Naomba tofauti ya maneno haya yanayotumiwa serikalini

Una idea ila umezunguuuka
 
Baraza ni kundi la watu ambalo liko kwa ajili y a kutoa ushauri, kuongoza n kuandaa taratibu ndogo ndogo za kuongoza Jambo fulani
Mabaraza Mara nyingi yanakuwa na vikao vya Mara kwa Mara kwa sababu kazi yao kubwa ni consultation hivyo wanahitaj discussion za Mara kwa Mara
Mf Baraza la michezo, Sanaa,kiswahili

Tumefanya ni kundi la watu linalochaguliwa either na serikali au organization yoyote kw ajili ya kushughulikia jjambo fulani la muda mfupi
Kazi ikiisha time inavunjwa




a
 
"Taasisi" nadhani inafaa kutumika kwa vyombo vinavyofanya tafiti.
 
"Taasisi" nadhani inafaa kutumika kwa vyombo vinavyofanya tafiti.
.fano w taasisi tulizonazo
Taasisi ya elimu
Taasisi ya elimu ya watu wazima
Taasisi ya afya na sayansi shitokishi
Taasisi ya udhibitu ubora was mbegu
 
Idara ni kitengo kilichomo ndani ya taasisi
Mfano taasisi ya elimu Ina kitengo cha fedha au idara ya fedha
 
Utofauti wake uko katika maeneo kadhaa nitafunguka machache;

1. Ukubwa wa majukumu

2. Mipaka ya majukumu

3. Muundo wa Taasisi

4. Idadi ya vitengo

5. Mamlaka ya uteuzi

1. Ukubwa wa majukumu:

Idara huwa ni sehemu ndogo ya Taasisi kubwa. Mara nyingi Idara inakuwa na majukumu maudhui tu na haijihusishi na mambo mengine;

Mfano Idara ya Maji. Idara ya usalama wa Taifa (siku hizi haiitwi Idara) bali ni TISS (mawakala wa ulinzi anuai) . Jina la Idara yawezekana liliasiliwa toka kwenye iliyokuwa (special Branch)

2. Mipaka ya Majukumu

Hii ndio makazini tunapewa wanaiita JOB DESCRIPTION. Hapa utakutana na neno Mamlaka zaidi kwa kuwa na mamlaka katika kutekeleza majukumu yaliyo ainishwa.

Mipaka hii ya kimajukumu inaweza ikatokea hata kwenye Idara (yaani Idara ukawa ina kitengo kidoko chenye mamlaka).

Mfano ndani ya Idara kunakuwa na watu wenye mamlaka juu sehemu Moja tu.

3. Muundo wa Taasisi
Kuna muundo ambao fulani ndio unao amua.

Mfano;

Mkurugenzi anaendesha Taasisi/shirika ambayo ndani yake inakua na Idara na mamlaka huo ukubwa ndio unaosababisha utamkwaji.

Kwenye muundo huo utakuta sheria inatamka kwamba anaueongoza Shirika/Taasisi ataitwa Mkurugenzi au Mkurugenzi Mtendaji.

4. Idadi ya vitengo
Hapa naomba nihamishe goli kidogo
(Utofauti Kati ya University na college)

Chini ya Taasisi hiyo iko complex kiasi Gani, ina idadi ngapi za vitengo na vitengo.

Mfano; BODI ya wakurugenzi inaundwa na Wakurugenzi wanaounda Taasisi/Shirika lakini wakugenzi ni viongozi wa vitengo vyao lakini wanapangiwa majukumu na Mkurugenzi Mkuu/Mtendaji na anapotamkwa kama Mtendaji ina maana naye kuna kitengo mahususi chini yake.

Tofauti na Wakurugenzi wakuu ambao wao huwa watch dog wa Taasisi/Shirika katika ngazi ya maamuzi pekee.

5. Mamlaka ya uteuzi
Taasisi/Shirika yapo ya aina mbili

Mosi lile ambalo anayeliongoza anateuliwa na Rais na

Pili wale wanaopanda vyeo hadi kufikia cheo hicho kutokana na sababu mbalimbali.

