Naomba ushauri: Mchepuko wangu ameolewa leo, nimekubwa na msongo wa mawazo

Naomba ushauri: Mchepuko wangu ameolewa leo, nimekubwa na msongo wa mawazo

Haya mambo ya uzinzi ndio yanasababisha ndoa nyingi siku hizi kuwa jehanam maana watu mnajisifu kabisa kuwa na michepuko.
Kabla hujanitazama mimi kwa kunihukumu jitazame moyoni kwako kama u msafi kuliko mimi.
 
MIMI nadhani inabidi uiheshimu ndoa yake kama yeye alivyokuwa anaiheshimu ndoa yako...amesha kuwa mke wa mtu...na wewe ni mume wa mtu...ni vibaya sana kuharibbu ndoa ya watu kwa sababu zinazozuilika ni bora ukatafuta mchepuko mwingine...!
 
Habari zenu wadau wa Jamiiforums.

Ni mara yangu ya kwanza kutuma ujumbe wenye maudhui kama haya hapa jukwaani.

Naomba mnipe ushauri jinsi ya kukabiliana na stress zinazonikabili.

Suala liko hivi; mwaka jana Oktoba mpenzi (mchepuko) wangu alipata mchumba akaja kuniuliza nikubali au nikatae asiolewe.

Mimi niliona sio vema kumkataza asiolewe maana mimi nina mke, lakini huyu mdada tulielewana sana, aliheshimu ndoa yangu sana, alikua mshauri mzuri mpaka kwenye masuala yangu ya kifamilia na kikazi.

Kuna wakati alikua akinishawishi nimuoe awe mke wa pili, lakini sikuwahi kuwaza kuwa na mke zaidi ya mmoja hivyo nilikataa, akasema sio shida anataka tuendelee kuwa wapenzi no matter what.

Sasa baada ya kumshauri akubali kuolewa, kweli jamaa mwezi Januari akaleta barua, kisha taratibu zote zikafuata.

Sasa leo ndio siku wapo wanafunga ndoa, kuna bonge la sherehe, dada zake (shemeji zangu) wamenipigia simu niende, rafiki zake wa karibu wa kazini kwao wamenipigia simu niende lakini moyo umeshindwa kabisa japo zawadi nilinunua nikampa rafiki yake akapeleka.

Wakuu huyu mwanamke ameolewa kwa ruhusa yangu lakini nimepata stress tangu juzi kila ninachofanya hakiendi, kila ninachoshika hakiendi, yaani nahisi kama akili zangu zimesimama kufanya kazi.

Nisadieni namna ya kukabiliana na hali hii ndugu zangu. Naomba msinitukane, msinihukumu wakuu, nisaidieni natokaje kwenye huu msongo wa mawazo.
....i used to be the other man, now it's flipped i dont want you with another man....Nelly.
 
Mimi niliona sio vema kumkataza asiolewe maana mimi nina mke, lakini huyu mdada tulielewana sana, aliheshimu ndoa yangu sana, alikua mshauri mzuri mpaka kwenye masuala yangu ya kifamilia na kikazi.
Upuuzi mtupu... Yaani unashindwa kumshirikisha mkeo kwa kumdharau kuwa hawezi toa ushauri katika nyumba yenu unajidai kumuona huyo mchepuko ndo mshauri wako...

Sasa subiri huyo mchepuko wako aje akulalamikie kuwa mme wake hamshirikishi hapo ndo UKAE UKIJUA KUWA HATA MKEO ANASIKILIZWA AKITOA USHAURI KUSAIDIA FAMILIA YA MCHEPUKO WAKE.
 
Habari zenu wadau wa Jamiiforums.

Ni mara yangu ya kwanza kutuma ujumbe wenye maudhui kama haya hapa jukwaani.

Naomba mnipe ushauri jinsi ya kukabiliana na stress zinazonikabili.

Suala liko hivi; mwaka jana Oktoba mpenzi (mchepuko) wangu alipata mchumba akaja kuniuliza nikubali au nikatae asiolewe.

Mimi niliona sio vema kumkataza asiolewe maana mimi nina mke, lakini huyu mdada tulielewana sana, aliheshimu ndoa yangu sana, alikua mshauri mzuri mpaka kwenye masuala yangu ya kifamilia na kikazi.

Kuna wakati alikua akinishawishi nimuoe awe mke wa pili, lakini sikuwahi kuwaza kuwa na mke zaidi ya mmoja hivyo nilikataa, akasema sio shida anataka tuendelee kuwa wapenzi no matter what.

Sasa baada ya kumshauri akubali kuolewa, kweli jamaa mwezi Januari akaleta barua, kisha taratibu zote zikafuata.

Sasa leo ndio siku wapo wanafunga ndoa, kuna bonge la sherehe, dada zake (shemeji zangu) wamenipigia simu niende, rafiki zake wa karibu wa kazini kwao wamenipigia simu niende lakini moyo umeshindwa kabisa japo zawadi nilinunua nikampa rafiki yake akapeleka.

Wakuu huyu mwanamke ameolewa kwa ruhusa yangu lakini nimepata stress tangu juzi kila ninachofanya hakiendi, kila ninachoshika hakiendi, yaani nahisi kama akili zangu zimesimama kufanya kazi.

Nisadieni namna ya kukabiliana na hali hii ndugu zangu. Naomba msinitukane, msinihukumu wakuu, nisaidieni natokaje kwenye huu msongo wa mawazo.
watu wachache kama nyinyi na huyo mchepuko wako ndio mnafanya hii dunia watu waone ina machungu na kuchukia mapenzi wakati mwingine kuuana wewe badala ya kuachana naye kipindi yuko kwenye uchumba ulikua bado unaye kaolewa na bado utaendelea kuwa naye...huna aibu na akili watu kama nyinyi mnastahili kifo
 
lakini mbona ameonesha bado anaupendo kwa mke wake hilo haujaliona mpaka hata amekataa kumuoa huyo mwanamke.
hujamuelewa anachosema, ni kwamba wanaume mnasemaga mnachepuka kwa tamaa bila hisia lakini mleta mada ana hisia nzito sana juu ya mchepuko wake.

Ndo mjue wapo pia wanawake wanaochepuka bila hisia na mapenzi yanabaki kwa waume zao.
 
Pole sana kwa mkeo na kwa jamaa anayejichukulia bomu...

Unarudi nyumbani na stress, mkeo anakubembeleza akijua ni mambo ya kazi kumbe mchepuko kaolewa...

Jamani ndoa, ndoa hizi ndoa jamani!!!
This thing called marriage is just stupidity
 
Mmmh wanawake walio kwenye ndoa weng wanateseka jmn. Hpo hasira zote utahamishia kwa mke
 
Back
Top Bottom