Naomba kujua Umuhimu na Mantiki ya Rais kusindikizwa na kupokelewa na lundo la Waandamizi akisafiri na akirejea kutoka nje ya nchi

Naomba kujua Umuhimu na Mantiki ya Rais kusindikizwa na kupokelewa na lundo la Waandamizi akisafiri na akirejea kutoka nje ya nchi

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Na je, tunapoelekea Kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru wetu Tanzania utaratibu huu bado una Tija ya Kimaendeleo Kwetu au ni Utaratibu wa Kikoloni ambao kwa sasa unatufanya tuendelee kuonekana Mazuzu Kimataifa?

KEROZENE nasubiri tu Michango yenu.
 
Mtu ukishakuwa mwanasiasa automatically unakuwa zero brain. Kasoro Mbowe tu ndio mwanasiasa ambae ana akili.
Una uhakika kuwa hata Mbowe nae ingetokea angekuwa Rais wa Tanzania huu Utaratibu ambao KEROZENE siioni Aibu wala Uwoga kuuita ni wa Kizuzu nae asingeufuata?

Nasikitika umejibu Kiitikadi zaidi na siyo Kiuhalisia na hili ndilo limekuwa tatizo letu Kubwa Watanzania wengi siku hizi kwa Kupenda Kuhemka kwa Itikadi zetu za Kisiasa na siyo kwa Kufikiri vyema.
 
ni utaratibu na taadhima tuliyorithi toka enzi ya mkoloni tukainasibu kama mfumo wa kuonyesha utii na heshima kwa utawala,.hiyo sio kwa mkuu wa nchi tu, hata mkuu wa mkoa/ mkuu wa wilaya akitoka kwenda kikazi mahali protokali ya mapokezi/kuagana huwa inafanania ..yaani wale wanaowajibika chini ya mamlaka yake huwepo /hupaswa kuwepo.

Inawezekana sana kubadili uwepo wa mlundikano wa wasindikizaji /wapokeaji ila ni jambo la kimfumo ambalo kwa hulka ya watawala waliopo na wataokuja wasipoona haja ya kubadilisha hayo tutaendelea kuliongelea huku mitandaoni. fikiria kuna kipindi hadi vikundi vya ngoma kwaya na brass band vilikuwa vinaenda kuaga na kupokea viongozi wa ndani ya nchi [emoji2][emoji2], haishindikani kupunguza na kuondoa lundo iwapo nia ya dhati ikiwepo.
 
Inasikitisha sana yaani raisi akitoka na kurejea nchini ni rundo la viongozi yaani hadi makamu wa rais anaenda kumpsindikiza na kumpokea kweli ni upuuzi wa kiwango cha lami.....Mi nadhani ingependeza kuwe na mkuu wa wilaya na kamati yake basi.
 
Una uhakika kuwa hata Mbowe nae ingetokea angekuwa Rais wa Tanzania huu Utaratibu ambao KEROZENE siioni Aibu wala Uwoga kuuita ni wa Kizuzu nae asingeufuata?

Nasikitika umejibu Kiitikadi zaidi na siyo Kiuhalisia na hili ndilo limekuwa tatizo letu Kubwa Watanzania wengi siku hizi kwa Kupenda Kuhemka kwa Itikadi zetu za Kisiasa na siyo kwa Kufikiri vyema.
Nimesema tu ukweli mkuu. Mimi sio mchadema lakini kweli Mbowe ni mwanasiasa mwenye busara sana. Mbona nisingesema upinzani wote wana akili?
 
Na je, tunapoelekea Kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru wetu Tanzania utaratibu huu bado una Tija ya Kimaendeleo Kwetu au ni Utaratibu wa Kikoloni ambao kwa sasa unatufanya tuendelee kuonekana Mazuzu Kimataifa?

KEROZENE nasubiri tu Michango yenu.
Hutaki?
 
Inasikitisha sana yaani raisi akitoka na kurejea nchini ni rundo la viongozi yaani hadi makamu wa rais anaenda kumpsindikiza na kumpokea kweli ni upuuzi wa kiwango cha lami.....Mi nadhani ingependeza kuwe na mkuu wa wilaya na kamati yake basi.
Je, tukiitwa ni Mazuzu tutakuwa tunaonewa au tunakosewa? Ni Utaratibu wa Kinafiki ambao nahisi unataka kumuonyesha Mtu fulani kuwa ndiyo Mungu Mtu kwa Watanzania ( Waswahili ) wote.
 
Nimesema tu ukweli mkuu. Mimi sio mchadema lakini kweli Mbowe ni mwanasiasa mwenye busara sana. Mbona nisingesema upinzani wote wana akili?
Unajitahidi mno Kujificha, ila wenye Akili Kubwa kwa Uwasilishaji wako hapa uliojaa Machungu kwa Serikali ya CCM na Mahaba yako kwa Freeman Mbowe unaonyesha kabisa Wewe ni mwana CHADEMA 100% na sijui ni kwanini unaogopa Kujitanabaisha hivyo.
 
Na je, tunapoelekea Kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru wetu Tanzania utaratibu huu bado una Tija ya Kimaendeleo Kwetu au ni Utaratibu wa Kikoloni ambao kwa sasa unatufanya tuendelee kuonekana Mazuzu Kimataifa?

KEROZENE nasubiri tu Michango yenu.
hakuna logic ya viongozi kurundikana airport

inacost muda wa watumishi wa umma na resources za nchi

inasababisha foleni

inatoa watu muhimu ofisini ambao wanasubiriwa watoe maamuzi, wahudumie wananchi n.k n,k

lakini Waafrika hatukulelewa kujifunza, kuheshimu na kutumia logic

tunafanya vitu irrationally, ndio maana hatuendelei.
 
Back
Top Bottom