Naomba kuuliza kuhusu chimbo zuri la kununua mitumba balo za mitumba


Viatu mzunguko wake upo chini ila unapata faida nzuri, tofauti na nguo zinatoka haraka.
 
Too bad una limit ya viewers, anyway I hope nitapata msaada hapa hapa.
Nahitaji kuanza kufanya biashara ya mashuka niwe nanunua belo pale zinakopatikana kwa bei nzuri na supplier wa uhakika (Grade iendane na bei). shuka nazotafuta ni zile za cotton nzito unakuta ndani ziko either pair 2 na foronya nne na king size, na belo lingine lililonipa changamoto kupata ni la nguo za kulalia za kina dada material ya kuteleza mostly zinakuaga pair (hii nilijaribu kumuuliza mtu mmoja instagram huwa anachukua wapi mzigo wake maana ni mzuri ila nikaishia kula block) nimehangaika sana kutafuta na ni biashara ambayo nataka niikomalie ila nakutana na changamoto mbalimbali.
 
Sawa Sawa kabisa. Kwa mitumba kutoa pea ni rarely case. Kipindi robota linafunguliwa inatokeaga kupata nguo zinafanana. Kwa taulo, MASHUKA ni kawaida sabb ni (nguo) ambaz hazina fasheni nyinginyingi. Mara kadhaa nimeona MASHUKA yanayofanan huwaga ni moja (mattrress cover) linapasuliwa katikati. Ni MASHUKA yanayoveshwa kwenye godoro yana'Editiwa'. Hilo linawezekana. Kwa nguo za kulalia wanawake mkuu siufichi. Ile haina baro maalum. Unanunua tu kama POINTA. huyo jamaa kama Ana 'CODE' hizo ujue hafunguo balo anachagua Kwa anaefungua.
USHAURI : Anza na hili la MASHUKA, nunua balo. Kama una wateja wengi ( mtu wa watu) lifungulie nyumbani kwako. Chagua MASHUKA mazuri yote weka pembeni ( Zingatia material/ Ukubwa / mapambo. Nk) then yahesabu. Kisha, hayohayo yatenge Kwa ukubwa na yachuje mpaka upate super quality-ambayo unaweza uza moja hata elf 50), middle quality yawekwe Kwa bei ya elf 30. Pia low quality kadiria alf 15-20.yale ambayo hukuyatenga (Majority side) yahesabu kisha mpe kijana akayanwage barabarani /minadani mwambie auze moja elf 6 ( yakague) yatenge. Mengine mwambie auze elf 4 ( yahesabu pia). Kaa chini fanya mahesabu yako ikiwa yote yatatoka utapatkias gani. Huyu kijana mpe elf 5 Kwa siku na mnunulie chakula cha mchana mpaka uone uuzaji wake.
Robota zote hizo z inauzwa mnazi mmoja. (Nb) fanya tafiti ya bei ya robota kwanza kabla hujaingia mzigoni
 
Kwa kufanya hivyo, kuna kundi la wateja wako hapo umelikata (MAWINGA) ambao wangechagua zile shuka za middle /super quality na kukuacha shuka z kawaida.
Kama una basic knowledge y mitumba utakuw umenielw vizur hapo ( ona pg no. 1)
 

Shukrani sana mkuu nitafanyia kazi huu ushauri
 
nina ilo wazo toka ktambo sana naamini Mungu ataniongoza siku moja wazo litimie
 
Habari za Usiku wakuu,

Naomba Msaada wa Chimbo la wahindi wanaouza Viatu vya Mitumba kwa Jumla yaani kwa Mabello, kule ambapo hata wafanyabiashara wa Karume na Ilala wamekuwa wakitoa mzigo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…