Mfano; BODI ya Sukari Mkurugenzi anateuliwa na Rais. Ila BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU Mkurugenzi wake anaomba Kazi na analia Mkurugenzi Mtendaji kwa kuwa kipo kitengo mahususi chini yake.

Ilihali wale wakurugenzi wanaoteuliwa na Rais wao wanakuwa ni ma overall in charge na mara nyingi huisimamia zaidi BODI YA WAKURUGENZI kuliko Taasisi husika.

NIPO TAYARI KUBORESHEWA AU KUKOSOLEWA
 
Oni Sigala
 
mamlaka, taasisi, wakala, bodi baraza vyote vinasimamia na wizara husika
Na zinaanzishwa kwa sheria maalumu
Tume inaundwa pale kunapokuw na Jambo la kushughulikiwa maana sio kitu Cha kudumu
 
Wataalamu wa kiswahili hebu waje
 
mamlaka, taasisi, wakala, bodi baraza vyote vinasimamia na wizara husika
Na zinaanzishwa kwa sheria maalumu
Tume inaundwa pale kunapokuw na Jambo la kushughulikiwa maana sio kitu Cha kudumu
Sio kila tume inakua inaundwa kushughulikia jambo mahususi na inapomaliza jambo hili basi muda wake nao unaisha. Mfano wa tume hizi unazozizungumzia wewe ni Tume ya Nyalali (Vyama vingi), Tume ya Warioba (katiba mpya), Tume ya Prof. Osorro (Makinikia) n.k

Zipo tume ambazo ni vyombo vya kudumu na zina majukumu ya kila siku (endelevu) ya kiutendaji. Mfano Tume ya madini, Tume ya Uchaguzi (NEC), Tume ya vyuo vikuu (TCU), Tume ya utumishi wa mahakama, n.k
 

Mkuu, katika ufuatiliaji wangu nimekuja kugundua haya mambo yana mkanganyiko mkubwa sana na hakuna clear difference baina ya hayo majina ya hivyo vyombo vya kiserikali.

Ukitaka kuweka utofauti, kuna sehemu nyingine utakutana na kukiukwa kwa ile tofauti (contradiction).

Kwa mawazo yangu ni kwamba, hayo maneno sio kwamba yana maana moja, la hasha. Ila yanatumika ili angalau kuleta utofauti baina ya vyombo mbalimbali vya serikali maana viko vingi sana (isingependeza kila chombo kuitwa taasisi).

Mfano, ukisema kurugenzi ni chombo ambacho kinaongozwa na mkurugenzi, unakuja kugundua kwamba kuna mamlaka, wakala au taasisi zinaongozwa na wakurugenzi pia (contradiction).

Nizungumzie TAASISI kidogo. (Hoja yako namba 5).
Kwa ufahamu wangu, najua kuna taasisi za aina mbili, kuna zinazoitwa "institutes (au institutions)" na zile zinazoitwa "Bureau". Sasa je kuna tofauti gani kati ya hizi "taasisi mbili"
Mifano:
Taasisi Bureau
NBS (Takwimu)
TBS (Viwango)
PCCB (Rushwa)
N.k
Taasisi Institute
TARI (Utafiti kilimo)
NIMR (Utafiti afya)
JKCI (Taasisi ya Moyo J. Kikwete)
MOI (Taasisi ya mifupa)
TIE (Elimu)
N.k

Sasa kama hata kwenye taasisi tu kuna mkanganyiko, itakuaje huko kwingine?

Umelata hoja nzuri, ngoja wajuvi na wajuzi watutoe tongotongo
 
Hata hyo tume ya vyuo vikuu inaweza ikavunjwa Kama itafika mahali itakuwa haihitajiki Tena the same kwenye tume ya madini nk
Tume sio kitu Cha kudumu inaweza ikafanya kazi hata miaka kumi lakini sio kitu Cha kudumu Kama taasisi
Hicho nduo nilimaanisha

Tume ya uchaguzi , je uchaguzi ukiisha inafanya kazi gani. Naomba unieleweshe
 
Tofauti ipo
Kila chombo kinaendeshwa kisheria
Na kinaanzishwa kisheria na sheria hazifanani, pia majukumu ya Kila chombo kulingana na sheria zilizowekwni tofauti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…