Smart Guy
JF-Expert Member
- Dec 19, 2016
- 6,808
- 6,934
Hivi kazi ya infrared ni nini wakuu?Siku pixel akitubless hata na infrared tu nitampenda zaidi .bonge la useful feature ambalo wazungu wengi hawalitaki
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hivi kazi ya infrared ni nini wakuu?Siku pixel akitubless hata na infrared tu nitampenda zaidi .bonge la useful feature ambalo wazungu wengi hawalitaki
Google pixel simu Bora kwangu ukweli usemwe Tena kwao sisi wapenda kusoma vitabu ikigika usiku Inajiweka Night mode yake Ile amazing and gorgeous and fire [emoji91][emoji28][emoji28] Ndio maana wanasema ni love it or hate it. Mtu anayeikubali Stock Android ukimpeleka MIUI ataona mapichapicha tu. Na wa MIUI ukimpeleka Stock Android naye ataona mapichapicha tu [emoji28][emoji28]
Kuna ile premium look naipenda kwenye Xiaomi kama hii[emoji116][emoji116]View attachment 2566322View attachment 2566323
Sasa ya Google Pixel ipo hivi[emoji116][emoji116]View attachment 2566325View attachment 2566327
Mimi kati ya hizo mbili naona ya Xiaomi inavutia mbele ya macho. Ila mwingine ataona ya Google Pixel inavutia zaidi. Tunatofautiana [emoji28][emoji28]
Ila unakubaliana na mimi kuwa kila mtu na anachokipendaGoogle pixel simu Bora kwangu ukweli usemwe Tena kwao sisi wapenda kusoma vitabu ikigika usiku Inajiweka Night mode yake Ile amazing and gorgeous and fire [emoji91]
Mkuu Reuben ChalleIla unakubaliana na mimi kuwa kila mtu na anachokipenda
Redmi Note 12 5G ina display kali kuliko Redmi Note 12 4GMkuu Reuben Challe
Nina redmi note 12 4g wiki ya pili sasa. Nataka niiuze ninunue Redmi nyingine isiyozidi 450k, unanishauri nichukue ipi yenye display kali kuliko ya note 12.
Kwa hiyo,ulitaka alinganishe na Nokia Asha?Uwe unalinganisha matoleo ya mwaka mmoja, pixel 6 ni mpya unailinganisha na masimu ya miaka minne nyuma
Kwani hajui? Kaulizia kati ya simu mbili anazozipenda yeye. Hakuuliza toleo jipyaHii simu angeilinganisha na Samsung Galaxy S21 Ultra! Analinganisha kitu cha 2019 na 2021?
Ungempa hiyo elimu kwanza.
Bottom line: umejibu kisomi sana.
Ni kweli!Hayo maelezo tu ila ukipewa kila moja uitumie ndani ya siku mbili, hakika utaenda Samsung.
Mkuu na vp kuhusu note 10 plus na Samsung s 22 plusSamsung Galaxy Note 10 Plus vs Google Pixel 6
Hizi simu ni za miaka tofauti ila nitajaribu kuzilinganisha ili upate mwanga kidogo ipi inakufaa.
1. Display
Kioo cha Samsung Galaxy Note 10 Plus kina resolution ya 1440x3040p wakati cha Google Pixel 6 kina resolution ya 1080x2400p kwa hiyo Cha Samsung kina resolution kubwa zaidi. Pia kioo cha Note 10 Plus kina pixel density kubwa ya 495ppi ukilinganisha na 411ppi ya kwenye Pixel 6. Lakini kioo cha Google Pixel 6 kina refresh rate ya 90Hz huku cha Samsung Note 10 Plus kina 60Hz refresh rate, na bado Pixel 6 kioo chake kinafikia brightness ya 844nits huku Note 10 Plus inaishia 789nits. Kama unaangalia kioo kizuri ninashauri uchukue Google Pixel 6.
