Naomba ushauri: Mchepuko wangu ameolewa leo, nimekubwa na msongo wa mawazo

Naomba ushauri: Mchepuko wangu ameolewa leo, nimekubwa na msongo wa mawazo

Tofautisha kati ya tamaa na upendo ingekuwa ni tamaa tu asingeumia huyo mwanamke kuolewa ila kwa vile ni mapenzi ndo maana kaumia haijalishi kama bado anampenda mkewe au la hapo tatizo ni kwamba kampenda na mchepuko wakati mnasemaga huko nje huwa hampendagi
lakini mbona ameonesha bado anaupendo kwa mke wake hilo haujaliona mpaka hata amekataa kumuoa huyo mwanamke.
 
Wewe roho inakuuma kuona leo kuna jamaa anaenda kukesha pale unapopumzikaga.
Ni wivu tu huna stress hapo.

Stress ni hapo usikie mkeo anachepuka halafu hujamkamata na kumuuliza unaona jau kwa anavyokuheshimu.
 
Kuna mwingine anakaa hpo mtaa wa chin mchukue awe mshaur wako
 
wa kushauriwa na kuonewa huruma ni huyo aliyemuoa mkeo mdogo. maana lazima atalea watoto wasio wake, yaani watoto wako
 
Jianamke linakuganda ulioe ili litoe nuksi na kupigwa chapa ya married kumbe nyuma ya pazia limeishi kwa mapenzi makubwa na mwanaume mwingine tena hata kuachana ni basi tu haikuwa na namna, sasa hapo unategemea hiyo ndoa kudumu kweli!,
 
Nimekurupuka nikajua mkeo ndo anaolewa kumbe mchepuko.HAYA NI MATUMIZI MABAYA YA UANAUME.
Habari zenu wadau wa Jamiiforums.

Ni mara yangu ya kwanza kutuma ujumbe wenye maudhui kama haya hapa jukwaani.

Naomba mnipe ushauri jinsi ya kukabiliana na stress zinazonikabili.

Suala liko hivi; mwaka jana Oktoba mpenzi (mchepuko) wangu alipata mchumba akaja kuniuliza nikubali au nikatae asiolewe.

Mimi niliona sio vema kumkataza asiolewe maana mimi nina mke, lakini huyu mdada tulielewana sana, aliheshimu ndoa yangu sana, alikua mshauri mzuri mpaka kwenye masuala yangu ya kifamilia na kikazi.

Kuna wakati alikua akinishawishi nimuoe awe mke wa pili, lakini sikuwahi kuwaza kuwa na mke zaidi ya mmoja hivyo nilikataa, akasema sio shida anataka tuendelee kuwa wapenzi no matter what.

Sasa baada ya kumshauri akubali kuolewa, kweli jamaa mwezi Januari akaleta barua, kisha taratibu zote zikafuata.

Sasa leo ndio siku wapo wanafunga ndoa, kuna bonge la sherehe, dada zake (shemeji zangu) wamenipigia simu niende, rafiki zake wa karibu wa kazini kwao wamenipigia simu niende lakini moyo umeshindwa kabisa japo zawadi nilinunua nikampa rafiki yake akapeleka.

Wakuu huyu mwanamke ameolewa kwa ruhusa yangu lakini nimepata stress tangu juzi kila ninachofanya hakiendi, kila ninachoshika hakiendi, yaani nahisi kama akili zangu zimesimama kufanya kazi.

Nisadieni namna ya kukabiliana na hali hii ndugu zangu. Naomba msinitukane, msinihukumu wakuu, nisaidieni natokaje kwenye huu msongo wa mawazo.
 
Hivi wanaume si ndo mnasemaga hamchepuki kwa mapenzi bali mnachepuka kwa tamaa na mapenzi yanabaki kwa mke tu? Sasa wewe huyo mchepuko mbona inaonekana umempenda kabisa hadi unaumia yeye kuolewa? Ndo maana wake zenu hawataki na hawapendi mchepuke

Ila mnajitahidi kutafuta kila sababu ambazo hazina hata vichwa wala miguu za kutetea uzinzi wenu kumbe hamna lolote wote wale wale tu siku hizi hamna cha mwanaume wala mwanamke jinsia zote wapo ambao wakichepuka wanahamisha upendo na wapo ambao wakichepuka hawahamishi upendo tusidanganyane

Kuna kuchepuka ile mara moja moja (one night stand) hapo hamna feelings za mapenzi ila tamaa, na kuna ule mchepuko wa kudumu, huu kusema ukweli kuna mapemzi flani yapo hapo ndio maana tunahonga n.k ila mke anabaki kuwa mke hamna namna mwanaume atamchagua mchepuko wake badala ya mke ikitokea anatakiwa kifanya maamuzi
 
Habari zenu wadau wa Jamiiforums.

Ni mara yangu ya kwanza kutuma ujumbe wenye maudhui kama haya hapa jukwaani.

Naomba mnipe ushauri jinsi ya kukabiliana na stress zinazonikabili.

Suala liko hivi; mwaka jana Oktoba mpenzi (mchepuko) wangu alipata mchumba akaja kuniuliza nikubali au nikatae asiolewe.

Mimi niliona sio vema kumkataza asiolewe maana mimi nina mke, lakini huyu mdada tulielewana sana, aliheshimu ndoa yangu sana, alikua mshauri mzuri mpaka kwenye masuala yangu ya kifamilia na kikazi.

