Naomba uniulize chochote kuhusu kufanikiwa katika Biashara na Ujasiriamali


Mkuu kama huta-mind naomba ufafanuzi kuhusu forex.Channel/platform zipi huwa unazitumia?Na unafanyaje ili kuzuia loss(pesa yako kupotea)?
 
Mkuu ONTARIO kwa kilimo cha Muhogo unachukua muda gani kupanda mpaka unavuna.
 
Mganga anayekupa dawa ha, biashara yako yuko wapi?
Biashara haiitaji mganga/Mchawi your the only mganga. kabla ya kuifanya unahitaji upembuzi wa kina thorough analysis in/out then kupangilia Manegiment yako, ubunifu juu ya unachotaka fanya (usifanye kwa mazoea) lakini pia usiendeshe biashara kwa remote na hii ndio sababu waajiriwa wengi hufeli kwenye biashara.
 
Yah! Ni hekari moja kwa laki, lkn inategemea pia na mwenyeji wa shamba, kama ni kipindi cha njaa unapata hata less than hapo.
Mkubwa kuna thread yako moja ya maisha ya SA sasa ndugu kuna chaka moja nimelifumania nahitaji trekta unaweza nifanyia uataarabu wa bei za MF 165 na MF 290 2WD na 4WD kwa huko SA maana naambiwa hata magari ni bei chee sana huko
 
Hapo kwenye kuacha ajira wengi wanashindwa sana coz wanaona Biashara kama mchezo wa pata potea wakati ajirani anauhakika na nini anapata/atapata. Na ujasiriamari unataka kwanza kujizila/kata mzizi wa aibu then kujitoa ustahimilivu kuachana na unnecessary spendings, kuwaelewa stake holder wa biashara yako, kua aggressive to market changes, yote kwa yote ubunifu na uthubutu maters alot. Sisi waoga kujaribu changamoto mpya wengi wetu tunaona mafanikio ni kama EVENT kumbe mafanikio ni PROCCES.
 
Mkuu ONTARIO unajua chochote kuhusu JOINT VENTURE CAPITAL/Mitaji ya Ubia, kama unajua hebu sema neno kidogo
 
Mkubwa jinmtu sikushauri hata kidogo kuacha kazi utaumia kuna kupata hasara kwenye ujasiriamali ukukufanya ukate tamaa kabisa ya maisha, mtoa mada ni kijana mdogo sana hana familia wala majukumu ya kumtunza mtu mwingine hata akianguka leo bado ana muda mwingi sana wa kuinuka. Jiangalie nafasi yako wewe kama wewe sometimes utakuja kugundua kwamba kuishi maisha mazuri si lazima sana uwe na pesa nyingi ajabu. Ridhika kwanza na maisha uliyo nayo then mambo yakiwa sawa tanua kwingineko lakini suala la kuacha kazi usijaribu ujasiriamali si lele mama
 
Mkuu Hongera sana sana!
I feel motivated though sina hata pakuanzia. Nimekuelewa sana kiongozi. Labda nami ni confess hivi, mimi ni graduate huu ni mwaka wa 3 nipo mtaani sina ajira na nimemaliza nna LLB degree. Nimetafta ajira mpaka nimechoka, nikatafuta internship bado sikupata mpaka leo hii, nikatafuta ata volunteering lakin shida ikawa ni ile ile. Kibaya zaidi katika famia sina ata mtu wa kuniboost japo MTAJI, kimsingi hali ni ngumu sana, nimefrah sana kuona una mafanikio makubwa ukiwa na umri mdogo. God bless you, natamani kukuuliza in private unipe japo mbinu moja tu ya mimi kutoka lakin umesema hujibu izo txt wala hutoi namba. Kimsingi mwanzo ni mgumu sana hasa pale unapokosa pakuanzia, naamin ipo siku nasi tutaangukia. Nilipata wazo la kuunda kikundi ili tukakope ela bank tufanye green house na wenzangu kwa kuwa hatuna mtaji lakin tulishindwana kwa kuwa na ideology tofauti baina yetu. Nilifikiria kufuga kama wewe lakin tatizo likawa mtaji na eneo. Sasahiv nafkiria kilimo popote nitaenda kulima lakin hata ela ya kukodi mashamba sina. Nipo tayar wadau yeyote anaedhani ana fursa tunaweza share nae tukatoka nipo tayar ancheki wakati wowote 0719 815018.
 
suluta unazingua umesoma chuo kikuu alaf unataka kunishawishi kuwa huna hata hela ya kukodi shamba uliitumia chansi vibaya wewe
 
Great ONTARIO. The thread is fullest of inspirational story, qn and answers. Tangu umepost nilikuwa wa kwanza kuona thread then nkajipa muda wa kupitia kimya kimya. Iam coming lol
 
Mkuu .. kuku 100 kama una banda na vifaa vy chakula na maji, unaeza tumia gharama kiasi gani na faida yake ni kiasi gani kwa kuku wa nyama wa wiki 4?
Kuna mahali nyuma amejibu kuwa kwa kawaida (kama unanunua chakula) utawauza kwa laki sita nawe utabaki na faida ya laki moja hivyo gharama za kuwanunua na matunzo ni laki tano.
 
Mkuu jaribu kupitia brighter Monday...shikana paralegal naona malipo ni laki tano...vilevile omba kwa kujitolea as legal officer angalau upate uzoefu kwa wengine
 

MTAJI ni nguvu yako ambayo Mwenyezi Mungu amekujalia!
Umeshindwa ktk miaka hiyo 3 hata kutafuta kazi ya kufundisha watoto 'tuition' ili upate pesa ya kuanzia biashara?
Ukisubiri mtu akupe mtaji au benki ikukopeshe pesa ya mtaji utasubiri mpaka mwenyewe utachoka!
 
Mkuu huwa nasoma sikoment. Ila kwa hili
 
Mkuu jaribu kupitia brighter Monday...shikana paralegal naona malipo ni laki tano...vilevile omba kwa kujitolea as legal officer angalau upate uzoefu kwa wengine
Brother, nimetembea na bahasha sana kwenye law firm nikatafuta pakujishkiza lakin kila ukiifika wanakwambia: watu wamejaa, ofisi yetu ndogo, hatuna nafasi, hatutoi posho na mengine mengi. Websites karibu zote nimejisajili kama Zoom tz, TAYOA, ajira zetu, brighternmonday, ajira tz et.c! Wala si kama nna matokeo mabaya sana, no nina UPPER SECOND. Labda zamu yangu bado
 
Nitumie PM boss, nitarudi kwako June nikiweka mambo yote sawa. Nafungua ofisi mpya very soon, km una vigezo unaweza kuwa kati ya waajiwa wa mwanzo kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…