2. Peformance
Samsung Galaxy Note 10 Plus inatumia chipset ya Samsung Exynos 9 octa 9825 ambayo imetengenezwa kwa 7nm process wakati Google Pixel 6 inatumia chipset ya Google Tensor iliyotengenezwa kwa process ya 5nm. Hapa bila kuzunguka Google Tensor ndio Ina nguvu zaidi, clock speed kubwa na stronger GPU. AnTuTu score ya Pixel 6 ni kubwa (718,000) kuliko ya Samsung Galaxy Note 10 Plus (549,000). Hii ina maana kwamba Google Pixel 6 ina uwezo mkubwa zaidi wa kufungua na ku-run apps nzito nzito kuliko Samsung Note 10 Plus. Kama unataka simu yenye peformance kubwa chukua Google Pixel 6
3. Kamera ya nyuma
Samsung Galaxy Note 10 Plus ina 12MP main camera na Google Pixel 6 ina 50MP. Simu zote mbili haziwezi kurekodi 8K videos ila zote zinarekodi maximum kwa 4K@60fps. Samsung Galaxy Note 10 Plus inaweza kurekodi video za 1080p@240fps ambayo ni kubwa kuliko 1080p@60fps ya kwenye Pixel 6. Samsung Galaxy Note 10 Plus inarekodi slow motion videos at 960fps(720p) huku Pixel 6 inaishia 240fps(1080p).
Tukija kwenye hitimisho, Google Pixel 6 ina kamera nzuri zaidi ya Samsung Note 10+. Picha za Google Pixel 6 ni nzuri kuliko za Samsung Galaxy Note 10+ na video quality ya Pixel 6 pia ni kubwa kuliko ya Note 10+. Kwenye kamera ya nyuma mshindi ni Google Pixel 6.
4. Kamera ya mbele
Samsung Galaxy Note 10 Plus ina 10MP selfie camera na inaweza kurekodi video za 4K@30fps. Google Pixel 6 ina 8MP selfie camera na video zake zipo limited kwenye 1080p@30fps. Kama unataka selfie camera nzuri basi chukua Samsung Galaxy Note 10 Plus
5. Battery life
Samsung Galaxy Note 10 Plus ina betri lenye ujazo wa 4300mAh wakati Google Pixel 6 ina 4614mAh. Ukizitumia simu zote mbili kuperuzi mtandaoni Note 10 Plus itadumu na chaji kwa masaa 7 na dakika 47 wakati Google Pixel 6 itadumu kwa masaa 8 na dakika 58. Ukizitumia kuangalia video Galaxy Note 10 Plus itadumu kwa masaa 14 na dakika 19 wakati Google Pixel 6 itadumu kwa masaa 16 na dakika 38. Kwa kucheza magemu Note 10 Plus itadumu kwa masaa 4 na dakika 55 wakati Pixel 6 itakaa kwa masaa 5 na dakika 24. Standby time ya Note 10 Plus ni 97 hours wakati Google Pixel 6 ni 92 hours. Kiufupi Google Pixel 6 ndio inatunza chaji zaidi.
6. Charging speed
Samsung Galaxy Note 10 Plus inatumia 45W charger na inajaza simu chaji ndani ya saa 1 na dakika 5 tu wakati Google Pixel 6 inatumia 30W charger inayojaza chaji kwa saa 1 na dakika 53. Kwa hiyo Galaxy Note 10 Plus inachaji faster zaidi.
7. Memory
Google Pixel 6 ina 8GB RAM, Galaxy Note 10 Plus inakwenda hadi 12GB RAM. Google Pixel inatumia memory type ya LPDDR5 ambayo ni faster zaidi ya LPDDR4X inayotumiwa na Samsung Galaxy Note 10 Plus. Kwenye hili suala Google Pixel 6 ndio mshindi.
8. Storage
Samsung Galaxy Note 10 Plus ina chaguo moja tu la storage yaani 256GB wakati Google Pixel 6 ina machaguo mawili ambayo ni 128GB na 256GB. Google Pixel 6 inatumia storage type ya UFS 3.1 ambayo ni faster kuliko UFS 3.0 ya kwenye Samsung Galaxy Note 10 Plus. Kwenye storage type mshindi ni Google Pixel 6.