Kuna wakati alikua akinishawishi nimuoe awe mke wa pili, lakini sikuwahi kuwaza kuwa na mke zaidi ya mmoja hivyo nilikataa, akasema sio shida anataka tuendelee kuwa wapenzi no matter what.

Sasa baada ya kumshauri akubali kuolewa, kweli jamaa mwezi Januari akaleta barua, kisha taratibu zote zikafuata.

Sasa leo ndio siku wapo wanafunga ndoa, kuna bonge la sherehe, dada zake (shemeji zangu) wamenipigia simu niende, rafiki zake wa karibu wa kazini kwao wamenipigia simu niende lakini moyo umeshindwa kabisa japo zawadi nilinunua nikampa rafiki yake akapeleka.

Wakuu huyu mwanamke ameolewa kwa ruhusa yangu lakini nimepata stress tangu juzi kila ninachofanya hakiendi, kila ninachoshika hakiendi, yaani nahisi kama akili zangu zimesimama kufanya kazi.

Nisadieni namna ya kukabiliana na hali hii ndugu zangu. Naomba msinitukane, msinihukumu wakuu, nisaidieni natokaje kwenye huu msongo wa mawazo.
Muhadithie mkeo akupe ushauri
 
Dah!!!... Wanaume wenzangu mnazidi kumpa point 3 shetani..
Hivi kweli kabisa una ndoa yako halafu unakuja kuomba ushauri tukushauri kuhusu mchepuko wako, that means tunashiriki kuharibu ndoa yako indirectly...
Mi Nakushauri nenda kanisani kaombewe na utubu.. Umuombe sana Mungu akupe roho ya kumuogopa na kumuona kila ufikiriapo uzinzi...
Kisha nenda nyumban muite mkeo mwambie akae muangaliene Kama dakika mbili bila kukwepesha macho na muda huo ujisemee kimoyomoyo akusamehe Kwa kwenda kinyume na kiapo chenu... Ujumbe utamfikia maana nafsi zenu zitaongea kimyakimya... Kisha ukimaliza umpende mkeo...
Utahisi naongea ujinga... Ukiona Vipi potezea halafu endelea kuchepuka na mke wa mtu.. Ila ujue naww una mke..
Good morning
 
Hata kwa wanawake pia ni hivyo hivyo
Kuna kuchepuka ile mara moja moja (one night stand) hapo hamna feelings za mapenzi ila tamaa, na kuna ule mchepuko wa kudumu, huu kusema ukweli kuna mapemzi flani yapo hapo ndio maana tunahonga n.k ila mke anabaki kuwa mke hamna namna mwanaume atamchagua mchepuko wake badala ya mke ikitokea anatakiwa kifanya maamuzi
 
Hivi wanaume si ndo mnasemaga hamchepuki kwa mapenzi bali mnachepuka kwa tamaa na mapenzi yanabaki kwa mke tu? Sasa wewe huyo mchepuko mbona inaonekana umempenda kabisa hadi unaumia yeye kuolewa? Ndo maana wake zenu hawataki na hawapendi mchepuke

Ila mnajitahidi kutafuta kila sababu ambazo hazina hata vichwa wala miguu za kutetea uzinzi wenu kumbe hamna lolote wote wale wale tu siku hizi hamna cha mwanaume wala mwanamke jinsia zote wapo ambao wakichepuka wanahamisha upendo na wapo ambao wakichepuka hawahamishi upendo tusidanganyane
Shost eeh utajipa stress bureee,wengi wanaokoment humu nimegundua ni vitoto vya sekondari na vyuo,wanapass time to, that's y hata kushiriki minakasha humu nimepunguza kwa asilimia 90,nimeona ntajipa kisukari buleee kusoma ama kujadil mada za kisekondari kila leo
 
Hahahahah anataka tumfariji,kila Leo wanasema michepuko ni kwaajil ya tamaa,ni wa kutumiwa na kusepa,sasa sijui mwanaume huyu yamemsibu yepi ama yeye sio kama hawa wanaume wa jf ambao wanawatumia michepuko,wanapiga na kusepaaa?hahahah
Hahaha labda kajisahau kajua yuko Facebook. Amesahau kuwa wanaume wote wa Jf hawababaishwi na wanawake hata wakiachwa hawaumii sana sana wanakuwa wamepewa nafasi ya kuvuta chombo kipya, na hata wakitaka mchezo kutoka kwa ma ex wao ni fasta tu hata kama wameolewa. Mkaribishe mgeni Jf
 
Shost eeh utajipa stress bureee,wengi wanaokoment humu nimegundua ni vitoto vya sekondari na vyuo,wanapass time to, that's y hata kushiriki minakasha humu nimepunguza kwa asilimia 90,nimeona ntajipa kisukari buleee kusoma ama kujadil mada za kisekondari kila leo
Ni kweli aisee mimi siku hizi sijisumbui kubishana na mtu kwa facts, kama nitatoa fact basi ni kwa ufupi maana nimegundua kuna watu wapo kwaajili ya kutujaza upepo na mimi kujaa nimegoma
 
Hahahaaaahhahhaha stress za nini??? Si alikuomba umuoe mke wa pili uligoma??? Acha balaa relax
 
Back
Top Bottom