Hawa watu wanasikitisha sana
Accumen Mo na
inamankusweke nakusihini pamoja na kuisihi nafsi yangu katika kumcha Allah na kusoma mafundisho Sahi ya dini yetu ili tuongeze ufahamu na ujuzi katika masuala mbalimbali ya kidini.
Ni ajabu sana muislamu kukataa hadithi kabisa kwa madai Qur'an inatosha na mengineyo hata kikawaida darasani lazima mwalimu awepo wa kufafanua mafundisho katika kitabu na kuelezea namna ya kuyaendea ndio maana haukupewa vitabu pekee ujisomee mpaka darasa la 7 , secondary nk japo mtu anauwezo wa kusoma na kuelewa sasa iweje elimi ya dini iachwe hivi hivi na kufungua mlango wa kila mtu kutumia fikra zake ?
Mimi nimesoma Qur'an yote word to word sehemu nyingine kibao vitu vimeweka in general ukiweka fikra zako unapotea lazima upate muongozo kuhusu umahasusi wa Aya ,lengo na ufanuzi kupitia hadithi n.k
Hata Ibada zetu tunazoziendea kila siku huwezi kukuta katika Qur'an in details nyingine hata kutwaja hazijatajwa , sasa kusema Qur'an inatosha hakuna haja ya hadithi ni sawa na kuipinga Qur'an yenyewe na kufanya uislamu uwe kama ugalatia kila mtu kutia fikra zake.
Uzuri ni kwamba hadithi hazikuwa zinachukukiwa kiholela kama maneno ya vijiweni bali kuna mlolongo wake na elimu pana katika hilo. Dini ninkusoma na sio kuleta fikra ,jazba na mihemko..