9. Software
Samsung Galaxy Note 10+ Ina Android 9 (Pie) na unaweza ku-update Hadi Android 12. Google Pixel 6 ina Android 12 na unaweza ku-update hadi Android 13 na bado Pixel 6 itaendelea kupata more updates zitakapoendelea kutoka. Software ya Galaxy Note 10+ ni One UI na ya Google Pixel 6 ni Stock Android.
Kwenye Note 10+ software peke yake imetumia 31.6GB wakati kwenye Google Pixel 6 imetumia 17.6GB tu. Kwenye software mshindi ni Google Pixel 6.
10. Design
Ziangalie mwenyewe uone ni design ipi itakufaa
11. Mambo mengine
*Samsung Galaxy Note 10 Plus ina telephoto camera, Google Pixel 6 haina.
- Samsung Galaxy Note 10 Plus ina sehemu ya kuwekea memory card yenye storage hadi 1TB, Google Pixel 6 haina sehemu ya kuwekea memory card.
- Samsung Galaxy Note 10 Plus inasupport laini 2, Google Pixel 6 inakaa laini 1 tu
- Zote mbili zinakubali 5G
- Samsung Galaxy Note 10 Plus ina FM Radio, Google Pixel 6 haina
- Google Pixel 6 ina eSIM technology, Samsung Galaxy Note 10 Plus haina.
12. Hitimisho
Kiukweli kati ya hizo simu mbili Google Pixel 6 ndio nzuri zaidi. Ninakushauri uchukue Google Pixel 6.
Mkuu hiyo S22 Plus ni flagship ya 2022 na Note 10 plus ni flagship ya 2019. There is no way Note 10 Plus ikawa better than S22 PlusMkuu na vp kuhusu note 10 plus na Samsung s 22 plus
Jomba uliua sana 🤣🤣A. DISPLAY
1. Google Pixel 6 kioo chake kina refresh rate ya 90Hz, hiyo iPhone 11 ina 60Hz tu.
2. Kioo cha Google Pixel 6 ni OLED panel na ni higher quality kuliko cha iPhone 11 ambacho ni LCD
3. Kioo cha Google Pixel 6 kina mwanga wa kutosha kuliko iPhone 11 na hufikia hadi 848nits, iPhone 11 inaishia 677nits tu.
4. Kioo cha Google Pixel 6 ni Gorilla Glass Victus ambayo ni bora kuliko cha iPhone 11 ambacho ni Tempered Glass tu.
5. Kioo cha Google Pixel 6 kina pixel density ya 411ppi wakati iPhone Ina 326ppi
6. Kioo cha Google Pixel 6 kina resolution kubwa (1080x2400p) kuliko cha iPhone 11 ambacho kina resolution ya 828x1792ppi.
7. Kioo cha Google Pixel 6 kina feature ya Always on display, iPhone 11 haina.
Conclusion: KIOO CHA GOOGLE PIXEL 6 NI KIZURI KULIKO CHA IPHONE 11.
B. PEFORMANCE
1. Google Pixel 6 inatumia chipset ya Google Tensor na ina hadi 8GB RAM. iPhone 11 inatumia chipset ya Apple A13 Bionic na ina 4GB RAM
2. Chipset ya Google Tensor ina clockspeed kubwa 2800MHz kuliko ya iPhone 11 ambayo clockspeed yake ni 2650MHz tu.
3. CPU cores kwenye Google Tensor ni nyingi 8 (2+2+4) kuliko za Apple A13 Bionic 6 (2+4)
4. Lithography process ya Google Tensor ni 5nm wakati hiyo Apple A13 Bionic ni 7nm
5. AnTuTu score ya Google Pixel 6 ni kubwa (726882) kuliko ya iPhone 11(640641)
Conclusion: GOOGLE PIXEL 6 INA UWEZO MKUBWA ZAIDI WA KUFANYA VITU VIZITO NA HUVIFUNGUA KWA HARAKA ZAIDI KULIKO IPHONE 11.
