Naomba msaada juu ya jambo hili la ajabu ambalo limetuchanganya kama familia

Naomba msaada juu ya jambo hili la ajabu ambalo limetuchanganya kama familia

Niko hapa nijuavyo mimi mtu akifa namba yake haipaswi kutumika na mwanafamilia yeyote tena! Hata mimi mtu akishakufa na nanba yake naifuta kwenye phone book yangu
Nina kisa kinachofanana na hicho kidogo..
Kuna bibi mmoja tulifahamiana katika mazingira ambayo nisingependa kuyaweka wazi hapa, nikawa na ukaribu naye kiasi cha kuniita mjukuu wake aliyepewa na Mungu .. Nikiri wazi alinisaidia kwa mengi sana na mimi pia hivyohivyo
Namba yake ya simu nimeikariri hata sasa! Lakini alipofariki 2012 niliifuta kwenye phone book yangu
Sasa mwezi uliopita ile namba ikanipigia.. Nikastuka sana lakini nikaipokea hakukuwa na majibu upande wa pili.. Nikiipiga ni kama inapokelewa lakini hakuna sauti.. Hiyo hali iliendelea karibia wiki nzima mpaka nilipoamua kuiblock
Mshana na wewe unamaruweruwe,🤔
 
Kama kichwa cha habari kinavyoeleza, ni jambo lililotushtua kama familia kutokana na uajabu wake.

Ipo hivi, siku ya juzi tar 19 majira ya saa sita kasoro usiku nikiwa nimelala fofofo, simu yangu ambayo ilikuwa kwenye 'vibration mode' ilikuwa ikiita.

Wife kwakuwa alikuwa bado hajalala akawa ananiamsha niipokee lakini kabla hajafanikiwa kuniamsha akashangazwa kuona namba iliyokuwa inanipigia ni namba yake mwenyewe ambayo anatumia kwenye simu yake na wakati huo simu yake akiwa nayo mkononi, cha kushangaza zaidi ni kuwa simu yake haikuwa na salio la kuweza kupiga wala kubeep na haikuwa inaonesha kama inapiga simu, lakini kwenye simu yangu inaonekana ni namba yake ndiyo inapiga, namba yake ambayo nimeisave vizuri kabisa.

Wife akaamua kupokea mwenyewe tu ili aone ni kitu gani. Hakukuwa na sauti yoyote iliyosikika na yeye pia hakuongea chochote. Akawa ameiskilizia mpaka sekunde ya 31 akakata.

Kwakuwa nilikuwa nimechoka sana wife hakutaka kuniamsha na badala yake akaja kunielezea kila kitu asubuhi ambapo iliingia habari nyingine ya kushangaza tena.

Mama yangu mzazi alimpigia simu wife kumuuliza kwanini alikuwa anampigia usiku wa manane, hii ikiwa na maana kuwa namba hii ya wife ilionekana ikimpigia mama yangu mzazi pia usiku ule ule hali ya kuwa haikuwa na salio na kwenye simu ya wife hakuna call history wala hakuna salio la kupiga wala kubeep.

Sasa kitu kinachochagiza wasiwasi kwenye hili ni kwamba namba hii anayotumia wife ni namba iliyokuwa ikitumiwa na marehemu bibi yangu mzaa mama kama namba ya akiba na ina usajili kamili wa marehemu bibi ambae alifariki mwaka jana.

Hapa ndo kidogo pamefanya tuwe na wasiwasi.


Mimi kichwani mpaka sasa nina maswali mawili, kwamba je inawezekana likawa ni swala la kimtandao? au ni jambo linalohusiana na mambo ya giza kutokana na kua namba hii ilikua ikitumiwa na marehemu bibi yangu?


Kiukweli nimeshindwa kabisa kuelewa mpaka sasa. Naombeni msaada wa mawazo yenu jamani kwa ambao huenda mnafahamu au mmewai kuona mambo kama haya.
wafu hawajui neno lolote
 
Ishu ni kuachana na hiyo laini coz kisheria tu mkeo ana kosa,,sasa mnavyotaka kuchimba tatizo nini ndo huenda mkajikuta kwenye matatizo kabisaaaaa.
 
Kuna kisa huko kenya:
Tajiri mmoja baada ya kufariki ndugu wakataka kuzikwa na simu yake mshindi kipindi hiko.
Kumbe wezi wakapata habari tajiri kazikwa na mali za kutosha.
Baada ya maziko kumalizika usiku wakafukua na kuondoka na kila kitu pamoja na simu.
Mmoja wa wezi kuangalia simu kakuta majina ya familia si ndo kupiga simu kuwa anakuja kuwafata walio sababisha yeye kafa.
Kumbe usiku wanaambiwa asubuhi kuna ndugu katoka kijiji cha mbali kuja kuasalimia na pole,kilichotokea nusu wamzimishe ndugu getini.
 
W
Imetokeaje mkeo akarithi namba ya marehemu wakati hawana undugu?
watanganyika tunapenda kuhifadhi vitu chakavu bila sababu wengi wetu tuna vitu ambavyo tunavyo na hatuvitumii lakini tunaona fahari kuwa navyo. sasa fikiria huyu hata hajui kuwa kuendelea kutumia hiyo namba ni kinyume cha sheria na anaona sawa tu.
 
matatizo ya kutumia tecno,itel na infinix hayo.ujui jina lipo dublicate
Sina hamu na itel zamani kuna siku nipo kwenye ofisi kubwa hapa mjini posta nafanya presentation pale katikakati ya presentation nasikia vikelele vya mahaba mara vinaongezeka vinapungu..

Kimoyomoyo nikajua wale nilikuwa nawafanyia presentation wameacha YouTube ya monitor wazi ingawa nikawa najiuliza wanawezaje kuweka sound kam ile ofcn.

Kidogo sauti ikapanda juu ndio kushtuka hapo hivi natoa simu mfukoni alafu mbele za watu nilihisi aibu sana sikujua saa ngapi simu ile imejitoa password na ikaenda YouTube na kuchagua video mbovu vile..

Siku ilivurugika vibaya sana!
Kiukweli sikuwah kurudi ile ofc tena na ikawa mwanzo mwisho wa kuwa na brand bovu za simu. Nipo makini sana kwenye hili maana yameshanikuta..!
 
Back
Top Bottom