kutahitajika kiasi gani kwa ajili ya kupanda eka 20?

2. Inapatikana wapi mkoani Mwanza au mikoa ya jirani?

๐Ÿ™๐Ÿ™๐Ÿ™
Kuhusu upatikanaji zinapatikana Arusha.
MEngine watajibu wengine
 
Zinalimwa sana Magugu,Babati nafikiri Hazina tofauti sana na maharage ...ila Kuna wajuvi watakujibu ...pia tafuta Uzi kuhusu ngwara upo humu Kuna wakulima walitirika vizuri...mwaka jananafikiri
 
Usijali mkuu.
NGwara soko lake kubwa ni Nairobi, wakati wa mavuno wanunuzi toka Nairobi hujaa Arusha
Inaelekea Wakulima wengi wa Tanzania bado "hawajaligundua" hilo zao. Naamini linaweza kustawi katika maeneo mengi ya Tanzania.
 
Unaweza kuyakuta kwenye mighahawa ya nchini Kenya?
Kwenye migahawa sidhani, ila labda iwe mighahawa ya wazawa au wakenya wenyewe.

Hayo maharage nikama chakula chao cha asili, Wewe wataka maharage kiasi gani?

Umejarubu kuangalia hapo arusha, maana nakumbuka kipindi flani niliwahi kuyakuta Soko kuu wanayauza
 
Kwenye migahawa sidhani, ila labda iwe mighahawa ya wazawa au wakenya wenyewe.

Hayo maharage nikama chakula chao cha asili, Wewe wataka maharage kiasi gani?

Umejarubu kuangalia hapo arusha, maana nakumbuka kipindi flani niliwahi kuyakuta Soko kuu wanayauza
Sipo Arusha mkuu. Hata hivyo nimeshaongea na mtu aliyeko Arusha akaniangalizie Soko Kuu Arusha.
 
Upatikanaji wake kwa Sasa umekuwa mgumu maana wakulima wengi hawapandi kutokana na soko lake kuyumba ivyo wameenda kwenye Mbaazi lakini unaweza kuipata maeneo ya Babati, Manyara au Singida

Kuna aina tatu za Ngwara ambazo ni Nyeupe, Nyeusi na langi ya udongo

Ivyo ukiwa kama mkulima inabidi ijue ipi inapendelewa sokoni maana kwa upande wa Singida wanapenda iyo langi ya udongo kuliko Nyeusi

Pia unaweza kuipanda yenyewe ama ukachanganya na Mahindi

Huwa zinapandwa katikati ya msimu maana ukiwai sana huwa zinaharibiwa na mvua
 
Upatikanaji wake kwa Sasa umekuwa mgumu maana wakulima wengi hawapandi kutokana na soko lake kuyumba ivyo wameenda kwenye Mbaazi lakini unaweza kuipata maeneo ya Babati, Manyara au Singida

Kuna aina tatu za Ngwara ambazo ni Nyeupe, Nyeusi na langi ya udongo

Ivyo ukiwa kama mkulima inabidi ijue ipi inapendelewa sokoni maana kwa upande wa Singida wanapenda iyo langi ya udongo kuliko Nyeusi

Pia unaweza kuipanda yenyewe ama ukachanganya na Mahindi

Huwa zinapandwa katikati ya msimu maana ukiwai sana huwa zinaharibiwa na mvua
Nashukuru sana mkuu๐Ÿ™
 
Back
Top Bottom