C. MEMORY
1. Google Pixel 6 ina hadi 8GB RAM iPhone 11 Ina 4GB RAM tu.
2. Google Pixel 6 inatumia memory type ya LPDDR5 ambayo ni faster kuliko LPDDR4X ya kwenye iPhone 11.
3. Google Pixel 6 ina storage ya 128GB na 256GB basi, iPhone 11 ina storage ya 64GB, 128GB na 256GB.
4. Zote hazina sehemu ya kuwekea Memory Card.
Conclusion: HAPA MSHINDI NI GOOGLE PIXEL 6
D. BATTERY
1. Google Pixel 6 ina betri la 4614mAh na iPhone 11 ina betri la 3110mAh
2. Google Pixel 6 ina 30W wired charger na iPhone 11 ina 18W wired charger.
3. Kwa kutumia chaja zao iPhone 11 hujaa kwa saa 1 na dakika 45 ambayo ni faster kuliko Google Pixel 6 inayojaa kwa saa 1 na dakika 53.
4. Zote mbili zina wireless charging
5. Google Pixel ina wireless reverse charging, iPhone 11 haina.
6. Google Pixel hudumu kwa masaa 8 na dakika 58 kwa kuperuzi mtandaoni. iPhone 11 inafanya hivi kwa muda mrefu zaidi kuliko Pixel 6, masaa 11 na dakika 39
7. Google Pixel 6 hudumu na chaji kwa masaa 16 na dakika 38 kwa kuangalia video, iPhone 11 inadumu kwa masaa 15 na dakika 16
8. Google Pixel 6 hudumu na chaji kwa masaa 5 na dakika 24 kwa kucheza magemu, iPhone 11 masaa 5 na dakika 9
9. Standby time kwenye Google Pixel 6 ni 92hrs na kwa iPhone 11 ni 121hrs
Conclusion: KWENYE SUALA ZIMA LA BATTERY IPHONE 11 IPO VIZURI ZAIDI OVERALL INGAWA TOFAUTI NI NDOGO SANA.
E. KAMERA YA NYUMA
1. Google Pixel 6 ina 50MP main camera, iPhone 11 ina 12MP main camera.
2. Simu zote mbili haziwezi kurekodi video za 8K.
3. Simu zote mbili zinaweza kurekodi video za 4K@60fps, 1080p@60fps na slow motion za 240fps(1080p)
Conclusion: PICHA ZINAZOPIGWA NA KAMERA YA NYUMA YA GOOGLE PIXEL 6 NI ZA HIGH QUALITY KULIKO ZA IPHONE 11. PIA GOOGLE PIXEL 6 INATOA VIDEO NZURI KULIKO IPHONE 11.
F. KAMERA YA MBELE
1. Google Pixel 6 ina 8MP selfie camera na iPhone 11 ina 12MP selfie camera.
2. Selfie camera ya iPhone 11 inarekodi hadi video za 4K@60fps wakati Google Pixel 6 inaishia 1080p@30fps
Conclusion: IPHONE 11 INA SELFIE CAMERA NZURI KULIKO GOOGLE PIXEL 6.
G. MAMBO MENGINE
1. Google Pixel 6 inatumia Bluetooth version ya kisasa zaidi (v5.2) wakati iPhone 11 inatumia Bluetooth v5
2. Google Pixel 6 inatumia USB version 3.1, iPhone 11 inatumia USB version 2
3. Google Pixel 6 inasupport OTG, iPhone 11 hai-support OTG.
4. Google Pixel 6 ina 5G internet speed, iPhone 11 haina 5G
5. Google Pixel 6 ni simu ya October 2021, iPhone 11 ni simu ya September 2019.
6. iPhone 11 itapokea iOS support kwa muda mrefu zaidi kuliko ambavyo Google Pixel 6 itapokea Android updates
7. Google Pixel 6 ina fingerprint scanner ndani ya display, iPhone 11 haina kabisa fingerprint scanner.
8. Kwa mtazamo wangu, Google Pixel 6 ina mwonekano wa kisasa zaidi kuliko iPhone 11
H. GENERAL CONCLUSION
Google Pixel 6 ni simu bora zaidi ya hiyo iPhone 11 kwa hiyo hapo chukua Google Pixel 6. Hizi simu hazipaswi hata kufananishwa.